IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 53

 


SCENE 53: -

BAADA YA MWEZI MMOJA

HARUSI YA EDMOND NA CATHERINE

(usiku mwingine wa furaha sana kwa Edmond na Catherine maana ni usiku ambao wanasherekea muungano wao mara baada ya kuunganishwa mbele ya Mungu na wanadamu,kabla ya maharusi kuingia wanaanza kuingia watu ambao ni karibu sana na maharusi hao.Miongoni mwao ni wazazi wa Catherine na baada ya wazazi wa Catherine wanaingia Mr.Bembele na Mrs.Bembele,na kwa mara ya kwanza baada ya kuchumbiwa Christina anaingia na mchumba wake,wamependeza sio mchezo,na baada yao ni Raymond na Angelina wanaingia,wamependeza sana Raymond amevaa suti yenye upindo wa zambarau na Angelina amevaa gauni refu linalomshika umbo vyema nay eye ni rangi ya zambarau.)

Raymond :( anamuona Christina na Peter) baby...Twende tukawasalimie…kina Christina

Angelina :( akiwa amejipamba amepambika anamfuata nyuma mchumba wake)

Raymond :( anawafikia) mambo zenu

Christina: nzuri mwenyekiti wa kamati

Raymond: acha tu ndugu yangu

Peter:(anacheka) mambo vipi? (anampa mkono)

Christina:(anamuona Angelina) wow…jamani katoto kamependeza

Angelina :( anatabasamu kidogo) shikamoo (anapiga magoti)

Christina: marahaba mama hujambo?

Angelina: sijambo (Kwa Peter) shikamoo

Peter: marahaba hujambo

Angelina: sijambo…

Christina: wow…mmependeza Sana

Raymond: hata nyie…

Christina: by the way…unamjua mchumba wangu (anamshika Peter)

Raymond: yeah…tunajuana

Christina: mlijuana wapi?

(Raymond na Peter wanacheka)

Christina: mlijuana wapi?

Raymond: kitaa tu kwenye harakati za maisha

(Wote wanacheka)

Raymond: mmefurahi…kweli kuwaona…Mimi namjua Peter na Peter ananijua ila tu hamjui mchumba wangu

Angelina :( anatabasamu)

Raymond :( anamshika bega Angelina) huyu ndo mke wangu mtarajiwa…anaitwa Angelina

Christina: tunamjua

Raymond: unamjua wewe…Peter hamjui

Peter: namjua…Christina alikuwa anapenda kumuongelea

(Wote wanaangua kicheko)

Christina: yaani nyie maisha dah!!

Angelina :( anatabasamu)

Raymond: Ni safari ndefu

(Wazazi wa Christina na wa Raymond wamekaa pamoja na wanawaangalia watoto wao wanaoonekana kuwa katika wakati mzuri pamoja)

Raymond: njooni tukae tusije tukaanguka… (Anamuita mhudumu) tafadhali naomba utuletee vinywaji

Christina: hongera umeipigania harusi ya rafiki yako mpaka imekuwa bwana

Raymond: si unajua tena ananichukulia kama ndugu (anamuwekea Angelina nguo vizuri)

Christina: yaani kuanzia kanisani mambo yalikuwa mambo na picha, vinywaji, chakula nyumbani kila kitu kipo safi…hongera sana baba

Raymond: Asante (anatabasamu)

(Mhudumu anawaletea vinywaji)

Christina: sasa mbona sherehe haina pombe jamani

Peter: wewe pombe ya nini?

Raymond: harusi ya walokole hii…

Mc: habari za jioni mabibi na mabwana…

(Watu wanaitikia)

Mc: karibuni sote kwenye hafla ya kuwapongeza Edmond na Catherine ambao leo mbele yetu na mbele za Mungu wameunganishwa na Mungu na kuwa kitu kimoja yaani wanandoa...Anayewakaribisha ni mimi MC mazoea karibuni sana… (Kimya kidogo) basi baada ya utambulisho mfupi sasa tuwakaribishe maharusi waingie ukumbini

(Muziki mkubwa unapigwa)

Mc: karibuni…Dj fanya yako

(Ma-brighter wa kiume na kike wanaingia wakiwa wanacheza kwa mbwembwe zote huku watu wakiwashangilia kwa shangwe nyingi)

Christina :( anamuangalia Angelina aliyekaa pembeni yake) unaonekana unapenda sherehe

Raymond :( anadakia) anawaza nyama tu…anapenda nyama huyu anafurahi maana anajua kuna nyama mwisho wa yote anajua lazima tukale vyuku (anacheka)

Angelina: anakudanganya…

(Wanacheka)

Mc: baada ya mabrighter sasa matron na best man wanaingia...Dj

(Matron na best man wanaingia kwa mbwembwe zote huku watu wakiwashangilia, wanacheza kwa muda kisha wanafika mbele ya kadamnasi)

Mc: sasa…mabibi na mabwana tukae tayari kabisa kwa ajili ya kuwaruhusu malkia na mfalme wa usiku huu…Edmond na Catherine

(Watu wanapiga makofi na meza inayoonekana ina shangwe kuliko zote ni meza waliokaa kina Raymond tena ya mbele kabisa)

Mc: Dj…niletee maharusi wetu

(Watu wanasimama huku Catherine anaingia akiwa amependeza sana gauni lake lenye mkia mrefu limebana vyema umbo lake, anaingia akiwa anacheza kwa madoido na kuringa na anaonekana kutambua kuwa ile ni siku yake na sio siku ya mtu mwingine...Baada ya muda mumewe akiwa na furaha sasa kumzidi mke anaingia kuungana na mkewe na wanacheza kwa madoido na watu wanafurahishwa sana na mpangilio huo wa uingiaji)

Edmond :( anaangaza macho huku macho yake yanamtafuta Raymond na anapofanikiwa kumpata anamuonyeshea ishara ya kumshukuru kwa yote)

Raymond :( Kwa sauti ya kunong’oneza) usijali

(Maharusi hao wanacheza Kwa furaha nyingi wakielekea mbele walipo matron na best man, baada ya hatua chache hatimaye wanafika mbele kabisa, wanapofika mbele mziki unazimwa ghafla)

Mc: Asante Sana... (Kwa maharusi) wow…mmependeza na mmeingia kwa mbwembwe

(Watu wanacheka)

Mc: nimependa…anyway… (Kwa watu) makofi tena na vigelegele kwa maharusi wetu jamani

(Watu wanashangilia)

Mc: utambulisho…sasa Kama bibi harusi una aibu tuambie mapemaaaaa

Catherine :( anachukua kipaza sauti) sina aibu

Mc: kweli…

Edmond :( anacheka)

Mc: haya Anza kutambulisha…

Catherine :( Kwa ujasiri) asanteni wote…naomba kwanza niwasalimu kwa jina la Bwana

(Watu wanaitikia)

Catherine: napenda kuwatambulisha wazazi wangu baba na mama…naomba wasimame na muwapungie watu mikono

(Wazazi wanasimama)

Catherine: kaka zangu na mawifi zangu

(Makaka na ma wifi wanasimama na kuwapungia mikono)

Catherine: wadogo zangu wote tuliozaliwa tumbo moja, watoto wa baba zangu wakubwa, wadogo naomba msimame muwapungie watu mikono

(Wadogo zake ambao ndo wengi wao akiwemo Angelina wanasimama na kupungia watu mikono)

Catherine: mwisho kabisa ninamtambulisha mume wangu, ubavu wangu, chaguo la moyo wangu na namshukuru kwa kunichagua mimi kuwa mkewe na mama wa watoto wake

(Watu wanashangilia)

Catherine: Mr. Edmond Mutalemwa…

Edmond :( anamkumbatia mkewe)

Mc: safi kumbe kweli bibi harusi huogopi haya zamu yako sasa bwana harusi…utaweza

Edmond: naweza…

Mc: haya muombe mkeo kipaza sauti sio unampokonya kibabe…ichukue taratibu halafu tutambulishe

Edmond :( anafanya kama alivyoambiwa na Mc) asanteni bwana Yesu asifiwe…

(Wanaitikia)

Edmond: asalama le kum

(Wanaitikia)

Edmond: tumsifu yesu kristu

(Wanaitikia)

Edmond: kwanza kabisa … (anajisikia uchungu ghafla)

Catherine :( anamshika bega kumpa moyo)

Edmond: natamani kuwatambulisha wazazi wangu lakini kwa bahati mbaya wametangulia mbele za haki

Watu: oh maskini…

Edmond: lakini ninao wazazi walionisimamia mpaka Leo hii nimefanikisha kumuoa mwanamke wa ndoto zangu Mr na Mrs.Bembele nyinyi ni wazazi wangu naomba msimame muwapungie mikono

Raymond :( anafanya utundu Kwa kumzomea mama yake)

(Mr & Mrs.Bembele wanasimama na kuwapungia watu mikono)

Edmond: asanteni Sana…kaka zangu na mashemeji zangu wote…naomba msimame muwapungie watu mikono

(Makaka pamoja na mashemeji wanasimama na kuwapungia watu mikono)

Edmond: wadogo zangu…Mimi kwetu ndo wa mwisho ila nina mdogo wangu wa nguvu…Mr. Raymond Bembele naomba usimame uwapungie watu mikono

Raymond :( akiwa anatabasamu anasimama na anapungia watu mikono)

(Shangwe nyingi zinatawala ukumbini hapo ishara ya kuonyesha kuwa Raymond ni mtu wa watu)

Edmond :( anacheka) nimefurahi ukumbi umelipuka Kwa shangwe

(Shangwe zinalipuka tena)

Raymond :( anacheka)

Edmond: mwisho kabisa napenda kumtambulisha mke wangu mpenzi…. wa ubavu, asali wa moyo wangu, panado yangu

Catherine :( anacheka) panado

Edmond: Mrs. Catherine Edmond Mutalemwa

(Shangwe zinalipuka)

Mc: Asante Sana…Kwa utambulisho

(Sherehe inaendelea huku matukio yanaenda jinsi yalivyopangwa, watu wanaserebuka, wahudumu nao wanajitahidi kugawa chakula na vitafunwa mbalimbali, muziki unapigwa na kuna burudani mbalimbali zinaendelea, sherehe imefana sana na kila mtu anaonekana kufurahi sana kwa usiku huo. muda wa zawadi unafika na watu tofautitofauti wanatoa zawadi, zawadi ni nyingi sana, kamati ikiongozwa na Raymond wanatoa zawadi yao)

Raymond:(anachukua kipaza sauti) asanteni sana, habari za jioni mabibi na mabwana mbele yenu ni wana kamati walioweka nguvu zao katika kufanikisha sherehe hii…kutokana na muda wala sitawambulisha ila nitajitambulisha kwa niaba ya wote…mimi naitwa Dk. Raymond Desmond Bembele ni mwenyekiti wa kamati

(Makofi na vigelegele vinasikika mahali hapo)

Raymond: Kama kamati ile nyumba uliyoianza…sisi tutaimalizia na kila kitu kimeshanunuliwa (anamkabidhi risiti)

Edmond: thank you so much brother…

Raymond: sambamba na hivyo vitu vya ndani…interior zote ni juu yetu...na baada ya hapo tunakukabidhi milioni 30 ya kuanzia maisha

(watu wanashangilia sana, baada ya makabidhiano ya zawadi kamati inarudi kukaa na sherehe inaendelea huku kila mmoja anafurahia sherehe hiyo)

 

Post a Comment

0 Comments