IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 55

 


SCENE 55: -

(Siku kadhaa mara baada ya sherehe ya kutolewa kwa mahari kwa Angelina kupita, wadogo zake Angelina pamoja na mama yao wamekaa katika sebule kubwa nay a kifahari ya Raymond mume mtarajiwa wa Angelina, wanashangaa uzuri wa kila kitu ndani humo)

Clara :( Kwa mama yake) mama ona li TV likubwa

Mama: naliona mama

Monalisa: mama ona palivyo pazuri…

Mama: Sana

Angello: mama shemeji tajiri si eti eeh

Mama: ndio mwanangu Mungu hamtupi mja wake ona mwanangu anapoenda kuolewa yaani nafurahi Mimi…asante Mungu wangu

(Wakati huu Angelina amesimama nje ya dirisha moja linaloelekea sebuleni anawasikiliza na kila mara anatabasamu)

Angelina: hata mimi namshukuru Mungu kwa haya yote…sikutegemea kama Raymond alikuwa ananiambia ukweli tangu mwanzo kuwa anataka kunioa…sikudhani kama alikuwa ananiambia kweli pamoja na misukosuko yote ya maisha bado Raymond alionyesha kunipenda Zaidi na Zaidi

(Raymond anakuja Kwa nyuma yake na kumkumbatia)

Raymond: mbona unaongea peke yako…

Angelina :( Analia huku anacheka) Asante sana Raymond

Raymond: machozi tena? (anamgeuza ili amuangalie vizuri)

Angelina:(anacheka) ona wadogo zangu walivyo na furaha…nimekuwa nikifanya kila kitu kuona tabasamu kama linavyoonekana sasa hivi…Mungu ni mwaminifu…

Raymond:(anamshika mkono huku anamuongoza kuelekea bustanini) twende mke wangu mtarajiwa twende mahali mapenzi yetu yalipoanzia…

(Wanafika palepale Raymond alipopamba kwa ajili ya kumwambia hisia zake kwa mara ya kwanza)

Raymond: hapa nilipachagua sababu ya utulivu wake, nilipapamba kwa mara ya kwanza na kukuambia hisia zangu kuwa ninakupenda sana mpenzi wangu…kabla sijakuambia nilikuwa naogopa watu, Edmond, Catherine.baba. mama na Zaidi Christina ambae kwa kipindi hicho alikuwa ni mchumba wangu…

Angelina :( anamuangalia sana)

Raymond: siku ile niliweka pembeni uoga na kukutamkia hisia zangu nashukuru ukazipokea…

Angelina:(anatabasamu)

Raymond:baada ya penzi letu kujulikana…ulipata tabu sana mara uambiwe nina mtoto….(anacheka)ukabeba mizigo yako ukaondoka nikakufata huku nikiwa naogopa sana pengine labda ndo mara yetu ya mwisho na kwamba penzi letu litaishia hapo…nilikuambia ukakubali kurudi na mimi nyumbani…baada ya muda ukatekwa na kupigwa vibaya ila ulipotibiwa ukasahau yote na kuruhusu penzi letu kuendelea…hilo likapita,nikarudishwa akili nyuma lakini bado ukasimama na mimi hukuniacha mpaka siku nikawa vizuri na penzi letu likazidi kuota mizizi

Angelina :( anatabasamu)

Raymond: Asante sana Angelina kwa kunipenda kunijali na kuniheshimu…asante kwa kumheshimu baba yangu pamoja na kwamba alikuwa anakutukana sana na kukusema vibaya ila hukuacha kumheshimu kama baba yako mzazi… (Anamuangalia kidogo) wewe mwanamke ni bora sana nataka nikupe zawadi sijui kama itatosha kwa furaha uliyo nipa katika maisha yangu…siku namwambia Edmond anitafutie msichana wa kazi za ndani sikuwa na wazo kama msichana huyo atakuwa mke wangu na mama wa watoto wangu

Angelina :( anacheka)

Raymond: I fell in love with my housegirl…I AM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL (anacheka)

Angelina :( anacheka pia)

Raymond: umeelewa?

Angelina: nimeelewa kidogo…sana, si unajua nimeanza kusoma kiingereza naelewa

Raymond: nimesemaje?

Angelina: love maana yake kupenda na housegirl maana yake msichana wa kazi za nyumbani sasa hapo lazima itakuwa labda nampenda msichana wangu wa kazi za nyumbani

Raymond: umepatia (anamnyanyua kidogo)

Angelina :( anambusu)

Raymond: wakati wote tupo kwenye mahusiano kwanza kama kaka na dada, baadae wapenzi na baadae wachumba nilikuwa nakujengea nyumba kama zawadi…yaani sasa hiyo ni ya kwako hata ikitokea leo nimekufa ni yako wewe Angelina

Angelina: baby usiongelee kufa bwana...

Raymond :( anamuonyesha picha kwenye simu) hi indo nyumba yako

(Nyumba nzuri hatari)

Angelina: Mungu wangu nyumba nzuri sana...Jamani asante mume wangu (anamkumbatia) asante sana sana tena sana...Wow...Jamani (anambusu mfululizo)

Raymond: ninafurahi kwamba umefurahi sana, wadogo zako utawasomesha…sio kwa mshahara wa udada wa nyumbani bali…nimekufungulia kampuni ya wadada wa kazi za nyumbani yaani housegirl utakuwa unawatoa mikoa mbalimbali unawaleta huku unawafundisha labda na wenyewe watapata bahati kama yako(anacheka)kisha unawasambaza watu wana uhitaji wa mabinti wa kazi…

Angelina :( anafurahi Sana)

Raymond: nyumba ya kijijini kwa mama yako imeshaanza kurekebishwa na kila kitu kinaendelea vizuri

Angelina:(Analia kwa furaha) Mungu nikurudishie nini jamani… (kwa Raymond) asante mume wangu mpenzi…

Raymond: lakini mbali na kampuni ya wadada wa kazi kuna saluni ya kike ya kisasa nimeifungua kwa ajili yako yaani sitahusika labda ukitaka kunikopesha

(wanacheka)

Angelina: yaani wewe

Raymond: nini tena?

Angelina: I love you

Raymond:(anashangilia) Angelina kajua kiingereza

Angelina: nilimuuliza mwalimu akaniambia ni hivyo…nimeitaja vizuri

Raymond: sana (anamuangalia kwa umakini) halafu mimi mchumba wangu ni mrembo jamani yaani watoto watakaotoka hapo ni visu…wakifanana na wewe lakini

Angelina: mimi nataka wafanane na wewe…

Raymond: mama yangu na sura baya hili?

Angelina: sio mbaya na mashavu ya kubonyea ni noma

Raymond: yanabonyea kama ya Gloria Bembele

Angelina: enhe…halafu unafanana kweli na mama kuliko baba

Raymond: eti ee… (anaangaza angaza) yaani huyu mdada wa kazi hajui kazi sijui yuko wapi?

Angelina:(anacheka) huna lolote unataka kunituma kitu, naenda kukuchukulia hiyo juisi unayopenda (anacheka huku ananyanyuka kuelekea ndani)

Ramadhani:(ambae amesimama anawaangalia muda mrefu) jamani haya maisha acheni yaitwe maisha na Mungu ndo muweza wa yote akipanga, amepanga…hata waje na waganga lori zima Mungu atabaki kuwa mkuu…ona sasa hawa, kulikuwa na kina Christina kina Mz. Bembele leo hii wamenawa mikono wanachekelea tu (anacheka) sema nini Raymond Angelina amekufaa mwaya…mimi nilikuwa nakula hela bure za Christina ila hata mimi nilikuwa naona hamuendani (anacheka huku anarudi getini) mmependezeana bwana

Angelina :( anarudi alipo mchumba wake na juisi glasi mbili) yaani wadogo zangu wanapenda Tv wanachelea tu (anampa glasi moja Raymond huku moja anabaki nayo)

Raymond: waache wafurahie jamani Kwa shemeji...

Angelina: wanatakiwa warudi shule

Raymond: we nae (anakunywa juisi kidogo) ila kwenye harusi watakuwepo?

Angelina: watakuja

(Wanaendelea kupunga upepo safi huku wanapata juisi zao baridi huku wanazungumza mambo mbalimbali)

Post a Comment

0 Comments