IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 44

 


SCENE 44: -

(Asubuhi nyingine iliyo ya kawaida kabisa, Christina anafika katika ofisi ya Mr. Bembele, Kama ilivyo kawaida anaingia bila kumsalimia mtu yeyote, anapita na kufika alipo Mr. Bembele)

Christina: habari yako

Mr. Bembele :( ananyanyua uso maana alikuwa ameinamia kitabu Fulani kisha anacheka kwa kejeli)

Christina: nimekusalimia

Mr. Bembele: nimesikia lakini je unahisi wewe unaweza kunisalimia mimi hivyo? Ndo maana Raymond anasema huna adabu (anacheka)

Christina: wewe si mpenzi wangu lakini?

Mr. Bembele :( anacheka sana, kisha anajizungusha kwenye kiti chake) umesahau? au umekuwa Raymond?

Christina: kafanyaje?

Mr. Bembele: kasahau…mambo mengi sana

Christina:(anajisemea moyoni) ushindi huo(anatabasamu)

Mr. Bembele: ila hatujui atakuwa hivyo kwa muda gani…au atakuwa anatudanganya

Christina:(anajisemea moyoni) hajifanyishi nimemtengeneza na nimehakikisha anakumbuka penzi letu na sio penzi la huyo housegirl

Mr. Bembele: umekuja kufanya nini Christina?

Christina: nataka turudiane

Mr. Bembele:au sio (anacheka) unataka yaani lazima? kwanini? ili iweje?

Christina: nakupenda…sana baby

Mr. Bembele:(anacheka sana) sikiliza Christina…it was a mistake my dear mimi wala sitaki kesi mimi na familia yangu tuko vizuri na sitaruhusu yeyote aharibu yote hayo, sitaki na wala sijisikii kurudiana na wewe nampenda sana mke wangu

Christina:(anatoa simu yenye meseji na picha walizokuwa wakipiga wakati wana mahusiano) nitamuonyesha mkeo kila kitu

Mr. Bembele:(anamuangalia kwa muda) are you blackmailing me?

Christina: nah baby nah (anamsogelea)…iam warning you…

Mr. Bembele:(anasikitika sana) maskini unahangaika…kweli…vipi huna hela?

Christina:(anapandwa na hasira)

Mr. Bembele: nakuuliza huna hela?

Christina: nataka kurudiana na wewe

Mr. Bembele: haiwezekani…na nipo serious…siwezi kumsaliti tena mke wangu hasa na wewe

Christina: naenda kumuonyesha hizi picha

Mr. Bembele: sitakuruhusu unichezee akili yangu kama unataka kumuonyesha mke wangu picha hizo sitakuzuia…unaweza kwenda tu ukamuonyesha

Christina:(anamshangaa)

Mr. Bembele: unatoa macho…nenda ukamuonyeshe hizo meseji…huna video ambazo zinaonyesha mimi na wewe tukiwa pamoja kitandani? kama unazo pia kamuonyeshe…

Christina:(anabaki anashangaa)

Mr. Bembele: sitakuruhusu Christina unipeleke kama ulivyokuwa unanipeleka sijui ulikuwa unatumia dawa…sijui nini (anakaa kimya kidogo) embu subiri kidogo…au ni wewe ndo umecheza na akili ya mwanangu…

Christina: hamna

Mr.Bembele:anyway…fanya utakavyo ila sitakuruhusu utuingilie mimi na familia yangu…tena,mke wangu ni mzee ndio ila nampenda sana mke wangu na kuhusu hizo picha kama unahisi hizo picha na meseji zitanivunjia ndoa umechemsha…nitamwambia kila kitu Glory wangu nitamuomba msamaha najua atakasirika siku mbili tatu ila hataniacha,yataisha ndo maana nimekuambia nenda peleka tena upeleke zote usipeleke nusu nusu kusanya zote ili kama unaenda kumwambia Glory umwambie ili nikikaa kumuomba msamaha iwe moja kwa moja na sio kila saa na kesi mpya

Christina :( kimya)

Mr. Bembele: nakuelewa Christina kuwa hutaki kupoteza zile raha tulizokuwa tunakupa Mimi na Raymond, najua tulikuwa tunakupa pesa unakula raha utakavyo, ila sasa maisha yanabadilika sana Christina…mimi ni wa Glory na Raymond ni wa Angelina

Christina:(anakumbuka maneno ya shangazi yake) Mhhh (anakumbukia maneno ya shangazi yake) Raymond ni wa Angelina na Bembele ni wa Glory waache mwanangu…wewe ni wa Peter… (anashusha pumzi)

Mr. Bembele: wewe uliwahi kuwa mtu wetu wa karibu sana ukiwa unaomba pesa tutakuwa tunakupatia tu

Christina:(anajisemea moyoni) siwezi kushindwa hivihivi…mimi sio wa kushindwa, nawataka wote wawili, nitafanya kila kitu mpaka muwe wangu tu

Mr. Bembele: wewe ni binti mzuri sana unajua…kwanini usitafute kijana tu mzuri akuoe

Christina:(machozi yanamlenga huku anamuangalia Mr. Bembele kwa hasira sana)

Mr. Bembele: now if you don’t mind naomba uondoke nina kazi nyingi nina kikao muda si mrefu

Christina: huwezi kuniacha hivihvi Desmond

Mr. Bembele: wow leo umeniita jina langu kabisaaaaa…halafu mbona kama unani command?

Christina: yaani umenichezea weee halafu unakuja kuniacha solemba?

Mr. Bembele: ndio kwani wewe ulijua mimi nitakuoa? ulidhani mimi Desmond baba yake Raymond naweza kumuacha Gloria mama yake Raymond na kukuoa wewe?

Christina:(anamuangalia) sio vizuri lakini

Mr. Bembele: sasa wewe sisi tukufanyeje? nimekuambia sisi hatutakuacha kila mara ukitaka msaada tuambie ila sasa naona huelewi unanilazimisha nikurudie yaani niachane na mke wangu nikurudie wewe embu acha zako hizo, halafu naomba uende bwana mimi nina kazi zangu na pia mke wangu atakuja muda si mrefu na pia tambua mwanaume yeyote hawezi kumuacha mkewe na kumuoa hawara my dear…sisi kutembea nje ya ndoa huwa tu ni tamaa zinatutesa and nothing more

Christina: nataka nimuone mkeo Desmond nataka kumwambia kila kitu

Mr. Bembele:(huku anacheka) karibu sana…keti msubiri Glory anakuja sawa ee

Christina:(anashangaa)

Mr. Bembele: kaa mbona bado umesimama

Christina:(anajisemea moyoni) mbona haogopi?

Mr. Bembele: najua unajiuliza sana ila ukweli ni kwamba yaani sikuogopi hata kidogo fanya utakavyo...sio mimi sio Raymond huwezi kutupata Christina nenda kwa waganga, walete hata kama umejaza lori zima mama hatutakuwa na wewe mama yangu…nilikuwa na wewe tu kama tamaa zangu mwenyewe na sio kwamba mke wangu ana kasoro yoyote hapana…kwanza mke wangu pamoja na uzee wote ule bado humfikii uzuri…unadhani au ulidhani naweza kabisa kumuacha mke wangu na nikakuoa wewe?

Christina:(anakasirika sana)

Mr. Bembele: nenda karoge…mama nenda mpaka kanisani ukaombewe…yaani kama umekosa mwanaume wa kukuoa basi piga maombi sana acha kunisumbua mimi na mwanangu…hatukutaki…(anafyonza)unakuja kunionyesha picha na kunitishia mimi ili nikutetemekee umechemsha wewe kama una shida sema usaidiwe lakini sio kuforce…na nina wasiwasi hata mwanangu ni wewe ndo umemfanyia hayo yote ili akukumbuke wewe tu…jiandae kwa mshangao mama (anacheka sana) get ready christina mdada mrembo usiyejua kujishughulisha kazi kuvizia wanaume za watu wanawake sasa hivi hawako tena huko chez ahata upatu basi ujikwamue uache kuhangaika na waume za watu.embu nenda zako bwana

Christina:(anatoka nje kwa hasira)

Mr. Bembele: njoo umsubiri Glory yupo njiani anakuja (anacheka sana)

Christina:(anatoka nje na kuelekea alipoegesha gari lake) shit!!!mbona nimefeli mimi…sijaweza kumshawishi huyu mzee arudiane na mimi… (anashusha pumzi) lakini hapana nisikate tamaa bado nina Raymond (anacheka)maskini basi kajua ameniweza…nina Raymond baada ya muda Raymond atakuja kunioa (anacheka)mali zote za huyu mzee zitakuwa zangu...(anacheka)

(Gari la Mrs. Bembele linakuja, linaegesha karibu na gari la Christina, kisha Mrs. Bembele anashuka akiwa amependeza kwelikweli, ama hakika mama yake Raymond ni mrembo bwana na anastahili sifa zote)

Christina: kile kibibi kizee(anafyonza)kibayaaa!!(anapanda gari kisha analiondoa kwa mwendo wa kasi sana)

Post a Comment

0 Comments