IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 58

 


SCENE 58: -

BAADA YA MWEZI MMOJA NA NUSU

HARUSI YA ANGELINA NA RAYMOND

(KANISANI)

(Hayawi hayawi mbona yamekuwa wamesema haolewi mbona anaolewa, asubuhi iliyo tulivu kabisa machoni pa kila kiumbe chenye uhai na kisicho na uhai, siku hii imebarikiwa na bwana maana kuna hali nzuri kabisa ya hewa, kaubaridi kwa mbali na upepo mwanana unavuma na hali inavutia sana, ndugu jamaa na marafiki wa Angelina na Raymond wamekusanyika katika kanisa kubwa la T.A.G wakisubiri muungano kati ya Angelina na Raymond)

Christina :( Kwa mama yake) ah…hatimaye Raymond anamuoa mwanamke aliyempenda Kwa dhati

Mama: ndio mwanangu kila kitu kinakaa jinsi Mungu anavyotaka kikae unaweza kupanga hivi yeye akapanga hivi

Christina: Nina furaha Sana siku hizi mama…

Mama: nashukuru kusikia furaha yako mwanangu

(Raymond anafika akiwa na Edmond, Raymond amependeza kwelikweli suti yake inaonekana ni ya gharama sana)

Christina: bwana harusi huyo

Mama: kapendeza…kweli

Mrs.Bembele :( anamfuata mwanae) mwanangu…kipenzi changu (anambusu kwenye paji la uso)

Raymond :( anatabasamu) naam mama

Mrs.Bembele: umependeza Sana

Mr. Bembele :( anawajia) wow…Mr. Bembele junior umewaka (Anatabasamu huku anamshika bega)

Raymond: Asante baba…Asante kwa kila kitu…asante hata kwa kukubali penzi langu na mke wangu mtarajiwa…nakupenda sana baba

Mrs.Bembele :( anafuta machozi) nakumbuka zamani mlikuwa kila mkikutana mnagombana…ona Leo mnavyofurahia maisha pamoja, sifa na utukufu tumrudishie yeye aliyeziumba mbingu na dunia

Raymond: usiyakumbuke ya kale mama…tena Zaidi siku ya Leo sio ya kukumbuka mabaya yote yaliyowahi kutokea maana tutaiharibu bure siku hii

Mr. Bembele:(kwa Edmond) asante kwa kuwa rafiki mzuri kwa mwanangu…leo wewe ni bestman wake, inanipa Amani sana

Edmond :( anatabasamu) usijali baba tupo pamoja…

Mchungaji :( anakuja akitokea ndani ya kanisa) jamani bwana yesu asifiwe…

Watu: amina…

Mchungaji: Kwa utaratibu uliowekwa, naomba bwana harusi na bestman wake waje ndani ili tuwasubiri bibi harusi na matron wake…

(Watu wanafuata utaratibu)

Raymond :( anaenda mbele kabisa)

Edmond :( anamfuata nyuma)

Mchungaji: asanteni…sasa naomba utulivu wakati msafara wa bibi harusi unajiandaa kuingia kanisani

Mama Angelina :( anatabasamu wakati wote)

Raymond :( analengwa na machozi anajitahidi kuyazuia)

(Watoto wa kike tofauti wakiwemo wadogo zake Angelina wanapita mbele wakiwa wamebeba maua, wanapita kwa zamu mpaka wanaisha, baada ya tukio hilo anapita Catherine ambae anasimama kama matron wa Angelina)

Mrs.Bembele:(kwa mumewe) wow…harusi inapendeza kweli

Mr. Bembele: saaaana mke wangu

Mrs.Bembele: ona mtoto wetu kule mbele alivyopendeza

Mr. Bembele: Mungu alitupendelea mwenzangu alitupa mtoto… (Anaguna) sio kwa uzuri huo (anatabasamu huku anamuangalia mwanae aliyeko mbele anasubiri kumpokea mpenzi wake)

(Wakati huo wanaingia watoto wadogo kati ya miaka mitani na sita wanaingia huku wanamwaga maua yenye rangi nyeupe na nyekundu)

Watu: wow…

(Mlango unafungwa)

Mchungaji :( Kwa watu) sasa Kwa heshima kabisa tunaombwa kusimama Ili kumkaribisha bibi harusi...

Watu :( wanasimama)

(Lango linafunguliwa, Oh Yes!!!malkia amesimama akiwa amevalia gauni lenye mkia mrefu sana, veili lake ni refu limemfunika mwili mzima, nay eye anaonekana kwa mbali sana kupitia veili hilo lililonakshiwa kwa urembo mwingi.Angelina anatabasamu mara baada ya lango hilo kufunguliwa, wapiga picha mbalimbali wanampiga picha .akisindikizwa altareni na mdogo wake wa kiume (Angello) pamoja wanaanza kupiga hatua taratibu sana kuelekea altareni alipo Raymond na Edmond.Wakiwa njiani kuelekea altareni watu wanakuwa katika hisia tofautitofauti kuna watu wanalia,kuna watu wanafurahi tu,kuna watu wanashangaa aina ya shela alilovaa bibi harusi huyo,miongoni mwa watu wanaotoa machozi ya furaha ni mama mzazi wa Angelina na mume wake mtarajiwa.Angelina anatabasamu sana na mara zote anawaangalia watu waliosimama kwa heshima ya kumpokea yeye malkia wa siku hiyo.baada ya hatua kadhaa hatimaye yeye na mdogo wake wanafika altareni,Angello anamkabidhi dada yake kwa shemeji yake kisha yeye anaenda kukaa walipo mama na wadogo wengine,wakati huku nyuma Raymond anamshika mkono mpenzi wake na kupanda nae altareni,anamuangalia sana.Watu wanakaa mara baada ya Angelina na Raymond kupanda altareni)

Mchungaji :( anacheka kidogo) eeeh ni yeye au sio yeye

Raymond :( anacheka)

Mchungaji: embu mfunue tumuone…na wewe umuone

Raymond :( anamfunua) wow…wewe ni mrembo sana (kwa mchungaji) ni yeye

(Watu wanaangua kicheko)

Mchungaji: Ni yeye ee…

Raymond: kabisa

Mchungaji: hawajakubadilishia?

Raymond: hapana

Angelina :( anatabasamu vizuri)

Raymond:(anamuangalia Angelina) jamani Mungu kajua kuumba…tangu siku ya kwanza nakuona kama mwaka na miezi imepita…nafsi yangu ilikiri kuwa nakutaka wewe kuwa mama wa familia yangu sio uzuri wa sura na umbo bali uzuri wa moyo na tabia yako…ni mwanamke mchapakazi, mwenye upendo, mwenye heshima, mwenye kujali, nakupenda sana Angelina, namshukuru Mungu kwa kuruhusu leo hii iwe

Mchungaji :( Kwa watu) mpigieni bwana makofi mengi

(Watu wanapiga makofi na vigelegele)

Mchungaji: ndoa takatifu ya watakatifu na iwe takatifu (anawaangalia Angelina na Raymond) kaeni wanangu niwafundishe jambo kabla Mungu hajawaunga kuwa wamoja…

(Angelina na Raymond wanakaa)

Mchungaji: ni jambo la kuhuzunisha kabisa kuona mke na mume wanagombana na kuivunja ndoa, unajua ni mpango wa Mungu kwetu sisi wanadamu kuwa pamoja yaani mwanamke na mwanaume kuwa pamoja katika ndoa takatifu,mmeishi muda mrefu katika uchumba,mmejuana sasa ni jukumu lenu kuchukuliana nyinyi ni binadamu na haimpendezi Mungu hata wazazi kuona watoto wao wanaachana na kuvunja ndoa…vumilianeni,mkikosana ombaneni msamaha muwe wasiri sio mnagombana kila siku dada anajua,mama anajua jamii nzima inajua kuwa ,leo Raymond amegombana na mkewe..

Raymond :( anawaangalia Catherine na Edmond kisha anacheka)

Mchungaji: basi kwa kusema haya machache naomba tuanze taratibu za kufungisha ndoa hii... (kwa watu) je kuna yeyote mwenye pingamizi ya ndoa hii isifungwe?

(Kimya)

Mchungaji: basi Kwa maana hiyo naruhusiwa kufungisha ndoa hii kati Raymond Desmond Bembele na Angelina Deus…

(Mchungaji anawafungisha ndoa wawili hao huku watu wanashuhudia matukio hayo ya kheri. baada ya kufanya hatua zote zinazotakiwa hatimaye mchungaji anawatangaza Angelina Na Raymond kuwa mume na mke)

Mchungaji: alichokiunga Mungu binadamu hawezi kukipangua Nina watangaza Angelina Na Raymond kuwa mke na mume na ikawe Kheri kwenu na uzao wenu

(Vifijo, nderemo na vigelegele vingi vinaendelea katika kanisa hilo, Angelina na Raymond wanakumbatiana na kuukubali umoja wao wa kuwa mume na mke, watu wanapita mbele kuwapongeza wawili hao)

Mr. Bembele: hongereni Sana jamani…ikawe Kheri kwenu

Mrs.Bembele: mmependeza, hongereni Sana

Angelina Na Raymond :( wanatabasamu) asanteni Sana

Mama Angelina: hongereni Sana wanangu, Mungu awatunze

Angelina Na Raymond: amina mama

Christina: hongereni Sana mmependeza

Raymond: Asante mama katumbo…mbona huna tumbo?

Christina: bado ndo kwanza miezi miwili

Raymond: sawa. Tunasubiri kubeba katoto

Christina: usijali (anacheka kisha anaondoka)

Peter: hongereni Sana bibi na bwana Bembele

Raymond :( anawanyooshea kidole wazazi wake) wale pale

Peter: nyie Ni Mr & Mrs.Bembele junior

(Angelina, Raymond na Peter wanacheka sana)

(Watu wanaendelea kuwapongeza)

Mchungaji: sawa, vyeti vya ndoa vipo tayari Kwa ajili ya kusainiwa

Angelina na Raymond :( wanaenda kusaini vyeti vyao)

(mashahidi yaani Edmond na Catherine nao wanasaini vyeti hivyo. Baada ya zoezi la kusaini vyeti wanaruhusiwa kutoka nje na kwendelea na ratiba nyingine, nao pamoja na ndugu na jamaa wote wanatoka nje na ratiba nyingine zinaendelea. Wanapongezana, wanafurahi pamoja kisha wanapanda kwenye magari maalumu kwa ajili ya kwenda sehemu maalum kwa ajili ya kupiga picha za ukumbusho wa ndoa ya Angelina na Raymond)

Raymond :( akiwa kwenye gari yeye na mkewe) Mrs.Bembele…

Angelina :( anatabasamu) abeee

Raymond: umefurahi

Angelina: Sana… (Anataka kulia)

Raymond: usilie... (anamfuta machozi)

(Wanaendelea na safari huku kila mmoja wao ana furaha nyingi moyoni)

Angelina na Raymond: (wanapungia watu mikono)

Post a Comment

0 Comments