IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 57

 


SCENE 57: -

(jioni nyingine wiki kadhaa mara baada ya harusi ya Christina na Peter kupita, Edmond, Catherine, Raymond na Angelina wamekaa katika bustani safi iliyopo nyumbani kwa Raymond, wanajadili kuhusu harusi iliyopo mbele yao)

Edmond: hii harusi inatakiwa iwe bab’kubwa kama ya mastaa kwenye picha(anacheka)picha zenu mnazoangaliaga ITV

(Angelina na Catherine wanacheka)

Raymond: oh, finally naenda kumuoa kipenzi changu imekuwa Zaidi ya mwaka tangu nimekuwa nae

Edmond: uzuri wako umekaa na mkeo mtarajiwa hata kabla ya kumuoa

Raymond: ndo hivyo (anacheka kidogo)

(Christina na Peter wanakuja mahali pale)

Edmond: wow…wanandoa wapya kabisa mjini

Peter: eeh baba…mpo poa

Raymond na Edmond: poa

Christina :( anatabasamu) za hapa jamani

(Wanaitikia)

Edmond: za honeymoon?

Peter na Christina: nzuri tu

Raymond: wacha we… (Anamuangalia Christina) mbona Kama umenenepa

Edmond: na wewe (anampiga ngumi moja)

Raymond: utaniua unajua Mimi ndo bwana harusi pekee niliyebaki

Edmond: hai au?

(Wanacheka)

Angelina :( Kwa Christina na Peter) karibuni jamani niwaletee vinywaji gani?

Christina: chochote ukipendacho wewe

Angelina: eti ee… (Kwa Peter) Na wewe shemeji?

Peter: maji tu

Angelina: sawa (anaelekea kwenda jikoni)

Raymond: enhe…naona mama mwenye nyumba kaenda kuleta vinywaji sisi tuendelee na mazungumzo

Edmond: kabisa…

Christina: mlikuwa mnaongelea nini?

Catherine: harusi ya hawa ma staring

(Wanacheka)

Raymond: kwani muvi hii?

Catherine: Kwa mfano ingekuwa tamthilia mngekuwa ma staring

Edmond :( anatikisa kichwa) yaani wanawake bwana wao kila saa mnawaza tamthilia…tu…na wale wakalimani wenu utasikia yoooo anakujaaaaa

(Wanacheka Sana)

Angelina :( anakuja amebeba glasi mbili za maji kwenye trei)

Raymond: dear dada yuko wapi?

Angelina: yupo jikoni…

Raymond: si ungemwambia alete yeye?

Angelina: ana kazi nyingine...

Edmond: embu muache bana na wewe…

Angelina :( huku anawapa maji Christina na mumewe) karibuni sana

Christina: hivi Angelina wadogo na mama yako walishaondoka

Angelina: siku nyingi Sana watakuja kwenye harusi lakini

Christina: aha!!!Kumbe sikujua ndo kidogo nikuulize mbona sijawaona kwenye harusi?

Angelina: walishaondoka walikuja kusalimia tu

Christina: basi sawa… (kwa wengine) jamani tumekuja na habari hapa?

Raymond: ipi tena na wewe mbaya nzuri

Christina: eeh baba tuliza mzuka

Edmond: eti mbona unapanikigi sana wewe (anacheka)

Raymond: wewe, Mimi sasa hivi sitaki kukonda

Edmond: Na nini sasa

Raymond: Na mawazo…

Catherine: nyie hawa hawamalizi utani wao naomba tu mama utuambie hiyo habari

Christina :( anatabasamu) ah… (Anavuta pumzi ndefu) Mimi na mume wangu tunatarajia kuwa wazazi maanake nina ujauzito… (Anatabasamu)

(Wanalipuka na shangwe, vifijo na makofi kwa sana)

Edmond: kwahiyo habari za ujauzito zimefika mbili…

Christina: na nani tena? Angelina?

Angelina: hapana…

Edmond: mke wangu mpenzi Sana…Mrs.Catherine Mutalemwa…

Christina: wow…hongereni Sana

Edmond: hongereni pia jamani…

Raymond: party…tutoke jamani jioni tukajirushe

Edmond: wazo zuri…

(Wanafurahi Sana)

Edmond: bado Angelina

Angelina: baada ya ndoa... (Anafunika macho yake kwa mikono miwili ishara ya kuona aibu)

Raymond :( anaguna)

Catherine: eeh hiyo ndo vizuri maana wenzio hapa tumekuwa wajawazito baada ya ndoa (Kwa Raymond) sasa Shem unaguna nini?

Raymond: Mimi nataka sasa hivi

Edmond: embu kwenda huko…hili lisukuma vipi hili…

Raymond: mi nataka tu mtoto

Edmond :( anamtania Kwa kumsukuma kidogo) embu tupishe huko

Christina :( anacheka) yaani hawa…

Peter :( anacheka)

Raymond: hongereni Sana…

Peter: tunashukuru mwenyekiti

Raymond :( anacheka) nyie hilo jina (anaguna)

Angelina :( Kwa Peter na Christina) hongereni sana jamani

Christina: Asante katotoooo

Raymond: katoto…kazae hivyo hivyo

(Wanacheka Sana, wanaendelea kuongea na kufurahi na kupanga mipango mingi ya harusi ya Angelina na Raymond)

Post a Comment

0 Comments