IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 7

 

SCENE 7: -

(Raymond amekaa ofisini kwake ila anaonekana amechoka sana sio chini ya mara kadhaa anapiga miayo, ambayo inamshangaza sekretari wake ambaye yupo hapo akipanga mafaili)

Sekretari: kaka…unaonekana una uchovu kweli

Raymond: yaani acha tu dada Glory…yaani ni matatizo…naamka saa kumi na moja nasafisha nyumba yangu, naosha vyombo nilivyolia jana yake usiku…nahakikisha kila kitu kipo sawa ndo nakuja kazini na huku natakiwa saa kumi na mbili na nusu ili saa moja kamili niingie kwenye kikao cha bodi yaani we acha tu

Glory: pole mdogo wangu, si utafute msichana wa kazi? Awe anakusaidia?

Raymond: Hilo nalo neno…nitafutie basi dada yangu

Glory :( anaguna) yaani kaka siwezi kukudanganya naweza kupata msichana ila wengi wao wanaweza wakawa si waaminifu…ukaja kunilaumu bure

Raymond: ndo ubaya, sasa nifanyeje dada je niedelee kuwa nafika kazini nalala au nifanyeje?

Glory: ila si nasikia una mchumba wewe?

Raymond: tena hata usinikumbushe hiyo mada

Glory: kwanini mdogo wangu

Raymond: mwanamke hajui hata kupika hata chai

Glory :( anashangaa) Hee!!!Kwanini?

Raymond: hata sijui…huyo sasa ndo mke wangu…wa maisha…si nitaumbuka mimi?

Glory :( anacheka) acha kukata tamaa mdogo wangu Mungu atakusaidia anaweza hata akamfanya abadilike

Raymond: ni ngumu kwa huyo mwanamke

Glory: pole mdogo wangu nakuombea yaliyo mema

Raymond: unasali wapi?

Glory: Lutheran

Raymond: Mimi nasali T.A.G ILA wazazi wangu wote ni wa katoliki

Glory: kwanini sasa wewe ukaamua kuwa mlokole

Raymond: maamuzi tu…

Glory: hongera kaka kwa maamuzi hayo mema nay a kupendeza (anacheka)

Raymond: (anacheka kidogo) kwahiyo umekataa kunisaidia dada…msichana?

Glory: nitajaribu

Raymond; au nisikuchoshe…ngoja (anampigia Edmond)

(simu inaita)

Raymond: hello brother, nambie

Edmond: poa my brother uko poa…?

Raymond: nalala tu mwenzio…Nina uchovu kweli yaani

Edmond: pole…oa… (Anacheka Sana)

Raymond: ah!!!Mpaka nije nipate wa kumuoa si nitakuwa nimekufa jamani

Edmond: kwahiyo nikusaidieje?

Raymond: nisaidie kaka…unaeza kunitafutia binti wa kazi anisaidie kazi mwenzenu

Edmond: mama mtu mzima au binti

Raymond: vyovyote bwana

Edmond: una bahati wewe kuna ndugu yake Catherine katoka Ngara juzi wanakaa nae hapo kwake, anatafuta kazi yoyote… hata za ndani tena nilitaka kukuambia sijui nikasahau vipi...yupo kwa Catherine

Raymond: Safi sana nan do maana nilikufikiria maana nilijua tu nitapata nachokitafuta kwako…embu mlete nitamlipa vizuri

Edmond: Kwa Leo haitawezekana maana nina kazi Fulani imenitinga labda tufanye kesho asubuhi kabla hujaenda kazini

Raymond: Ni mwaminifu?

Edmond: anaonekana ingawa simjui vizuri kwakweli

Raymond: umesema ni ndugu yake shemeji eeh

Edmond: ndio…

Raymond: we si ulisema shemeji yuko peke yake kwao?

Edmond: huyo ni mtoto wa mama yake mdogo

Raymond: sawa kaka…nashukuru Sana…maana dah…nahangaika Sana mwenzio

Edmond: naelewa Sana tu…ndugu yangu hivi (anaanza kucheka) huwa unadeki kweli jamani au ndo kupitisha ufagio tu halafu kwaheri mpaka kesho kutwa tena (anacheka)

Raymond: kwahiyo unanicheka mwenzio jamani

Edmond: sikucheki…nakuhurumia mdogo wangu

Raymond: haya fanya kuleta huyo mwanamke

Edmond: nitakuletea

Raymond: poa (anatabasamu kisha anakata simu)


Post a Comment

0 Comments