I KILLED MY LOVER 11

 


SCENE 11: -

(Ni asubuhi na mapema kumepambazuka vyema, kwa kuwa ni siku ya jumapili watu wanaanza kwenda kwenye nyumba za ibada ili kumshukuru Mungu, katika nyumba ya Liliana anapoishi kama mtumwa nao wanajiandaa kwenda kanisani, Anna anampa Liliana gauni zuri ili nae aende kumtukuza Mungu wake, wanajiandaa kutoka lakini kabla hawajatoka, shangazi yaani mama yao Anna na Bella anaingia)

Bella:(kwa furaha isiyo ya kifani) mama… (anamkimbilia na kumkumbatia) shikamoo mama…

Shangazi: marahaba mwanangu (anamgeukia Anna) hujafurahi kuniona

Anna:(anaonyesha hasira wazi) shikamoo mama

Liliana:(kwa sauti ya unyonge) shikamoo shangazi

Shangazi:(kwa jazba) pumbavu sana wewe yatima usiyekuwa na wazazi wala ndugu

Anna:(anapandwa na hasira) mama…

Shangazi:(anaendelea kuongea kwa jazba) hivi kwa mawazo yako ulidhani nitafungwa? mimi jeshi kubwa ndugu yangu na hakuna atakaenishinda…umeelewa sio hao maafisa wala mapolisi wote nimewaweka kiganjani mwangu

(Mjomba anaingia akitokea nje)

Shangazi: mume wangu mpenzi amekuja leo asubuhi sana kunifanyia mpango nitoke

(Bella, shangazi na mjomba wanacheka kwa dharau)

Anna:(anawaangalia kwa hasira sana)

Shangazi:(kwa Liliana) sasa nitakachokufanyia hautaamini…yaani umenichokoza vibaya sana wewe ni wakunilia timing mimi?

Liliana: sio mimi shangazi mimi nitawezaje kupigana na wewe shangazi?

Anna:(anasikia uchungu sana) mama ni mimi ndo nilimwambia mwalimu na wale maafisa wakaja nyumbani kwetu siku ile sorry sio nyumbani kwetu nyumbani kwa Liliana

Shangazi:(anacheka kwa dharau) eti nyumbani kwa kina Liliana…. yeye hana chake hapa mama yangu na nikikumbuka ulivyokuwaga unadeka tukija hapa ndo tunakuwa wafanya kazi wako ni muda wetu sasa wa kutesa hiyo inaitwa kutesa kwa zamu

Anna: unatesea kwenye nyumba ya watu? mama Liliana alifanya fadhila kukubali sisi ndo tumlee alipokubali tuje tuishi nae…inakuwa sio vizuri wala sio busara tunachofanya kumbuka tulipokuwa na leo hii tunaishi pazuri

Mjomba:(anaingilia) kimya wewe mtoto usiyekuwa na heshima hata kidogo kwa wazazi wako…wewe unajua nini?

Anna: sijui chochote Zaidi ya kumuonea huruma binamu yangu…

Shangazi: eti binamu…yaani undugu ulikufa siku wazazi wake walipokufa

Anna: hapo ndipo mnapokosea wazazi wangu na ndio maana basi baba anambaka binamu kwa kisingizio kuwa undugu umekwisha…

Mjomba:(anashikwa na kigugumizi) nani…alikuambia?

Anna: nilikuona jana usiku kwa macho yangu, ulimtoa Liliana chumbani kwetu na kumpeleka stoo… (anatokwa na machozi) baba…Liliana bado mtoto sana bora hata angekuwa mkubwa kidogo jamani…maskini hawezi hata kujisimaia hawezi hata kupiga kelele kwahofu yakwamba utamuua

Mjomba:(anainamisha kichwa)

Shangazi: utakuwa ulikuwa unaota mwanangu

Anna: nilimuona kwa macho yangu mawili na wala sio ndoto mama…ila tu nilishindwa kufanya lolote kwa aibu niliyopata sikutaka kuamini kuwa baba yangu mzazi anaweza kumfanyia haya mpwa wake…

Shangazi: acha kumshuhudia uongo baba yako Anna

Bella:(amekaa kimya huku anakumbuka kuwa hata yeye alimuona baba yake akimchukua Liliana na kwenda nae nje)

Anna: sisemi uongo mama sasa niseme uongo inisaidie nini mimi?

Shangazi: mume wangu hawezi kufanya kitu cha kipuuzi kama hicho…

Anna:(machozi yanamtoka) najuta na ninajionea aibu kwamba huyu baba ni baba yangu mzazi

Shangazi: acha kuongea upumbavu wewe mtoto usiye na akili vizuri

Liliana: dada acha tu msije mkagombana…na wazazi wako

Anna: naishangaa hii serikali hivi polisi inashindwa kutetea haki za watoto mpaka watu wanapata nafasi ya kupata dhamana hata baada ya kuwepo kwa ushahidi wa kutosha?

Shangazi:(anacheka kwa dharau) ushahidi haukuwepo ndo maana nilipatiwa dhamana… hakuna atakayeniweza kwa hili

Anna: pengine uko sawa au pengine hauko sawa kila kitu kipo mikononi mwa Mungu

Shangazi: Mungu??/Mungu gani unayemzungumzia wewe

Anna: aliyeziumba mbingu na dunia na kila kitu kinachoonekana na kisichoonekana…ni kweli leo umetoka kwa dhamana na ni kweli baba unajifanya hujui nachozungumzia ila amini nakwambia ipo siku Mungu atakuadhibu kwa jinsi anavyojua Mungu huyu sio kipofu wala kiziwi hata asione wala asisikie yeye ni mkuu na yeye peke yake ndo atawaadhibu… (anamshika mkono Liliana) twende mdogo wangu…

Shangazi: unadhani kuna sehemu ataenda huyu mbwa? haendi popote…nimerudi unadhani ni nani atanitengea maji ya kuoga na kunipikia chakula

Anna: mama, Liliana bado mtoto mdogo anahitaji kuishi maisha yake kama mtoto mdogo

Shangazi: nitakutandika…wewe unajua nini? hujui lolote mshenzi wewe unajifanya kubishana na mimi unadhani utanishinda? bora uwe mpole na kufata nayokuambia…mimi ndo mkuu na malkia wa nyumba hii na nitabakikuwa hivyo hata wazazi wa huyu mbwa wakifufuka hakuna atakayenishinda

Anna: mama mbona uko hivi jamani mama yangu?

Shangazi:(anamvuta Liliana kwa nguvu) embu njoo huku jikoni

Anna:(anajaribu kumsaidia Liliana)

Shangazi:(kwa Anna) acha kujifanya una huruma mshenzi wewe, wewe ni mwanangu na ni lazima uwe kama mimi na si vinginevyo (anamsukumiza Liliana kwa nguvu) nenda jikoni haraka mshenzi wewe… nipikie chai na uniandalie maji ya kuoga…

Liliana:(anatembea taratibu)

Shangazi:(anamfuata na kumpiga vibaya sana kisha anamsukuma)

Liliana:(anaanguka chini) shangazi

Shangazi: ninakutuma kitu naomba uelewe...kwamba nikimtuma mtu kitu nataka afanye haraka na si kujivuta

Liliana: samahani shangazi…nisamehe shangazi

Shangazi: leo hautakula chakula chochote…unaniletea mimi madeko nimekuwa mama yako? mfuate kaburini…na sijui ilikuwaje tu wakazikwa kwenye uwanja huu nitaenda kuwafukua nitupe mifupa yao huko nje

Liliana:(Analia sana)

Anna:(anajikuta anatokwa na machozi)

Liliana: shangazi nimeumia…

Shangazi: kwahiyo kama umeumia mimi itanisaidia nini? au inanihusu nini? nitakuadhibu kwa kunifanya mjinga mwenzio na kwenda kuwaita hao wajinga wenzio hapa eti wanikamate

Anna: nimesema mimi ndo niliwaita hapa

Shangazi: sijali, hasira zangu zote zipo kwa huyu mbwa.,.

Anna: nitakutengea maji na kanisani siendi tena…nakupikia chai Liliana ameumia

Shangazi: nataka afanye hivyohivyo asilete uzuri hapa

(Liliana anaenda jikoni huku Anna anamfuata nyuma, wanawasha jiko kwa kusaidiana wanafanya kila kitu anachotaka shangazi ambae kwa sasa anajiita malkia wa nyumba ile ya kifahari. wakati Anna na Liliana wanafanya kazi Bella, shangazi na mjomba wamekaa sebuleni kama mabosi Fulani.Liliana na Anna wanaendelea na shughuli zao bila kipingamizi)

Anna: Vumilia binamu yangu

Liliana: nimewakumbuka sana wazazi wangu

Anna: jikaze binamu jamani

Liliana: natamani kujikaza lakini siwezi nimechoka natamani kufa Anna

Anna; usiseme hivyo sasa ukifa mimi nitabaki na nani

Liliana: na Bella

Anna: (anaguna kidogo)

Liliana: mbona unaguna?

Anna: acha tu binamu (anaendelea na kazi za hapa na pale)

Post a Comment

0 Comments