IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 49

 


SCENE 49: -

(Majira ya saa saba usiku Christina anafika nyumbani kwa mganga aliyemtengenezea dawa ya kumpoteza kumbukumbu Raymond)

Christina:(anagonga kibandani) uncle

Mganga:(anaamka) naam… (anafungua mlango) wewe nini usiku huu

Christina: nina mazungumzo na wewe

Mganga:(anatoka) sasa ndo uje usiku? (anatoa kiti nje) haya karibu uketi (anapiga miayo) ah yaani ni usiku kweli

Christina:(anakaa)

Mganga: enhe niambie

Christina: ah…sina mengi ya kukuambia

Mganga:(anamsikiliza kwa makini)

Christina: naomba ile dawa uitengue

Mganga:(anamuangalia usoni) kwanini?

Christina: ah haijafanya kazi kama nilivyo tegemea

Mganga: kivipi?

Christina: yaani hata hanipendi kama ilivyokuwa bado anampenda yule dada niliyekuambia

Mganga:(anacheka kidogo) ila mimi si nilikuambia?

Christina:(kimya huku anaangalia chini)

Mganga: yeye na yule dada wanapendana kweli…na hata tukifanyaje wataishia pamoja

Christina:(anaangalia chini) yaani nimepoteza muda…na mimi nimegundua kuwa wanapendana ingawa inaniuma sina budi kukubaliana nalo...na mimi naogopa kuishia vibaya anko

Mganga: ndo hivyo…usije ukaishia vibaya mwanangu...

Christina:(anavuta pumzi ndefu) mimi na Raymond tumetokea mbali sana

Mganga: najua…na mara nyingi ulikuwa ukigombana nae unakuja nakutengezea mnapatana

Christina: ila sasa huyu msichana wake wa kazi amekuja kupoteza kabisa uwezekano wa mimi nay eye kuwa pamoja isije ikawa kesi naomba tu uitengue…najua inauma kumkosa Raymond

Mganga: kwani unampenda sana?

Christina: hapana...nimemzoea tu

Mganga: basi mpe nafasi aishi maisha yake maana hata yeye anajua kabisa kuwa wewe humpendi hata kidogo nan do maana mara nyingi alikuwa anakukwepa na alipopata nafasi ya kupenda amependa kwa moyo wake wote na akili yake yote inamfikiria huyu mwanamke

Christina: naelewa anko kuwa anampenda sana msichana wake wa kazi

Mganga: ngoja tuitengue dawa (anaingia kibandani mwake na baada ya dakika kama kumi anatoka akiwa na vifaa vyake kama vibuyu n.k) sasa tuanze kazi…kwanza zile nywele tulizochimbia tuzifukue…tuzichome moto

Christina: sawa

Mganga: fanya wewe maana hata mara ya kwanza ulifanya wewe

Christina:(anachukua jembe lililopo pembeni yake na kufukua nywele za Raymond)

Mganga:(anaongea maneno Fulani kwa sauti ya kunong’oneza)

Christina:(anachukua nywele za Raymond na kuzitupa mbali)

Mganga :( anaongea lugha za kiganga huku anataja jina la Raymond)

Christina:(amesimama kinyonge)

Mganga:(anamalizia kwa kuvunja chungu alichopikia dawa na kumwaga dawa waliyompulizia Raymond siku wanampoteza kumbukumbu)

(upande wa Raymond, amelala kitanda kimoja na mpenzi wake lakini ghafla anasisimuka mwili na kupiga kelele ya ajabu, inayomshtua Angelina)

Angelina:(anakemea kwa jina la Yesu kristu wa Nazareth)

Raymond:(jasho linatiririka)

Angelina: asante bwana Yesu (kwa Raymond) ni nini?

Raymond:(anatulia) sijui…(anamkumbatia)malaika

Angelina:(anakumbuka kuwa ni jina alilokuwa anapenda kumuita) hili jina si alikuwa ananiita kabla hajapoteza kumbukumbu

Raymond:(anacheka) kwani bado tupo Serengeti?

Angelina: kwanini?

Raymond: tumelala wote

Angelina: asante bwana Yesu amekumbuka…

Raymond: nini?

Angelina: hapana tumesharudi nyumbani

Raymond: nakupenda Sana Angelina

Angelina: nami nakupenda Sana Raymond…hatimaye umekumbuka

Raymond: kwani nilikuwa nimesahau?

Angelina: acha tu…tulale nitakusimulia kesho asubuhi

Raymond: yaani nimetoka jasho utasema nilikuwa nalima

Angelina: pole Mungu wetu hashindwi

Raymond: hakika…

(wanajifunika kisha wanalala)

Raymond: bwana nimekuambia nasikia joto

Angelina: pole (anamfunua)

Raymond:(anasinzia)

Angelina: lala…

(upande wa Christina na mganga)

Mganga: basi kwa kufanya hivi huko alipo anaweza akawa amesharudisha akili na kumbukumbu zake

Christina: asante sana

Mganga: kwa mara ya kwanza tangu nimejua kufanya dawa sijawahi kuona mwanamke mwenye busara kama wewe

Christina: kwanini?

Mganga: hii dawa ni kali sana, siku ingebuma ungekuwa chizi

Christina: nimshukuru shangazi yangu ambae yeye ndo alinikaribisha katika ulimwengu wa dawa lakini yeye ndo amekuwa chachu ya mimi kujitoa kwenye huu ulimwengu…aliniambia hasara za kung’ang’ania ambapo hakuna mapenzi nilitafakari sana nikaona ni kweli ndo maana unaona leo nimekuja kutengua dawa na kumuacha huru. Raymond alipenda sana pamoja na kwamba tumeachana basi tuwe marafiki ila mimi nikaona itakuwa hasara kwangu Raymond akiwa rafiki tu

Mganga: umefanya jambo jema

Christina: Asante sana anko

Mganga: haya safari njema

Christina: unanifukuza?

Mganga: hapana

(wanacheka kisha wanaagana)

Mganga: haya mama uwe unanikumbuka

Christina:(huku anaanza kuondoka) usijali… (anaondoka zake)

Mganga:(anaingia ndani)

Post a Comment

0 Comments