IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 6

 


SCENE 6: -

(Majira ya saa moja na nusu usiku,Mr.Bembele na mkewe wanafika katika jumba la kifahari la mtoto wao wa pekee na mpendwa Raymond,wanapiga honi na haraka mlinzi anafungua geti hilo  wanaingiza gari lao la kifahari kisha wanaliegesha katika sehemu maalumu ya maegesho nyumbani hapo,wanashuka kwenye gari,mama Raymond anamsalimia mlinzi huku Mr.Bembele akionyesha kutojali uwepo wa mlinzi huyo,mara baada ya salamu ya mama Raymond kwa mlinzi huyo wanaingia ndani ambako wanafunguliwa mlango na Raymond)

Mrs.Bembele: wow…mtoto wangu hujambo baba?

Raymond :( huku anawaongoza kwenda ndani) sijambo mama shikamoo…

Mrs.Bembele: marahaba mziwanda wangu

Raymond :( anacheka huku anamgeukia baba yake) shikamoo baba

Mr. Bembele: marahaba baba hujambo?

Raymond: sijambo, karibuni jamani (anaelekea jikoni baada ya sekunde kadhaa anarudi akiwa amebeba juisi glasi tatu kwenye trei) karibuni (anatenga juisi hizo)

Mrs.Bembele: Asante baba (anatabasamu kidogo kisha anakunywa kidogo)

Mr. Bembele: hii nyumba inahitaji mwanamke, mwezi wa sita si uje haraka uoe, umuoe mwanamke wako jamani au aje aishi hapa

Raymond: hapana

Mrs.Bembele: unahitaji msichana wa kukusaidia kazi za hapa na pale

Mr. Bembele: wa kazi gani? Christina aje aishi hapa hata kama hamjafunga ndoa

Raymond :( amekaa pembeni ya mama yake) hata kama Christina akija kuishi hapa msichana wa kazi ni lazima maana hajui chochote hajui kupika hata chai

Mr. Bembele: mvumilie tu si ndo kipenzi chako

Raymond: baba…mi wala simtaki tena Christina

Mrs.Bembele :( anamkonyeza)

Mr. Bembele: baba unatania eeh

Raymond :( anajichekesha) natania dad… (Anamuangalia mama yake)

Mr. Bembele: kidogo nishangae unamkataa mwenzio kisa hajui kupika huku hata wewe hujui kupika

Mrs.Bembele; hivi nani huwa anakupikia?

Raymond; rafiki yangu huwa akija ndo huwa ananipikia lakini huwa  ananifundisha pia

Mrs.Bembele :( anacheka) sipatii picha mnavyojipikilisha kinatokaga kweli chakula cha kueleweka hapo kweli

Raymond; we acha mama halafu mwenyewe huwa ana mtindo wa kujisifia huyo

Mr. Bembele: mnamuongelea nani hapo?

Raymond: rafiki yangu Edmond

Mr. Bembele: huwa ni mtoto wa nani?

Raymond: wazazi wake walishafariki

Mr. Bembele: nay eye ana kazi gani?

Raymond: huwa ni mwalimu…wa shule ya msingi?

Mr. Bembele: na wewe ni nani?

Raymond: mimi ni dokta

Mr. Bembele: ilikuwaje ukawa na urafiki na mwalimu?

Raymond :( anaanza kuchukia) dad

Mr. Bembele: sio dad…halafu nakumbuka kuwa nilishakuambia kabisa kuwa sitaki uwe na urafiki na kijana ambae hana pesa, anachokifata kwako mwanangu ni hizo pesa zako otherwise asingekuangalia na kuanzisha urafiki na wewe, wanafata pesa mwanangu

Mrs.Bembele: baba Raymond...

Mr. Bembele: sio baba Raymond hapa, mwanangu nimemlea kwa shida sana, halafu leo aje awe na urafiki na mwalimu wa shule ya msingi yaani hamuendani hata kidogo na anachotaka yeye ni pesa zako

Raymond; enough dad...

Mrs.Bembele: tafadhali jamani msianze kugombana Kama ilivyo kawaida yenu

Raymond: mama, mimi na dad hatuwezi hata siku moja kupatana kutokana na kwamba mawazo yetu hayako sawa… (anamuangalia baba yake) nachukia dad unavyokuwa unawasumbua na kuwasema vibaya maskini, utasema nao sio watu, inaniuma sana, maskini nao ni watu dad tena watu walioumbwa na Mungu, hawakupenda kuwa hivyo…na pia dad tuliumbwa ili tusaidiane ili Mungu ajitwalie utukufu wake, embu tafakari dad kama wote yungeumMra matajiri nani angemsaidia mwenzie? Mungu katuumba hivyo ili tuhudumiane

Mrs.Bembele :( anatikisa kichwa kuonyesha kuwa anakubaliana na alilosema Raymond)

Mr. Bembele: umaskini ni dhambi na pia ni laana, ndo maana hata maskini wanachukia laana hiyo na mwisho wa siku wanaona sasa watumie watu wengine kujinufaisha

Raymond; siwezi kubishana na wewe maana hata hivyo akili yako umeshailazimisha iamini kuwa sisi matajiri ni lazima tuchangamane na matajiri wenzetu na maskini wafanye hivyo hivyo ya kwamba wachangamane na maskini wenzao halafu mwisho wa siku Mungu atajitwaliaje utukufu wake?

Bembele: ongea yote Raymond ila tu elewa kuwa ni lazima uachane na huyo sijiui nani

Raymond: siwezi dad...

Mr. Bembele :( Kwa hasira huku anatoka nje) wewe naona unataka kunipanda kichwani yaani mimi kama baba yako nakwambia ninayoyaona wewe unajifanya kidume huyo Edmond hajawaoana walimu wenzake mpaka aje kwako?

Raymond: sasa dad…hiyo inakuwa sio vizuri ukifanya hivyo hata yeye ni mtu baba nay eye anahitaji mapenzi ya kweli na si hivyo tunavyofanya dad

Mr. Bembele: wewe mtoto Mimi nakupenda na nimekuonyesha kila kitu kuonyesha hayo ila unaona haitoshi, nikupendeje?

Raymond: hapo dad…you are blackmailing me…unanifanyia hivi vyote halafu mwisho wa siku niendeshe? Baba Mimi ni mwanao na sio mtumwa wako, sio kwasababau umenipa nyumba nzuri na gari la kutembelea ndo unaweza kunifanyia chochote nikanyamaza,

Mrs.Bembele: naomba muache ugomvi jamani angalau nisikilizeni mimi

Mr. Bembele :( anamshika mkewe mkono na kumvuta nje) twende mke wangu naona mtoto wetu tayari keshachotwa akili na huyo rafiki yake

Raymond: sio kuchotwa akili dad…naongea uhalisia

Mr. Bembele :( anaondoka yeye pamoja na mkewe)

Mrs.Bembele:(anajifanya kuwa kasahau kitu hivyo anarudi ndani) mwanangu Raymond nakupenda baba na ninakubaliana na wewe kwa kila kitu mtoto wangu, nachokuomba mimi kama mwanamke niliyekuzaa baba usiwe unagombana na baba yako mwanangu

Raymond:mama,upo kama hukusikia maneno mabaya aliyokuwa anaongea juu ya Rafiki yangu  Edmond,mama siwezi na wala sitaki kusikia mwanadamu yoyote anasemwa vibaya na yoyote atakayemsema vibaya mwanadamu mwenzie mbele yangu basi ni lazima nimueleweshe,hata ikiwa baba yangu mzazi,mama sisi ni mavumbi wote iwe tajiri iwe maskini sisi wote ni mavumbi,na mavumbini tutarudi sasa sio kwamba Mungu ametusaidia tuna maisha mazuri ndo tudharau na kuwatenga ambao wana maisha duni yaani hayo malezi siyawezi na wala sikubaliani nayo

Mrs.Bembele: unajua hata Mimi baba siyakubali hayo mawazo aliyo nayo baba yako, ila sasa ndo tutafanyaje ndo kichwa cha familia yetu

Raymond: kwahiyo mama wewe unatakaje? Niachane na Edmond?

Mrs.Bembele: hapana mwanangu

Mr. Bembele :( sauti kutoka nje) hicho ulichosahau kimeota mabawa kimeruka au, embu twende nyumbani

Mrs.Bembele :( Kwa Raymond) nitakupigia simu baadae mwanangu nakupenda

Raymond: nakupenda pia mama

(Haraka anatoka nje alipo mume wake anapanda kwenye gari kisha Mr. Bembele analiwasha gari na kwa mwendo wa kasi wanaondoka mahali hapo, huku ndani alipo Raymond nae kuingia chumbani kwake ili apumzike)

Raymond: mimi siwezi kubadilisha mawazo niliyowekewa na mama yangu tangu nipo mdogo kuwa sisi sote ni ndugu maana tuliumbwa na Mungu mmoja…(anapanda kitandani anachukua rimoti anawasha runinga kisha anajilaza)nampenda na kumheshimu mzee wangu ila siyaheshimu mawazo yake,halafu baba bwana kwahiyo kanipa vyote hivi ili anaiendeshe,yaani nifanye anachotaka,kweli baba yangu ana akili mbovu sana yaani hata mimi mwanae wa kuzaa anaonyesha ubabe?(anajigunia mwenyewe huku anaendelea kupekua chaneli kwenye runinga )

Post a Comment

0 Comments