IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 48

 


SCENE 48: -

(Edmond pamoja na Catherine wanafika nyumbani kwa Raymond wakiwa na shauku ya kujua yaliyomkuta Raymond kuhusu yeye kupoteza kumbukumbu na mambo mengine)

Edmond:(anagonga hodi)

Angelina:(anafungua) karibuni (huku anapiga magoti) shikamoo shemeji…

Edmond: marahaba…shem hujambo

Angelina: sijambo (kwa Catherine) shikamoo dada

Catherine: marahaba hujambo

Angelina: sijambo…karibuni (anawaongoza njia) karibuni

Edmond: asante…simuoni Mond….

Angelina: yupo sebuleni…

Edmond:(anaelekea sebuleni)

Raymond:(amelala)

Edmond:(anamuamsha) wewe vipi unaumwa…

Raymond:(anashtuka) ah…(anakaa)nambie

Edmond: wewe umekuwaje? mbona hata kazini huendi?

Raymond:mi bado mwanafunzi bwana…yaani Angelina ameshinda siku nzima ananiambia kwamba mimi ni daktari na inanipasa niende kazini yaani simuelewi unajua

Edmond: una shida gani Raymond kwanini kama akili yako imebaki nyuma sana...kuna mambo mengi sana yametokea…wewe tayari umeshamaliza elimu yako na tayari wewe ni daktari…baba yako kakupa ofisi wewe ndo daktari mkuu, na pia umepewa nyumba gari ina maana hukumbuki vyote hivyo?

Raymond: sina kumbukumbu

(Angelina na Catherine wanafika mahali hapo)

Edmond: nini kilikutokea wakati upo Serengeti?

Raymond:(anamuangalia usoni) Serengeti nilienda lini?

Angelina:(anasikitika)

Edmond:(kwa Angelina) nini kilitokea wakati mpo Serengeti?

Angelina: hamna kitu shem…tulikaa huko tukafurahia maisha na wala hakuna ambacho kilikuwa kimeharibika wala kuonekana kuharibika…tatizo lilianza kesho yake mara baada ya sisi kurudi ndo nikawa nikimpigia simu hakumbuki mimi ni nani na pia dada pendo na Rachel na wao wakasema hawamuelewi asubuhi alienda vizuri ila mchana eti akawasahau

Edmond:au kachezewa maana kama hakujigonga sehemu...na kama ingekuwa hivyo angeumwa kichwa

Catherine: atakuwa amerogwa

Edmond:na nani lakini?

Catherine: inaweza ikawa mtu labda anayetaka akumbuke mambo ya nyuma ili labda awe karibu nae

Edmond: Duh hii mpya na hatari kwa mantiki hiyo mtu pekee ambae anaweza kumfanyia hivyo Mond ni Christina ndo ambae anatamani kuwa na Raymond na yuko tayari kufanya chochote ili ndoa iliyokuwa ikisubiri itimie…yes ni Christina inaleta maana…

Catherine: cha kushangaza sasa pamoja na yote mbona Raymond anataka kumuoa Angelina?

Edmond: moyo…kilichotumika ni moyo

Raymond; yaani hata siwaelewi mnajua…

Catherine: tumuite mchungaji...amuombee huyu mtu la si hivyo atakuwa kichaa mnaonaje?

Angelina:ni kweli

Edmond:ni kweli ni mchungaji pekee ndo ataweza kutatua hili au tumpeleke kwanza hospitali

Angelina: wazazi wake walitaka wampeleke hospitali ila sijui ikawaje

Edmond: labda na wao wameona kuwa itakuwa ni nguvu za giza ndo zimefanyika hapa

Catherine: labda

Raymond: Mond…bora umekuja ndugu yangu tunaenda lini kwa ndugu zake huyu mrembo nimuoe mimi fasta

(Catherine, Edmond na Angelina wanaangaliana)

Edmond: tutaenda tu Mond

Raymond: haya mimi nalala bana… (ananyanyuka na kwenda zake ndani)

Edmond:au anajifanyisha

Catherine: ili iweje? huyu kweli amepoteza maana hata alivyo hayupo kawaida kabisaaa

Angelina: yaani mimi nimeshachanganyikiwa

Edmond: wala hata usijali Mungu yupo…

Catherine: Christina nae ni king’ang’anizi yote kamuharibu mtoto wa watu ilia pate hiyo ndoa jamani hajui kuwa ukiachwa inabidi uachike?

Edmond: yaani hachoki ameshawahi kusingizia mpaka mimba ili ampate Raymond sasa Raymond mwenyewe alivyo mtata (anaguna)

(Wanacheka)

Catherine: atakuwa poa tu siku sio nyingi…

Angelina: unajua yaani inashangaza mtu mlikuwa nae vizuri tu jana yake eti leo hakumbuki kitu kabisa…yaani mara ya kwanza alienda kwao akalala, akarudi kesho yake yaani akawa hata anikumbuki

Catherine: ila akawa anakupenda

Angelina:ee…yaani mpaka nikashangaa

Edmond: moyo…mama yaani na amekupenda…pamoja na kwamba kichwa chake hakikukumbuki ila moyo wake unakumbuka kuwa uliwahi kukupenda na bado anakupenda

Catherine: una bahati binamu

Angelina:(anacheka)

Edmond:(kwa Catherine) kama ninavyokupenda wewe

Catherine:(anacheka)

Edmond: kabla hamjafunga ndoa wewe na Raymond mimi na Catherine tutafunga ndoa…kila kitu tayari mpaka siku ya ndoa imeshapangwa…

Angelina:(kwa Catherine) hongera binamu

Catherine: asante…(anatabasamu)

Edmond: sema ndo hivyo mshenga wangu ndo kachanganyikiwa hana hata kumbukumbu na suala la kukutolea mahari wewe Angelina lilikuwa limepangwa kimyakimya

Catherine: dah…Christina katuharibia kweli maana ungeshangaa send off tu, yaani kila mtu alikuwa amejipanga mahali pake sio baba yake Raymond na ukali wake ule na sio mama Raymond na ule upole wake

Angelina:(anacheka) jamani

Catherine: ila usijali kila kitu kitakaa sawa wewe shukuru tu kuwa bado upon ae basi mengine mkabidhi Mungu atakutendea

Angelina:(anatabasamu) amina

Catherine: wewe nae tumekaa hapa muda wote jamani hata maji…Loh!!

Angelina: jamani nimesahau

Edmond:(anacheka) anamuawaza baby…baby mwenyewe sasa kulala…utasema kalogewa hapo

Catherine: anapenda kulala ee

Angelina: vibaya sana (anaenda jikoni na baada ya sekunde kadhaa anakuja amebeba glasi za juisi na maji anawapa Catherine na Edmond kisha nay eye anachukua moja)

Edmond: atakaa vizuri tu usijali

(Wanakunywa vinywaji huku wanaendelea na maongezi ya hapa na pale)

Catherine: Muamini Mungu mdogo wangu

Post a Comment

0 Comments