IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 46

 


SCENE 46: -

(Raymond na Angelina wapo nyumbani kwa Raymond)

Raymond:(anacheka) yaani huwezi amini ila nakupenda kwa mambo mengi sana…napenda una heshima sana, unajua kupika, unajua kupanga bajeti vizuri, na Zaidi unaonekana unanipenda sana…

Angelina:(anamuangalia kisha anatabasamu)

Raymond: mi nimechoka kusimama twende sebuleni

(Wanaenda sebuleni)

Raymond :( anampakata)

Angelina :( anajisemea moyoni) yaani huyu amesahau mambo mengi…nashangaa hajasahau kuwa mimi nay eye tunapendana sana

Raymond: mbona huongei…?

Angelina: wala sina usemi mimi nakusikiliza wewe

Raymond: unajua mwenzio sijui ninakuwaje yaani nimesahau kila kitu…hivi nimeshakutolea mahari eeh

Angelina: hapana bado…

Raymond: inabidi nimwambie baba ili twende tukatoe mahari mpenzi wangu yaani natamani nikuoe haraka uwe mke wangu

Angelina; unajua kabisa kuwa hata mimi natamani kuwa mkeo mpenzi

Raymond: twende tukaoane tutoroke(anacheka)

Angelina:(anacheka) tutauliwa

Raymond:ni kweli…sasa naomba nimpigie simu Edmond aje sasa hivi…

Angelina: unakumbuka kuwa Edmond ni rafiki yako?

Raymond:(anacheka) jamani Edmond ni rafiki yangu tangu tuna miaka 20…mpaka leo nina miaka 30

Angelina:(anajisemea moyoni) kasahau kuwa ana miaka 32…karudi miaka miwili nyuma

Raymond:(anamshika Angelina kidevu) yaani nakupenda wewe…ona ulivyo mzuri jamani

Angelina:(anacheka) asante hata mimi nakupenda sana na unajua hilo

(wanabusiana)

Raymond: ngoja nimpigie simu Edmond…aje (anapiga simu)

(simu inaita)

Edmond:(anapokea) hello

Raymond: mwana mpotevu

Edmond: (anashangaa) tangu lini mimi nikawa mwanampotevu?

Raymond: sijaongea na kukuona siku nyingi sana

Edmond: acha masihala…si tumeongea jana tu?

Raymond :(anashangaa sana)

Edmond: (anabaki anashangaa)

Raymond: anyway…tuachane na hayo…kuna dada mmoja wazazi wangu wanasema kuwa nimemchagua mwenyewe ila ukweli ni kwamba mimi sijamchagua yaani sikumbuki, ila Mond nampenda huyu dada uwiii yaani sijui nikwambieje

Edmond:(anaguna) inamaana umempenda demu mwingine mbali na Angelina?

Raymond: anaitwa Angelina

Edmond:(anashangaa sana) unajua masihala yako mimi huwa siyapendi yaani unaleta masihala mpaka kwenye mambo muhimu

Raymond: una maana gani nakutania Mond?

Edmond: huyo demu ni shemeji yangu na wewe umempenda muda mrefu sana mara baada ya kuishi nae hapo kwako alikuja kama housegirl

Raymond:(anashangaa) hausigeli tena?

Edmond: ndio na ni mimi ndo nilikuletea (anacheka)yaani dokta Raymond bwana kwahiyo unaniletea masihala mimi?

Raymond: dokta Raymond tena?

Edmond: ndio wewe dokta

Raymond: najua hiyo ni ndoto yangu ila bado sijawa dokta…nitamaliza baada ya miaka miwili, nasoma bado kwanza nilitakiwa kuwa india nashangaa nipo tanzania

Edmond: Raymond una nini?

Raymond: kwani vipi? nawashangaa wote mnanipeleka mbele miaka miwili...mara wengine wananiita dokta…nimeenda kwenye ofisi Fulani yaani kila mtu dokta…dokta yaani mnanichosha

Edmond:(anashangaa sana) jamani

Raymond: anyway…tunatakiwa kupeleka mahari kwa mchumba wangu

Edmond: tumeshapanga mimi, wewe na mama yako

Raymond: saa ngapi?

Edmond: ulifanyaje ulipoenda Serengeti?

Raymond: mimi sijawahi kwenda Serengeti ingawa natamani sana kwenda kupumzika na mpenzi wangu yaani mwanamke nitakayemchagua mwenyewe…kama Angelina, nitaenda na Angelina…by the way nimeshaachana na Christina yaani nilipomuambia amekasirika ila nikamwambia mimi nimeamua kama ana hasira sana basi agalegale

Edmond:(anacheka kidogo) unajua wewe uliachana na Christina siku nyingi sana lakini sawa…nitakuja huko

Raymond: karibu…sana uje umuone Angelina

Edmond: namjua

Raymond: haina shida njoo umjue tena

Edmond:(anakata simu) jamani

Catherine:(anamtengea chakula) nini? maana ulikuwa unashangaa tu muda wote mnaongea na Raymond kuna nini?

Edmond: kuna tatizo

Catherine: lipi tena?

Edmond: Raymond hayuko sawa…

Catherine: kivipi? (anakaa)

Edmond: amepoteza kumbukumbu…yaani hakumbuki kabisaaaa chochote kilichotokea hivi karibuni yaani akili yake imerudi miaka kama miwili nyuma

Catherine: wewe Edmond inawezekana vipi hiyo?

Edmond: sijui…labda kuna sehemu amejigonga vibaya kichwani

Catherine:(anashusha pumzi) yaani Angel sijui itakuwaje

Edmond: cha kushangaza anampenda sana Angelina

Catherine: yaani hiyo inachanganya…

Edmond: aha!!kuna kitu nakumbuka juzi mama yake aliniambia kuwa Raymond hayupo vizuri

Catherine: kwa mantiki hiyo wampeleke hospitali?

Edmond: ngoja kesho nitaenda ili nimuelewe vizuri maana hata simuelewi kabisaa

Catherine; kwahiyo hakumbuki hata kwamba mlikuwa marafiki

Edmond: tangu naanza urafiki na Raymond huu ni mwaka wa 12 na yeye akili yake imerudi miaka miwili nyuma na wala simuelewi

Catherine:(anakula chakula kidogo) yaani dunia ina mambo hii(anaguna)

Edmond:(anaguna) kuna nini hapo?

Catherine: sijui ndugu yangu atakuwa anaendeleaje huko? na penzi lao ni la muda mfupi lakini limepitia mambo mengi

Edmond; sana…ila watavuka maana kuna upendo wa dhati kati yao (anatafakari kitu)

Post a Comment

0 Comments