I KILLED MY LOVER 10

 


SCENE 10: -

(Ni Jumamosi nyingine ya kawaida kabisa kama jumamosi nyingine, siku moja baada ya Liliana kupokea kipigo cha mbwa kutoka kwa shangazi yake ambae pia ni mlezi wake, Anna na Bella wapo nyumbani kwani hawaendi shule siku hiyo, Liliana anaugulia maumivu ya kipigo cha jana)

Shangazi: na ufue hizo nguo

Anna: mama naomba simu yako…

Shangazi: ya nini?

Anna: kuna rafiki yangu nataka kumpigia aje tusome

Shangazi:(anatoa simu yake na kumpa Anna) fanya haraka

Anna:(anaipokea kisha anaenda pembeni na kuzungumza kitu Fulani ambacho hakisikikin kwa walipo hapo maana anaongea kwa sauti ndogo sana)

Shangazi:(anatoa nguo nyingi sana chafu na kumtupia Liliana) fua zote hizi acha kujidekeza unadhani mama yako yupo hapa?

Liliana:(Analia sana) shangazi naumwa sana

Shangazi:(anamzaba kofi kubwa sana) pumbavu nimekuambia fua nguo ukimaliza pika chakula kitakachotufurahisha wote hapa mbwa wewe mama yako hayupo hapa

Anna: mama…

Shangazi:(kwa Anna) kelele (anarudi kwa Liliana) unasubiri nini umesahau kile kipigo cha jana?

Liliana:(anabeba nguo na kutoka nazo nje lakini kabla hajatoka)

(maafisa wale waliokuja jana yake wanaingia)

Shangazi:(anapigwa butwaa)

Elizabeth: tulijua tu…kuwa unamtesa huyu mtoto…

Julieth:(anamuangalia Anna) asante sana kwa ushirikiano wako

Anna:(kimya huku akimuangalia mama yake)

Edson: mama unashtakiwa kwa kosa la kumnyanyasa mtoto mdogo na kumnyima haki zake za msingi

Shangazi:(anashangaa sana) lakini huyu si mwanangu

Edson: hatujaona kama unamlea kama mwanao

Julieth:(kwa maafisa wenzie) niliwaambia mimi nilimuona mtoto ana vidonda vingi mwilini mwake na pia hana raha wala nini nikajua hapa lazima ile taarifa tuliyopewa ni ukweli

Shangazi:(anashangaa sana)

Julieth:(kwa shangazi) ndo nikapata wazo la kukukamata mara moja natamani hilo wazo ningeliwaza mapema Zaidi ila hakijaaharibika kitu

FLASHBACK

(Inaanzia jana yake maafisa walipoaga na kuondoka zao, nje kukawa na mazungumzo baina yao)

Julieth: kuna kitu hapa…hizi taarifa tulizopata zina ukweli mtupu ndani yake mtoto ni kweli kabisa anafanyishwa kazi na kupigwa sana na hiyo inaonyesha hata jinsi anavyotuangalia anahitaji msaada wetu

Elizabeth: nini kifanyike?

Julieth: naomba namba ya mwalimu Monica

Elizabeth:(anampa) unataka kufanya nini Julieth?

Julieth:(anaichukua huku anawaongoza wenzie) twendeni

(pamoja wanapanda gari walilokuja nalo na kuliondoa mara moja)

Elizabeth: bado hujanijibu…unataka kufanya nini?

Julieth:tunatakiwa tumkamate shangazi akiwa anamfanyia unyama mtoto huyu

Elizabeth: tutafanyaje?

Julieth:(anaipiga namba ya mwalimu Monica inaita mwisho inapokelewa) Eliza...embu ongea kwanza atajua mara moja kuwa anaongea na nani

Elizabeth:(anaipokea na kuiweka sikioni) eeh...Monica mambo vipi shoga yangu

Mwl.Monica: poa shoga kheri?

Elizabeth: kheri mami…embu ongea na mwenzangu kuhusu ile inshu ya yule mtoto aliyekuwa anateseka

Monica: aaah!!!sawa mi niliambiwa na mwanafunzi wangu je mlienda?

Elizabeth: ndio tulikuwepo hapa muda si mrefu ila hatujapata ushahidi

Julieth:(anampokonya simu) dada habari yako?

Monica: salama vipi?

Julieth: unaweza kuniunganisha na huyo mtoto aliyekuambia taarifa hizi?

Monica: bila shaka kabisa...

Julieth: sawa…sasa nitawakuta wapi?

Monica: Njooni hapa shuleni bado yupo darasani nitamuita tu mara moja

Julieth: sawa…tunakuja hapo sasa hivi

Monica: sawa karibuni…

Elizabeth: wewe noma…unadhani mtoto ataongea…

Julieth: kitendo cha kumwambia mwalimu wake ni kwamba tayari amechoka na anamhurumia sana mwenzie kwahiyo atafanya kila kitu amsaidie mwenzie

Elizabeth: good plan

(Gari linaendelea kwenda wanaendesha na baada ya dakika kadhaa wanafika shuleni hapo, haraka wanampigia mwalimu monica na bila kupoteza muda mwalimu Monica anakuja kuwapokea)

Monica: karibuni sana

Edson: hatujaja rasmi…

Monica: naelewa nitasema tu nyinyi ni ndugu zangu…

Julieth: haya muite mtoto…

Monica: tayari yupo ofisini kwangu maana mliposemaa hivyo nimemuandaa…

Elizabeth:mi naona umuite tusimame nae pale chini ya mti tuwe kama vile tunapiga stori

Monica: sawa (anaondoka kuelekea ofisini kwake na baada ya muda anaruddi akiwa amemshika mkono Anna)

Julieth: oh…binti mzuri mzuri hujambo?

Anna: sijambo…shikamoo (kwa heshima anawasalimia wote)

Maafisa:(wanaitikia pamoja)

Julieth: haya...tuambie ulichomuambia mwalimu…kuhusu mtoto kuteseka

Anna: huyo mtoto ni binamu yangu…ni mtoto wa shangazi yangu…wazazi wake walifariki kwa ajali walipofariki wazazi wanguwakapewa jukumu la kumlea…sasa halelewi inavyotaakiwa anapigwa, anafanya kazi zote na mbaya Zaidi baba yangu ambae ni mjomba wake anambaka kila usiku…namhurumia sana na ni mtoto mdogo sana

Elizabeth: sana jamani tutamsaidia…

Julieth: sasa cha kufanya hapa ni kitu kimoja cha akili sana…nitakupa namba yangu...na tutakuwa tumekaa sehemu standby akianza tu…mambo yake nipigie

Anna: sina simu…

Edson: unaweza kuchukua simu ya mama yako bila yeye kujua na ukafanya tulichokuambia bila yeye kujua sawa ee

Anna: sawa...

Elizabeth: tunashukuru kwa msaada wako tunakutegemea sana…

Anna: haina shida

Julieth: poa basi tusipoteze muda sana mwanangu ni bora tukuache ili uendelee na masomo

(maafisa wanaondoka huku Anna na mwalimu Monica wanaenda kuendelea na kazi zao)

 

END OF FLASHBACK

Julieth:(kwa shangazi) sijui kama unaelewa kuwa unachofanya ni kibaya mpaka mwanao anachukia hiyo hali kwahiyo huna cha kujitetea na tayari polisi wapo nje hapo kukusindikiza rumande tunakufungulia mashtaka

(polisi wanakuja na kumshikilia shangazi na kuondoka nae)

Shangazi:(anamuangalia Anna vibaya sana mithili ya simba kaona swala na anataka kumla)

Anna:(wala hajali)

Bella:(Analia) mama

Anna:(kimya huku kamkumbatia Liliana)

Bella:(kwa Anna) yaani sababu ya huu uchafu (anamnyooshea kidole Liliana) umemfanya mama yetu kaenda jela

Anna: wewe koma na tena ukome zaidi huyu sio hausigeli wenu ni mwenye nyumba hii

Bella: nampigia baba sasa hivi…

Anna: fanya haraka kabisa…mpigie huyo baba yako…huyo mbwa anayebaka…watoto wadogo na bado yeye…tunatafuta ushahidi tu na yeye awekwe nguvuni

Bella: una roho mbaya sana... (Anaingia ndani kwa hasira)

Anna:(kwa Liliana) basi mdogo wangu…yameisha mama na baba watalipakwa yale yote waliyokutendea usijali mama umesikia?

Liliana: sawa…dada nashukuru kwa kunisaidia mama angekuwepo angekupa zawadi dada yangu (machozi yanamlenga) maskini wazazi wangu wangekuwepo leo…ningekuwa shule nzuri mimi na sio shule hizi

Anna: hapana usiseme hivyo mdogo wangu mimi nipo hapa kwa ajili yako na ninakupenda sana na nitakuwa kama mama yako nitakupigania kama mama yako usijali

Liliana: Asante dada Anna

Anna: usijali

(Wanakumbatiana huku kila mmoja wao anaonekana ana furaha)

Post a Comment

0 Comments