IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 56

 


SCENE 56: -

BAADA YA MIEZI MIWILI: -

HARUSI YA CHRISTINA NA PETER: -

(jioni iliyo njema machoni pa bwana, basi kama ilivyo kawaida ikimpendeza bwana basi na wanadamu wanapendezwa nayo, hali ya hewa inavutia ili kuendelea na shughuli yoyote ile. katika ukumbi mmoja wa kifahari watu wamekusanyika ili kusherekea muungano wa Peter na Christina, wapenzi wa karibia miaka mitatu. Watu mbalimbali wanaingia ukumbini, miongoni mwa watu hao ni wazazi wa Christina, wazazi wa Raymond, Edmond na mkewe na hatimaye Raymond na mchumba wake)

Mama Christina:(anajifuta machozi)

Shangazi: mwenzetu vipi mbona unalia?

Mama: nimefurahi sana…

Baba:(anacheka sana) mwanao alishtuka mapema sana...

Mama: Mungu ni mwaminifu leo Christina amefunga ndoa na yule yule mwanaume aliyekuwa anaona hamfai…mwisho wa siku mapenzi yakashinda pesa na mali zote

Shangazi: hakika!!!

Mama: mwanangu leo alikuwa amependeza sana kanisani

Shangazi: sana

Baba:my princess is married (anafurahi sana)

(upande walipokaa Angelina na Raymond)

Angelina: nimependa sana kanisani wakati Christina Analia

Raymond: yes…amelia sana maana yeye na huyo mwanaume wamepitia mambo mengi sana hakuamini kama leo amekuwa wake wa milele

Angelina:(anaangaza angaza) wow ukumbi umependeza

Raymond:na mwalimu wako wa English course anafanya kazi nzuri sana…

Angelina: kwanini?

Raymond: nazisikia hizo wow... (anacheka sana)

Angelina: bwana...niache, mimi nausifia ukumbi na wewe unanitoa kwenye mood

Raymond: kazi ya sisi kamati… (anacheka kwa kujidai)

Angelina:(anaguna) na unavyopenda kuwa mwenyekiti wa kamati sijui harusi yako nani atakuwa mwenyekiti?

Raymond: hata wewe sawa tu

Angelina:(anashangaa) mimi tena?

Raymond: ndio…(anacheka)

Angelina: huku mimi ni bibi harusi…

Raymond: wacha weeee

(kwa wazazi wa Raymond)

Mrs.Bembele: yaani ukumbi umependeza Sana

Mr. Bembele: kabisa

Mrs.Bembele: Christina kaolewa…nimefurahi Sana kwanza kwasababu hii miezi michache iliyopita amejua kujirekebisha na imependeza

Mr. Bembele: kweli kabisa (anajisemea moyoni) kikubwa nachomshukuru Christina ni kwamba hakuwahi kusema ukweli wa mahusiano yetu kwa mke wangu ameniokolea ndoa sana

Mrs.Bembele: nakupenda mume wangu

Mr. Bembele: nakupenda pia Gloria wangu mpenzi

(wanacheka)

Mc: habari za jioni mabibi na mabwana…

Watu:(wanaitikia)

Mc: tupo nje ya muda kidogo wapendwa wangu na kwa kutambua hilo, sasa naomba niwaruhusu ma brighter wasafishe njia ya maharusi wetu… (Kwa dj) Dj

(Muziki mzuri unapigwa wakati huo mabrighter wanaingia wakicheza kwa madaha yote, wanacheza wakielekea mbele ya ukumbi, wanacheza kwa muda na hatimaye wanafika mbele)

Mc: barabara kabisa mara baada ya mabrighter wenu wake Kwa waume sasa ni zamu ya matron na best man

(Edmond na Catherine kama matron na bestman wanaingia ukumbini hapo kwa mbwembwe Zaidi ya zile walizoonyesha siku ya harusi yao, wanacheza huku kila mmoja anawashangaalia sana, wakiwatiwa moyo na shangwe zile wanacheza mpaka wanafika mbele ambapo mabrighter wamesimama)

Mc: wow…basi bila kupoteza muda kwa shangwe hizohizo naomba tuwakaribishe maharusi wetu…bibi na bwana mbeikya…bwana harusi mhaya huyu (anacheka kidogo) wahaya mpo

(Unapigwa wimbo mmoja wa kihaya unaonawachangamsha Zaidi watu)

Mc: wwwwaaaah basi Dj imetosha Sana hiyo

(watu wanarudi kukaa kwa wale wote walioenda mbele kuyarudi mangoma ya kihaya)

Mc: safi sana…sasa mabibi na mabwana nawaomba sasa kwa heshima na taadhima tuwakaribishe maharusi wetu ambao wapo tayari kabisa kwa ajili ya kuingia ukumbini hapa...kwa ajili ya sherehe nzuri tuliyowaandalia siku ya leo…asante sana kamati kwa kufanya sherehe yetu ipendeze na wakahakikisha tunakula tunakunywa tunavyotaka…shoutout kwa Raymond Bembele mwenyekiti wa kamati ya harusi hii

(Watu wanapiga makofi)

Mc: basi Dj niletee maharusi wangu…

(muziki mzuri na wa amshaamsha unapigwa huku Christina na mumewe wakiingia kwa mbwembwe zote, watu wanawashangilia na wa kufurahi wanafurahi wenye kupiga picha wanapiga kwa kifupi kila kitu kipo sawa kama kilivyopangwa, wanacheza na kila mtu anavutiwa na jinsi wanavyoingia, wanacheza kwa muda na hatimaye wanafika mbele walipo matron na bestman)

Mc: asante Dj… (kwa maharusi) mmependeza jamani…

(Ama hakika wamependeza, tena wamependezeana Peter ni mrefu kijana mtanashati huku Christina ni mrefu kiasi na ni msichana mrembo sana)

Mc: wow…jamani maharusi mmependeza

Peter na Christina :( wanacheka) asante sana

Mc: tuendelee na ratiba nyingine maana nikianza kuwasifu jamani sitamaliza…

(Watu wanacheka Sana)

Mc: utambulisho

(Bila kupoteza wakati Peter anaanza utambulisho akitambulisha ndugu zake na kila akitambulisha ndugu wananyanyuka na kuwapungia watu mikono, anatambulisha wote na mwisho anamtambulisha Christina)

Peter :( anamshika bega mkewe Kama kumkumbatia hivi) na huyu ni kipenzi changu, chaguo la moyo wangu, mahabuba wangu

(Watu wanashangilia)

Peter: mke wangu…anaitwa Mrs.Christina Peter Mbeikya…

(Watu wanapiga makofi)

Mc: safi jamani bwana harusi yupo romantic…(anatabasamu)haya na wewe bibi harusi onyesha makeke yako tuyaone kwenye utambulisho…twende sasa

(Christina anachukua kipaza sauti na kuanza kuwatambulisha ndugu zake wakiwemo wazazi wake, shangazi yake na ndugu wengine, kila mara wakitambulishwa ndugu hao husimama na kupungia watu mikono, anatambulisha mwisho anamalizia na mumewe)

Christina :( anacheka kidogo huku anamshika mumewe begani) na huyu ni mume wangu mpenzi wa moyo wangu, rafiki yangu na mshikaji wangu anaitwa Peter Renatus Mbeikya

(Watu wanapiga makofi Sana)

Mc :( anaguna kidogo) hapo kwenye mshikaji embu tufafanulie tafadhali)

Christina: si mshikaji tu

(Watu akiwemo mama yake wanacheka Sana)

Mc: kiaje

Christina: ki hivyohivyo…

(watu wanacheka)

Mc:(anaguna) haya bwana umekataa kuniambia nasusa

(Vicheko)

Christina: ukisusa wenzio twala

Mc: heeeeeee! Bibi harusi huyu… (Anacheka)

Christina :( anacheka)

Mc: haya sina cha kuongezea, naomba nimtangaze bibi harusi kuwa ndo mshindi wa mtanange huu

(Watu wanapiga vigelegele)

Mc: amekataa kuniambia kwanini anamuita mumewe mshikaji

(Watu wanacheka)

Mc: basi sawa muda wa keki…

(Keki inakatwa, maharusi wanalishana, kisha wanawalisha wapambe wao na baada ya zoezi la kulishana keki zinapelekwa kwa wazazi wa pande mbili na baada ya zoezi la keki kuna zoezi la zawadi. watu mbalimbali wanatoa zawadi na hatiamye kamati inayoongozwa na bwana Raymond Bembele)

Raymond:(Baada ya kufika mbele) habari za jioni mabibi na mabwana, mbele yenu ni kamati ya maandalizi ya sherehe hii, ili tusipoteze muda mwingi nijitambulishe kwa niaba ya wote…mimi ninaitwa bw. Raymond Bembele ni mwenyekiti wa kamati hii mnayoiona hapa mbele

(Watu wanapiga makofi)

Raymond: zawadi zetu kwa maharusi ni kiwanja na vifaa vya ujenzi kwa ajili ya kujenga nyumba yao na watoto wao

(Shangwe za kutosha zinaendelea mahali hapo)

Raymond: gari aina ya prado naona lipo hapo nje…tutawakabidhi, tiketi za ndege kwenda south Africa kwa ajili ya fungate na mapumziko mafupi…

Watu: woooo…w

Raymond:na pesa taslimu milioni sita… (anawakabidhi cheki) asante na Mungu awabariki

(DJ anaachia ngoma nzuri ya kuwarudisha kamati wakakae, wanaenda kukaa sherehe inaendelea na watu wanacheza, wanakula wanakunywa na kila kitu kinaonekana kipo shwari, maharusi wamefurahi, wageni waalikwa wamefurahi na Zaidi kamati imefurahi. sherehe imefana sana, Christina na Peter wanawashukuru sana wageni waalikwa na wazazi kwa ujumla)

Post a Comment

0 Comments