IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 45

 


SCENE 45­: -

(Asubuhi ya siku kama ya tatu baada ya Christina na Mr. Bembele kukutana ofisini, Raymond anafika nyumbani kwa kina Christina, kama kawaida anakaribishwa na mama yake Christina ambae mara nyingi sana anapenda kukaa sebuleni akiangalia runinga)

Mama: karibu mwanangu

Raymond: asante mama, shikamoo

Mama: marahaba baba

Raymond: sijakuona siku nyingi kweli jamani umepotelea wapi?

Mama:(anaguna) Ray baba siku nyingi kama muda gani?

Raymond: mwaka na kitu hivi

Mama:(anacheka) masihala hayo baba…sisi tumeonana mara ya mwisho juzi tu hapa…

Raymond:(anaguna)

(shangazi anakuja mahali hapo)

Shangazi:( kwa Raymond) hujambo baba…

Raymond: sijambo mama shikamoo…(anamshangaa)yaani na wewe umepotea kweli shangazi

Mama:(anashangaa) yaani sijui kawaje huyu jamani…eti anasema mimi hajaniona mwaka

Shangazi:(anacheka) utamuweza huyu kwa vituko (anajisemea moyoni) kumbe kweli Christina kamfanyia vibaya mtoto wa watu(anaguna)

Raymond: yaani mimi ndo siwaelewi…lakini sawa Christina yuko wapi?

Mama: chumbani kwake…wewe muone tu

Raymond:(anaelekea chumbani kwa Christina cha kushangaza anaenda chumba alichokuwa anatumia Christina zamani)

Shangazi:(anamfuata) sio huko baba (anamuonyesha Christina alipo)

Raymond: amehama?

Shangazi:(anatabasamu) ndio amehama

Raymond:(anaingia chumbani kwa Christina)

Christina:(amekaa kitandani akiwa katika pozi la mitego) karibu mpenzi

Raymond: asante Christina…

Christina:(ananyanyuka na kumfuata aliposimama na kumkumbatia)

Raymond:(harudishi badala yake anamtoa kwa upole) Christina sikia kuna kitu nataka kukuambia

Christina: utaniambia baadae...kwa sasa nipe nafasi mpenzi wangu nikuonyeshe mambo mazuri

Raymond: No... (anamsukuma kidogo) kuna kitu nataka nikuambie please nipe nafasi...niongee

Christina: najua unataka kuniambia ni jinsi gani unavyonipenda baby…najua

Raymond: hapana Christina sitaki kukuambia hivyo

Christina: ila?

Raymond: sikia (anashusha pumzi) najua tumetoka mbali sana katika penzi letu…

Christina: ndio najua…

Raymond:na tambua kuwa sio kila penzi huishia kwenye ndoa

Christina: una maana gani?

Raymond: wazazi wangu wamenichagulia mchumba wananiambia kuwa nilimvalisha pete ya uchumba na kwamba mimi ndo nilimchagua mwenyewe…ukweli ni kwamba mimi sikumbuki chochote Christina

Christina: kama hukumbuki chochote basi hukumvalisha pete wanakudanganya hao…wazazi wako

Raymond: hiyo sijui…ninachojua mimi ni kwamba nampenda huyo binti sana…nisamehe tu Christina yaani nampenda kupita kiasi, yaani sijui nikuambieje...nampenda sana yaani ananivutia sana

Christina:(anakasirika sana)

Raymond: nielewe Christina najua sipaswi kukuambia hivi wewe ni mpenzi wangu wa siku nyingi sana…lakini kwa mapenzi nayoyahisi juu ya huyo binti haki ya Mungu tena nimejitoa mhanga itakavyokuwa naiwe tu

Christina: that is not fair Raymond mimi ni mpenzi wako kwanini unaniambia maneno hayo?

Raymond: ndo maana nimekuomba msamaha kwanza jamani nisamehe mwenzio...

Christina: get out

Raymond: usikasirike Christina...nampenda sana Angelina na nipo tayari kumuoa…

Christina: toka nje

Raymond:(anatoka) nielewe

(anafika sebuleni)

Mama: baba mbona mnagombana na mwenzio?

Raymond: mama kwani ni kosa kumpenda mtu?

Mama: sio kosa baba kwani nini?

Raymond: anyway, tuyaache hayo mama… (anaondoka zake)

Shangazi:(anaenda alipo Christina) imekuwaje?

Christina:(akiwa anatokwa machozi) wewe mwanamke ni mchawi

Shangazi: una maana gani?

Christina:(Analia)

Shangazi: kwanini unaniita mchawi?

Christina: umefanya nini?

Shangazi: nimefanya nini kwani?

Christina: umeenda kuipindua dawa yangu

Shangazi:(anacheka kidogo) imegoma?

Christina:(anamuangalia shangazi yake kwa hasira)

Shangazi:shoga yangu haijagoma…wewe  huoni Raymond anakumbuka tu vitu vilivyotokea miaka miwili iliyopita,miaka miwili iliyopita mlikuwa katika mapenzi motomoto,miaka miwili iliyopita hakumuona mama yako kama mwaka mzima na  ndo alichomuambia hapo…mpaka mama yako ameshangaa..hiyo dawa uliyoitengeneza kurudisha matukio nyuma kwa Raymond wala haijadunda ila…moyo wa Raymond umempenda Angelina kupita kiasi yaani anachotumia Raymond kwa sasa ni moyo…najua Angelina anashangaa haelewi nini kinaendelea anamuona mtu hakumbuki hiki wala kile ila anampenda…ni moyo mama…pole sana tangu mwanzo wewe na Raymond hamkuwa wala hamkupangiwa kuwa ni sisi t undo tulikuwa tunapanga ila kwa sasa Mungu ameona imetosha

Christina: nimemlipa pesa nyingi sana huyo mganga nilijua Raymond leo kaja turudishe penzi letu…nilipanga leo akija nitabeba mimba yake

Shangazi: pole mipango yako haijatimia ila huo ndo ukweli wa mambo na ni jukumu letu sote kulikubali na kulitii

Christina: nitamfanyia kitu mbaya angelina…mpaka atajuta

Shangazi: hata iweje Christina huwezi kuwatenganisha wale watu

Christina: naweza…ninaweza (kwa ukali Zaidi) nimesema naweza mimi ndo Christina sishindwi kitu

Shangazi: hushindwi kitu umekuwa Mungu wewe?

Christina :( anamuangalia shangazi yake kwa hasira) toka nje

Shangazi :( anatoka)

Christina :( Analia kwa hasira sana) yaani Raymond anakuja kuniambia kuwa hanitaki tena? pamoja na kufanya yote yale…(anafyonza)ngoja nimpigie yule mganga (anachukua simu kisha anapiga)

(simu inaita)

Mganga:(anapokea) hallo…

Christina: rudisha pesa yangu…wewe mwizi dawa haijafanya kazi

Mganga: labda ulikosea masharti (anakata simu)

(Christina anabaki amekasirika na Analia Sana)

Post a Comment

0 Comments