IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 8

 


SCENE 8: -

(Asubuhi ya siku ya pili, Raymond yupo chumbani kwake akijiandaa na siku, wakati anaendele kujiandaa anakumbuka kuwa ana miadi na Edmond, hivyo anampigia simu)

(simu inaita kwa muda mwisho inapokelewa)

Raymond: za asubuhi kaka

Edmond: poa mambo, ndo naingia getini kwako hapa, na uhakikishe kuna chai

Raymond :( anacheka kidogo) upo na binti?

Edmond: ndo hivyo… (Anaingia ndani) mambo Ramadhani

Ramadhani: poa mambo…

Raymond: wewe mbona sikuelewi mambo Ramadhani tena? (Anacheka)

Edmond: kwahiyo nilivyokuambia kuwa nipo getini uliona nakudanganya?

Raymond: ngoja niwapokee… (Anatoka nje ya chumba chake kuelekea sebuleni)

Edmond :( anaingia ndani akiwa na binti)

Raymond :( anapigwa butwaa baada ya kumuona binti) wow…umeniletea binti eeh

Edmond: ndio kama nilivyokuambia

Raymond: (Anajisemea moyoni) wazazi wangu walijitahidi kunipeleka nchi mbalimbali ila kote huko sikuwahi kuona mwanamke mzuri hivi…dah!!Haya si majaribu

Edmond: wewe…mbona huongei?

Raymond :( anamuangalia binti kisha anatabasamu)

Binti :( nae anatabasamu)

Raymond: dada…unaitwa nani…na je wewe ni mtu wa Ngara?

Binti: mi naitwa Angelina, ndio kaka mi ni mtu wa Ngara

Raymond: sawa…watu wa Ngara warembo sana

Edmond: tena?

Raymond :( anajishtukia) ah hata Shem mzuri yule yaani Sana tu, wewe humuoni?

Edmond: ah…kumbe…sawa…haya bwana huyu ndo dada wa kazi uliyeniagiza

Raymond: karibu dada (anajisemea moyoni) is it love at first sight…. Yaani nimemuona tu najihisi kumpenda

Edmond: we leo vipi yaani unakuwa kama una mawazo au (anamsogeza pembeni) hujafurahia?

Raymond: we Edmond umemtoa wapi binti mzuri hivi?

Edmond: Ngara…acha ujinga wako sio uje uanze kumbaka mtoto wa watu…yaani huko kijijini kwao wanampenda sana maana mtoto anajituma hana tabia za wanaume...

Raymond: anajituma ee

Edmond: Sana…yaani Catherine alinipa stori zake mpaka nikamfurahia so kaa na mtoto wa watu vizuri…

Raymond: bila shaka kabisa, nimekuelewa kaka Edmond…

Edmond: poa (anarudi kwa Angelina) haya mama umefika sasa ukae vizuri, heshima ni kitu cha muhimu sana mdogo wangu

Raymond :( bado anamuangalia Sana) una umri gani Angelina?

Angelina: ishirini na mbili…

Raymond: Mimi Nina thelathini na mbili

Edmond: kuna mtu kakuuliza umri wako (anacheka)

Raymond :( anatoka nje kumuita Ramadhani) Ramadhani…naomba uje mara moja (kisha anaingia ndani)

Ramadhani :( anaenda ndani) naam boss…

Raymond: jamani si nishakuambia kuwa sipendi unite boss. Usiniite boss bwana

Ramadhani: sawa nisamehe...

Raymond: usijali…sawa…sasa unamuona huyu ni dada wa kazi hapa…naomba ukae nae mpaka nitakaporudi toka kazini jioni

Ramadhani: sawa hamna shida (Kwa Angelina) binti Mrembo…Mrembo nambie…unaitwa nani

Raymond :( anaingiwa na wivu wa ajabu) sio sasa umeona kabinti ndo uanze kutongozatongoza kuwa makini saana…humu ndani ni kazi tu

Edmond :( anashangaa Sana) we vipi

Raymond: kwani nimesemaje?

(Wote wanacheka)

Edmond: hicho kibesi sijakielewa kabisa…kwahiyo mtu akisifiwa kwako kosa (Kwa Ramadhani) basi fanya kitu kimoja msifie yeye

Ramadhani:  basi poa...Dah!!Raymond we handsome, wewe Mnyarwanda au Msomali? (anacheka sana)

Raymond :( anacheka) ah!!Nyie nikianza kukuwasikiliza hapa sitoki…mi naenda jamani baadae

Edmond: lifti basi

Raymond: twende nikupe ofa mpaka ofisini kwako…

Edmond: poa

Raymond :( Kwa Angelina) sasa dada tupikie basi jioni nitakuja kula

Angelina: sawa kaka…

Raymond: halafu sijakuonyesha chumba chako?

Angelina: ndio kaka

Raymond :( anafungua chumba kimoja) haya chumba chako hiki hapa

Angelina :( anaingia huku kabeba mfuko wabluu wenye nguo Kama mbili hivi na viatu vilivyokatika) asante kaka…pazuri kweli jamani

Raymond: Asante sawa wewe kaa…hapa

Angelina: sawa kaka

Raymond :( anatoka humo chumbani) we Edmond…twende

(Wanatoka nje wanapanda gari kisha wanaondoka…wakiwa kwenye gari kuna machache wanayoongea)

Edmond: vipi unamuonaje huyu dada?

Raymond: wife material

Edmond: unasemaje?

Raymond: yuko vizuri Sana

Edmod: mdogo wangu stress zitakuua we kila ukimuona mtu wife material

Raymond: najisikia kumpenda sana Angelina

Edmond: Raymond…tuchungane basi…usije kumpa mimba mtoto wa watu

Raymond: nakutania…sasa nitampendaje Angelina hata baba hatoniruhusu, tulia kuwa na Amani kaka yangu handsome mume halali wa catherine

Edmond :( anacheka) umeanza (anaacha kucheka) poa Kama unasema hivyo haina shida mtu wangu

Raymond: muone umeshtuka Sana nilipokuambia nampenda…eeeh

Edmond: sasa utampendaje mtu ndo kwanza umemuona Leo

Raymond: huamini kuwa wengine wakimuona tu mtu hapohapo nafsi inakubali kuwa imeridhika…Angelina ni Mrembo sana hiyo haina ubishi

Edmond: sawa sina neno…

Raymond: she is so beautiful walahi jamani

Edmond: dogo kuwa makini bwana sitaki kesi na shemeji yako

Raymond: basi siongei tena (anaendelea kuendesha gari)

Edmond: ila utampenda huyu dada yuko vizuri (anacheka)

Post a Comment

0 Comments