IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 54

 


SCENE 54: -

BAADA YA WIKI MBILI: -

MAHARI YA ANGELINA: -

(majira ya saa nane mchana, Mr. Bembele, Mrs.Bembele, Edmond, Peter na Raymond wanafika nyumbani kwa kina Angelina ambapo wanapokelewa kwa shangwe nyingi sana na wanafamilia na ndugu mbali mbali wa Angelina, sebuleni wamekaa wazee wa Angelina yaani wajomba na jikoni kina mama mbalimbali wanamalizia kupika, nyumba ni ya kawaida sana sakafu haina simenti n.k, huku Angelina, Catherine na Christina wamekaa chumbani wakimuandaa Angelina)

Catherine :( anachungulia kupitia dirisha dogo linaloelekea sebuleni) wamewahi?

Christina: ni bora walivyoamua kuja jana wakalala hotelini mjini (anaguna) yaani wangesema waje leo tungekesha

Angelina :( anavuta pumzi) wameshakuja kwani?

Catherine: ndo wanaingia, wapo mzee mwenyewe, shemeji Raymond, shemeji Peter na mume wangu

Christina: tufanyeni haraka si watatuita muda si mrefu

Catherine: bado Sana ndo kwanza wanaingia

(Vinasikika vigelegele nje)

Angelina: Mungu wangu pamekucha…

Catherine: hata usiogope ukishatolewa mahari unakuwa na uhakika Fulani hivi…najua huwa inakupa presha…si eti Christina?

Christina: Sana…

Angelina :( Kwa Christina) shemeji ameshakutolea mahari?

Christina: muda mrefu mbona…

Catherine: ndoa lini?

Christina: baada ya miezi miwili

Catherine :( anamuangalia Angelina) maisha bwana nakumbuka Angelina alikuwa anamuogopa Raymond anamuita kaka mara sijui nini Leo mume

(Wanacheka)

Christina: ndo hivyo haya maisha hakuna anayejua Mungu kampangia nini

Catherine :(macho yake yanaangalia sebuleni) ni kweli

Christina :( anacheka) yaani wewe macho yako yapo sebuleni una utani

Catherine: acha tu

(Huku sebuleni, wajomba wanawakaribisha wageni wao vizuri huku shangwe zinatawala Kwa wachache waliopo hapo)

Mjomba: karibuni Sana ndugu zangu…nyie ni wenyeji wa wapi?

Mr. Bembele :( anakohoa kidogo) sisi Kwa uenyeji tumetoka Dar ila Kwa kabila sisi ni wasukuma wa Mwanza

Mjomba 2: aha…Safi Sana...Sisi ni wahangaza na ni wenyeji wa Ngara na ndo wahangaza hupatikana

Mr. Bembele: Asante Sana na tunafurahi na tushukuru kufahamu hilo

Mjomba: ndio karibuni wageni wetu labda tuanze Kwa kujitambulisha sisi kwa majina lakini baadae tutaendelea na ratiba nyingine…

Mr. Bembele: labda tusikie utambulisho kutoka kwenu maana nyinyi ndo wenyeji zetu

Mjomba 2: yupo sawa kabisa… (Anatikia kwa kichwa) Kwa majina naitwa Caisalius Rogders ni kaka kabisa wa mama yake Angelina….

Mjomba: nami naitwa Raymond…Rodgers ni mjomba wake Angelina

Mr. Bembele :( anacheka) bwana Raymond una jina sawa kabisa na kijana wetu hapa… (Anamshika Raymond)

Raymond Rodgers: ndio Angelina alitudokeza

(Wanacheka)

Caisalius: sawa inapendeza Sana…tusikie kwenu

Mr. Bembele: mimi naitwa Bwana Bembele ni mfanyabiashara jijini Dar es salaam, na huyu anayefata anaitwa Peter na yule mwingine anaitwa Edmond na huyu hapa (anamgusa Raymond) anaitwa Raymond...Bembele ni daktari nan do kijana aliyetuleta hapa, ameona ua katika bustani yenu kimila na desturi za wa Tanzania ameona aje aombe ridhaa yenu alichume…ni mwanangu

Caisalius: tunafurahi Sana kwake yeye kuchukua ustaarabu wa kuomba nasi tunasema aombae hupewa

(Wanacheka)

Mr. Bembele: basi Kama ilivyo kawaida tukikubaliwa tunatoa zawadi Kwa wale ambao wametupa ridhaa ya kuchuma ua

(Wajomba wanacheka)

Raymond Rodgers: wajina embu Kwa ustaarabu (anawageukia wanawake) leteni mabinti hao ili kijana atuambie ni ua gani amelichagua

Raymond :( anacheka)

(Wanawake wanawaleta wasichana waliovaa sare wakiwa wamejifunika khanga na hawaonekani kirahisi)

Caisalius: wafunue tuwaone

(Wanawake wanawafunua wasichana hao)

Raymond :( anatabasamu)

Caisalius: haya baba Kwa upole kabisa embu kamata ua unalotaka kulichuma

Raymond :( ananyanyuka na kwenda moja kwa moja mpaka kwa Angelina) huyu hapa

(Vigelegele vinalipuka)

Caisalius: sawa kabisa… (Kwa wasichana wengine) mnaweza mkaenda

(Wasichana wanaondoka)

Caisalius :( Kwa Angelina) enhe mama tuambie kijana amekupenda na anataka kukuoa je unamruhusu

Angelina :( anajibu huku anapiga magoti mpaka chini kisha kwa heshima kabisa anainamisha kichwa) ndio mjomba

(Vigelegele na shangwe vinatawala)

Raymond :( anafurahi Sana)

Angelina :( anamuangalia Raymond huku anatabasamu)

Raymond Rodgers: sawa wewe rudi tutakurudisha baadae

Angelina :( anarudi ndani)

Caisalius :( kwa Raymond) kijana rudi ukakae ulipokuwa umekaa...

Raymond :( anarudi)

Mr. Bembele: asanteni sana kwa kutupokea (anatoa zawadi nyingi ikiwemo vitenge, mashati, mablanketi na pesa taslimu kama milioni moja) hiyo ni zawadi ya kutupokea na kutukubalia

(Wajomba wanapokea na kuwapa wanawake mbalimbali)

Caisalius: tunawashukuru sana kwa zawadi hizi...Sasa Ni wakati wa kuongelea mahari

Mr. Bembele: sawa tunawasikiliza

Caisalius: sisi mtoto wetu tumemlea Kwa shida Sana na pia tumemlea katika maadili mazuri na anafaa kuwa mke na atakuwa mke bora

(Upande wa kina Raymond wanatikisa vichwa kukubaliana na kinachosemwa na mjomba)

Mr. Bembele: sawa tunakubali kabisa…

(Wajomba wanajadili jambo)

Raymond Rodgers: sawa sisi mahari tumepanga iwe milioni tano

(Upande wa kina Raymond wanajadili jambo)

Mr. Bembele: sawa tumekubali (anatoa kitita cha pesa)

(Mjomba anapokea Na kumuita mama yake Angelina)

Mama Angelina :( anazipokea pesa Kwa heshima kabisa)

Caisalius: huyu ni mama mzazi wa Angelina

Mr. Bembele: wanafanana sana

Mama Angelina :( anatabasamu)

Caisalius :( Kwa mama Angelina) hii ni mahari binti yetu Angelina ameposwa anataka kuolewa

Mama Angelina :( anapiga vigelegele) karibuni Sana

Mr. Bembele: Asante Sana

(Mr. Bembele na mama Angelina wanashikana mikono)

Caisalius: Na kijana aliyemposa mwenetu Ni (anamshika bega Raymond)

Mama Angelina: Asante baba…wewe ndo huwa tunaongea kwenye simu?

Raymond: ndio mama…

Mama Angelina: karibu baba (anamshika mkono huku anapiga vigelegele)

(Mrs.Bembele na mama Angelina wanakumbatiana ishara ya kukubaliana)

Raymond Rodgers: sasa zoezi la mahari tayari sasa tuwakaribishe wageni wetu kushiriki chakula cha mchana kwa mara ya kwanza kama ndugu

Mr. Bembele: haina shida kabisa…tunashukuru kwa mapokezi mazuri mnaonekana ni wakarimu sana

Caisalius: kawaida ya    waTanzania…halafu Angelina ana wadogo zake watatu… (kwa mwanamke mmoja) waiteni wageni wawaone

(Wadogo wa Angelina wanakuja kwa wageni na kila mtu anaonekana kuwafurahia)

Mr. Bembele: jamani watoto wazuri hamjambo?

(Wadogo zake Angelina wanawasalimia wageni Kwa heshima)

Mr. Bembele: mna heshima…

Caisalius :( anadakia) Kama dada Yao (anatabasamu)

Mr. Bembele :( kwa mkubwa inaonekana ndo anamfuata Angelina) unaitwa nani?

Mdogo: Angello...

Mwingine: Mimi naitwa monalisa

Mwingine: Mimi naitwa Clara

Mr. Bembele: majina mazuri Sana…tunaenda wote Dar

Monalisa: kule kwa dada?

Mr. Bembele: ndio kwa dada

Clara: ndio

(Wote wanacheka)

Mr. Bembele: haya jiandaeni twendeni sawa ee

Angello: sawa

(Wanarudi ndani wakiwa wana furaha Sana)

Raymond Rodgers: jamani chakula tayari tujongee mezani

(Catherine, Christina pamoja na Angelina wanakuja kuungana na wenzi wao kwenye chakula, Mr na Mrs.Bembele wanakaa sehemu moja huku vijana sita yaani Edmond na Catherine, Peter na Christina na Angelina na Raymond wanakaa sehemu moja)

Edmond: afadhali siku imeenda na kuisha vizuri

Raymond: kabisa

Peter :( Kwa Raymond) official mume wa mtu mtarajiwa

Edmond: kwa mara ya ngapi sijui

Catherine: acha kumchokoza mwenzio muone

Christina :( anacheka huku anakula chakula chake)

Angelina :( anatabasamu)

Edmond: najiuliza zile kesi sijui zitaendelea…zile za kubeba mabegi…

(Wanaangua vicheko, vinavyowashtua wazee waliokaa mbali nao)

Caisalius: mmefurahi ee

(Hawajibu kitu badala yake wanaangua vicheko tena)

Caisalius: vizuri kufurahi wanangu

(Mazungumzo yanaendelea baina ya watu)

Raymond :( anamshika mkono Angelina) namshukuru Mungu kwa ajili ya leo mpenzi wangu sasa mipango ya kujenga familia yetu

Angelina:ni kweli mume wangu mtarajiwa

Raymond: nakupenda Sana

(Wanaendelea kula, na kila mmoja wao anafurahia siku hiyo, picha nyingi zinapigwa na mara nyingi mpiga picha anawalenga Angelina na Raymond ambao ndo malkia na mfalme wa siku hiyo. sherehe ya mahari inaisha vizuri bila shida kabisa na kila mtu anaonekana kuridhika na kila kitu kinachoendelea)

 

Post a Comment

0 Comments