I KILLED MY LOVER 9

 


SCENE 9: -

(asubuhi ya siku nyingine tena Liliana akiwa anaendelea na kazi zake za kila siku kama mfanyakazi wa nyumba hiyo, ghafla mlango wa sebuleni unagongwa, kwa kujivuta shangazi yake anaufungua mlango na kukutana na watu ambao hawafahamu)

Shangazi: karibuni

Watu: asante sana…

Mwanamke 1: habari za hapa?

Shangazi: salama…

Mwanaume: tunaomba uturuhusu tuingie sisi ni maafisa kutoka taasisi ya haki za watoto…tunaomba tuzungumze mawili matatu...

Shangazi:(anasita kidogo) kuna nini? mbona siwaelewi?

Mwnamke 2: turuhusu tuingie tutakujuza usijali

Shangazi:(anawaruhusu kishingo upande)

(Maafisa wanaingia ndani na kuketi)

Shangazi: niwahudumie nini? chai, kahawa, juisi au nini?

Mwanaume: usijali tupo sawa kabisa…asante kwa kujali

Shangazi;(anakaa kimya na amepooza kama kuku kamwagiwa maji)

Mwanamke1: ndio kwanza tujitambulishe labda kwa majina yetu…mimi naitwa Elizabeth Kapera

Mwanamke 2: mimi naitwa Julieth Julius

Mwanaume:na mimi naitwa Edson Edward…

Elizabeth:na sisi ni maafisa wa haki za watoto…tunaangalia haki za watoto majumbani na mashuleni

Shangazi: sawa…kwahiyo niwasaidie nini?

Elizabeth: kuna watoto wangapi hapa?

Shangazi: wawili…wanangu…Anna na Bella

(Liliana anapita akiwa anaelekea chumba cha kina Anna)

Julieth:na huyo?

Shangazi: oh(anajichekesha)uzee nao mzigo si nilimsahau…ndio na yeye ni mtoto anakaa hapa…

Elizabeth: okay (anajisemea moyoni) okay sasa huyu mtoto anaweza kuwa ndo huyo mtoto…

Julieth: kuna mtu kweli anaweza kusahau idadi ya watoto wanaoishi nao?

Shangazi:(anajichekesha)

Elizabeth: hao watoto wawili uliowataja wako wapi?

Shangazi: wapo shuleni

Julieth: huyu yeye haendi?

Shangazi:(anajichekesha)

Edson: unajua…sisi tumepata habari nyingi sana kuhusu huyu mtoto…

Shangazi:(anaanza kutetemeka) habari gani?

Elizabeth: huyo mtoto anaitwa Liliana…ni mtoto wa marehemu wifi yako…hii nyumba ni yake yaani ya wazazi wake lakini anaishi kama mtumwa, mnamnyanyasa sana mpaka kimwili

Shangazi: hapana hiyo sio kweli…

Elizabeth: anabakwa huyu mtoto…

Shangazi: tumuite tumuulize habari hizo…

(maafisa wanaangaliana)

Elizabeth: muite…

Shangazi :(ananyanyuka kisha anaenda alipo Liliana na kumnong’oneza jambo Fulani) wakikuuliza chochote usiseme ukweli na ukisema ukweli nitakumaliza umeelewa?

Liliana;(kwa unyonge anaitikia) sawa shangazi

Shangazi:(anarudi sebuleni huku anajichekesha) mtoto anapenda kazi huyu

Elizabeth: anapenda kazi au unamlazimisha azipende

Shangazi:si anakuja mumuulize…

Elizabeth:(anaguna)

Liliana:(anakuja huku akiwa amenyong’onyea sana)

Julieth: maskini…halafu mtoto mdogo sana…mbona kama huna raha (anamvuta na kumpakata) eti mama mbona huna raha hivyo? Unateswa?

Liliana:(anatikisa kichwa kuashiria kukataa)

Elizabeth:(anamuita) haya njoo uniambie mimi mwanangu

Liliana:(anaenda kwa Elizabeth huku anamuangalia shangazi yake)

Elizabeth: nambie shangazi huwa anakupiga? je huwa unapika na kufanya kazi zote? mjomba je…huwa anakufanyaje usiku?

Liliana:(anajikuta anatokwa na machozi)

Shangazi:(anaanza kuingiwa wasiwasi)

Edson: usimuangalie shangazi

Liliana:(yupo kama vile kuna kitu anawaza)

Elizabeth: niambie…mwanangu hakuna atakayekupiga…sisi tupo…

Shangazi: labda hataki kusema jamani mbona hivyo?

Elizabeth: nadhani mama ungetuacha na mtoto…tumuulize maswali mawili matatu…

Shangazi: muulizeni na mimi ni mlezi wake nina haki ya kuwepo hapa

Edson: mtoto anaonekana hana raha na wewe…kabisa jamani

Shangazi: ndo alivyo huyu akiona watu mbona tukiwepo peke yetu hafanyi hivi?

Julieth:(anamuangalia shangazi kwa muda)

Shangazi:(anaonyesha jazba)

Julieth: twendeni…jamani haya mambo ya familia

Shangazi: wewe una akili mwaya…eti mnanifukuza kwangu

Elizabeth: nisamehe mama

(wanaondoka kuelekea nje)

Julieth: kuna kitu hapa taarifa tulizopata ni za kweli kabisa na mtoto anaonekana kabisa kuwa anateseka anapigwa na kufanya kazi na anaumia sana…we fikiria kitendo cha kumuuliza tu mtoto mdogo kama yule machozi yanamtoka yenyewe yaani ndo muone kuwa ana uchungu wa muda mrefu

Elizabeth: nini kifanyike?

Julieth: nitawaambia wala msijali huyu mtoto lazima tumtoe kwenye mateso haya makali…

Elizabeth: una mpango gani?

Julieth: naomba namba ya mwalimu Monica kama hautajali

Elizabeth:(anachukua simu kisha anampa namba za mwalimu Monica)

Julieth:(anazichukua na kuziandika katika simu yake) okay asante sana…twendeni…

(Kwa pamoja wanaondoka mahali pale)

(Huku ndani walipo Liliana na shangazi yake kipigo kwa Liliana kinaendelea, mtoto anapigwa kama mbwa)

Liliana:(kwa uchungu) nisamehee shangazi

Shangazi: wewe ulishindwa kuonyesha uso wa furaha? kwani huli humu ndani?

Liliana:(huku Analia kwa uchungu) nisamehe shangazi sitarudia tena

Shangazi:(anampiga na mikanda mara kadhaa tena kwa nguvu na bila huruma) kufa mshenzi wewe

Liliana:(anazimia)

Shangazi: mshenzi Sana...KUFAAA!!! (Anaingia ndani akimuacha hapo bila msaada wowote)

Post a Comment

0 Comments