IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 47

 


SCENE 47: -

(Mchana mwingine wa siku nyingine tena tulivu sana, kuna jua la kawaida na hali ya hewa iko sawa kabisa, muda ni majira ya saa saba, Christina anaegesha gari lake mbali kidogo na nyumba ya Raymond, hatoki ndani la gari badala yake anayaangalia mazingira yale kwa mbali)

Christina:yaani nimejisumbua nimeenda mpaka kwa mganga ili kumpoteza akili Raymond akumbuke tu mapenzi tuliyokuwa nayo badala yake karudi palepale kumpenda huyo kijakazi mnuka mikojo…mimi ni mzuri kuliko huyo Angelina…tena ni mzuri mbali sana mimi nafaa kuolewa na Ray kwanza tunaendana(anafyonza)huyu mjinga kaja kuniharibia ndoto zangu..mimi niliumbiwa kuishi maisha mazuri na mwisho wa siku natakiwa kuishi hayo maisha na hakuna mwenye mamlaka ya kuishi maisha niliyoyaota…ni kweli nampenda sana Peter ila Raymond ndo mwanaume pekee atakayenipa maisha nayoyataka

(Angelina anapita akiwa anatokea sokoni)

Christina: ona anavyojifanya wife material…(anafyonza)namkanyaga namtoa utumbo leo mshenzi huyu… (anawasha gari na kwa mwendo kasi analiondoa gari na kumfuata Angelina)

Angelina:(analiona gari linakuja kwa kasi sana anapiga kelele) mama…

Raymond:(amesimama karibu na geti anatoka anakimbia) nini?

Christina:(anakanyaga breki na kulisimamisha gari ghafla)

Angelina:(anaogopa sana)

Christina: shenzi sana…nitakuua una bahati sana huyo bwana wako ametoka kwa wakati ningekutoa utumbo…(analirudisha gari nyuma kisha anaondoka)shit!!!Raymond anampendea nini huyu mshenzi (anafyonza)yaani anataka kumuoa halafu mimi ameniacha pamoja na juhudi zote nazofanya ili kumfanya awe mume wangu lakini ameona aniache(anaendesha gari kwa hasira)lakini mimi ndo Christina…nisipoolewa na Raymond nitaolewa na Desmond yaani hawa baba na mwana nina usongo nao hawa hawajui tu…na siwaachii hivihivi nitamroga Desmond kama nilivyomroga Raymond lakini dah Raymond nimemroga imebuma yaani ana mizimu mikali huyu(anaendelea na safari)

(upande wa Raymond na Angelina)

Raymond: nini wewe mbona huongei?

Angelina: lile gari lililoondoka hapa lilitaka kunigonga

Raymond:ni la nani unamjua?

Angelina: hapana simfahamu…

Raymond: sasa mbona alitaka kukugonga kama ana uadui na wewe?

Angelina: mimi sijui dear…

Raymond:(kwa Ramadhani) wewe kaka…umeliona hili gari na labda unalijua?

Ramadhani: gari gani boss?

Raymond: halafu usiniite boss bwana

Ramadhani: mi nimeona umesahau ndo maana nikaanza kufanya Kama nilivyokuwa nafanya zamani

Raymond: kufanya nini?

Ramadhani: kukuita boss

Raymond: naomba usiniite boss…yaani sipendi Sana

Ramadhani: najua hupendi…

Raymond: umejuaje

Ramadhani: ndivyo ulivyo siku zote boss

Raymond: anyway sawa…by the way umeliona hilo gari?

Ramadhani: gari gani boss

Raymond: lililotaka kumgonga mke wangu?

Ramadhani :( analikumbuka) lile (anajisemea moyoni) si la Christina lile na aliyekuwa anaendesha ni Christina

Raymond: mbona hunijibu, Rama?

Ramadhani: sasa boss wangu mimi nitajuaje huku wote tulikuwa ndani tumetoka tu mara baada ya kumsikia Angelina anapiga kelele

Raymond: nina uhakika ulimuona hata kwa mbali…maana hata mimi nimemuona ila sijamtambua

Ramadhani: sasa wewe boss hujamuona vizuri mimi ndo naanzaje kumuona vizuri…

Raymonda: anyway, tuachane na haya…kikubwa kwamba wife hajaumia…ungeumia na mimi ningeumia sana… (Kwa Angelina) twende ndani mpenzi

Ramadhani: wacha we…

Raymond: naomba unitafutie msichana wa kazi huyu anatakiwa apumzike awe wa kukaa ndani…

Ramadhani: usijali boss ake…nitakuletea msichana nitamtoa kijijini kwetu

Raymond: sawa utakuwa umenisaidia sana… (Kwa Angelina) kabla hajaja huyo binti nitakuwa nakupeleka mimi na kukurudisha kila unapotaka kwenda popote mpenzi maisha yako hayako salama kabisa mpenzi

Angelina: unatakiwa uwe unaenda kazini

Raymond: sawa...Najua mama na baba wameniambia niende hospitali ila mimi sio dokta…bado

Angelina: dear…wewe ni daktari tayari mbona muda sana tangu umekuwa dokta

Raymond: Kama unaniambia wewe labda naweza kuwa ni daktari kweli

Angelina: wewe ni daktari na ni mchumba wangu

Raymond: nafurahi kuwa mchumba wako baby

Raymond: wow…Nina bahati Sana kuwa na mchumba mzuri kama wewe

Angelina: Asante dear

Ramadhani :( anaguna) mapenzi shatashata… (Anaguna tena)

Raymond: twende ndani… (kwa Ramadhani) usisahau na dereva maana mimi nitakuwa naenda kazini sitaki ataembee kwa miguu utasema sio mke wa Raymond Desmond Bembele

Ramadhani: sawa boss…nitawatafuta

Raymond: nikupe siku ngapi…maana nataka kuanza kufanya kazi mwenzio…

Ramadhani: mfanyakazi hata ukinipa hela leo kesho anakuja

Raymond: poa muite basi…aje na awe ana tabia nzuri

Ramadhani: sawa boss wangu

Raymond: niite Raymond

Ramadhani: sawa Raymond

Raymond :( anacheka) haya endelea na kazi zako sasa

Ramadhani: sawa Raymond…

(Raymond na Angelina wanaingia ndani)

Angelina:(anaingia ndani huku anajisemea moyoni) Raymond anajitahidi kunipoteza mawazo ya mimi kunusurika kifo ila ukweli ni kwamba siwezi kusahau na ni nani alitaka kuniua leo kwa kunigonga gari? je ni Christina labda kwasababu ya wivu au ni nani? (anaguna)hii nalo ni janga na ninatakiwa kuwa makini sana

Raymond :( amemshika mkono Angelina) vipi mbona umepoa?

Angelina: wala, mi mbona nipo sawa tu?

Raymond: nakupenda Sana Angelina natamani nikuoe hata sasa hivi

Angelina :( anacheka) hata mimi natamani hata sasa hivi niwe mkeo

Raymond: nitaenda kutoa mahari mpenzi, sijawahi kupenda mwanamke Kama navyokupenda wewe, sijui umenipa nini

Angelina: (anacheka) Raymond bwana, sawa ILA familia yangu itakukaribisha kwa mikono miwili na pia hata mimi sijawahi kupenda mwanaume kama navyokupenda wewe

Raymond: eti ee

(Wanacheka kisha wanaingia ndani)

Ramadhani: maisha haya…hausigeli anatafutiwa hausigeli… (Anaguna) kimasihara Angelina kampiku Christina (anacheka sana) sasa hausigeli kawa ‘mazahausi’ duh!!!dunia ina mambo hii…ila Raymond kama kachanganyikiwa

Post a Comment

0 Comments