I KILLED MY LOVER 13

 


SCENE 13: -

(Liliana anatembeatembea huku na huku na anaonekana amechoka sana na kwakuwa ana njaa sana anaomba msaada watu mbalimbali)

Liliana: naomba unisaidie mama…nina njaa

Mwanamke: embu toka hapa…kwani huna wazazi? Mnakimbia kwenu mnakuja kusumbua watu mitaani (anamsukuma) embu toka hapa (Anaondoka zake)

Liliana:(anaanguka na anajikuta Analia sana) sina mama wala baba na wala sina ndugu…nipo peke yangu kwenye hii dunia

Mwanamke:(anampuuzia na kuondoka zake)

Liliana:(Analia sana tena kwa uchungu sana) mama…uko wapi? nateseka mimi…nimekimbia kutoka kwenye nyumba yangu kabisa…na sasa sina hata sehemu ya kula wala kulala ...mama, baba kwanini mliniacha…napigwa nabakwa… (anapiga magoti) Mungu nimeumizwa sana maishani mwangu kwanini usinichukue tu, nichukue tu na mimi niende kwa baba na mama yangu nikapumzike sitaki kuishi tena nimechoka Mungu wangu

(Watu wanampita tu tena wengine wanamuona kichaa)

Liliana:(anaendelea kulia sana kwa uchungu)

(Upande wa nyumbani kwao kina Liliana walipo mjomba, shangazi na binamu zake)

Anna:(anaonekana hana raha kabisa)

Belle: sasa kama aliamua kuondoka si tumuache?

Shangazi: atajua mwenyewe bwana…mtoto kaanza umalaya akiwa bado mdogo atakuwa ameenda kwa wanaume wake

Anna: mtoto wa miiaka saba mama?

Shangazi: anashindwa nini?

Anna: sidhani na kwanini tusiende kutoa taarifa polisi

Shangazi: embu niondokee na upuuzi wako hapa

Anna: mama embu fikiria chukua mud ahata dakika moja mama tumia ubinadamu mama na tumtafute Liliana kwanza tunakaa kwenye nyumba yao…ambayo ni nyumba yake…

Shangazi: hivi huyo Liliana akija akadai hii nyumba unadhani utakuwa na sehemu ya kukaa?

Anna: sidhani kama Liliana ana roho mbaya…

Shangazi huna hata aibu mshenzi wewe kaa utulie hapo na unisikilize mimi…mimi ndo mama yako na ndo mwenye maamuzi hapa nyumbani hata baba yenu hana usemi

Mjomba:(amekaa kimya hana usemi)

Shangazi:au nadanganya (anamuangalia mumewe)

Mjomba: hapana hudanganyi mke wangu wewe ndo mwenye maamuzi yote

Anna:(anashangaa sana) baba…wewe si ndo kichwa cha familia yetu? na hii nyumba ni ya dada yako na mumewe…inakuwaje huna maamuzi yoyote?

Shangazi:(anamnong’oneza) ukinigeuka tu nitaenda polisi kusema ni kweli ulikuwa unambaka mpwa wako si unajua adhabu ya kubaka? sio polisi tu hata jamii nzima itakuadhibu…kwahiyo kaa hapo utulie na kunisikiliza maamuzi yangu yote

Mjomba:(kwa unyonge) sawa…usijali

Anna: baba kuna nini?

Mjomba: yaache tu mwanangu…na kama binamu yako amepotea basi hiyo ni kazi ya Mungu kumtunza au kumrudisha sio jukumu letu

Anna:(anashangaa sana) baba

Mjomba:(ananyanyuka na kuingia chumbani kwake)

Shangazi:(anacheka kwa kejeli)

Anna: baba kuna nini lakini?

Mjomba:(anaingia ndani na kufunga mlango)

Anna: mama…

Shangazi: embu usinsumbue na huyo sijui binamu yako…acha afie huko…hana faida

Anna: mama

Shangazi: kapike huku msichana wenu wa kazi kakimbia (anacheka kama mazuri) kuanzia leo utakuwa unapika mpaka pale tutakapopata msichana wa kazi

Anna:(anasikitika)

Shangazi: fanya tu kazi mwanangu kesho tu nakuletea msichana wa kazi (anaingia ndani alipo mumewe)

Mjomba: unachofanya sio kizuri kabisa mama Anna…

Shangazi: nafanya nini?

Mjomba: kila kitu…

Shangazi: wewe je ulichofanya ndo kizuri?

Mjomba: sio kizuri na ninajuta kumbaka mtoto wa marehemu dada yangu…na ninatamani nimuone mpwa wangu na kumuomba msamaha na kumrudisha aishi hapa kama malkia wa nyumba hii maana hii nyumba ni ya kwake

Shangazi:(anashikwa na hasira) nyamaza na nikusikie tena unaongea kuhusu huyo mdudu kurudi kwenye nyumba yangu nzuri kama (anaangalia huku na huku) hii wanangu wanahitaji maisha haya na sio maisha tuliokuwa tunaishi

Mjomba: hii nyumba na haya maisha sio yetu mama Anna haya maisha ni ya Liliana mtoto uliyekuwa unampiga kama punda uliyekuwa unamlaza na panya stoo…

Shangazi: maisha yake yalikufa pamoja na wazazi wake…na usinichanganye nitaongea siri nyingi tu…usinichezee tena usinichezee kweli

(Wakati huo Anna anapita nje ya chumba hicho, ila anajikuta anasimama kusikiliza maongezi ya wazazi wake)

Shangazi: nitawaambia watoto na huyo panya unaetaka arudi…

Mjomba: nimejuta maisha yangu yote na tangu dada yangu amekufa sina amani kabisa

Anna:(anajisemea moyoni) nini kinaendelea…

Shangazi: unaweza ukaniona mimi ndo mtu mbaya ila wewe ndo mbaya Zaidi na hii roho nilionayo sasa ni wewe ndo umenifundisha mara baada ya kuona unaweza kufanya chochote hata kwa ndugu yako ili upate maisha mazuri…

Mjomba: ongea taratibu mama Anna…

Shangazi: ulimuua dada yako na shemeji yako na ukataka kumuua na mpwa wako ili upate maisha mazuri…kwa bahati mbaya mtoto akapona…ilikuudhi sana hiyo hali ulikubali kumlea mtoto ila ukapanga kumkomesha kwa kumtesa sana ili aondoke mwenyewe…sasa leo unataka arudi ili iweje huku wewe mwenyewe ulipanga yote haya?

Anna:(anaziba mdomo kwa mshangao)

Mjomba: ninajuta tena najuta sana kwa kusababisha ajali kwa kukata breki kwenye gari ya dada yangu…

Shangazi: sasa wewe unadhani…umenionjesha maisha mazuri halafu sasa hivi unataka kunifanyaje? wewe tulia ameshaondoka na hicho tulichokuwa tunataka

Anna:(anasikitika sana) Mungu wangu…baba ndo alisababisha ajali kwa wazazi wa Liliana? aisee (anaondoka na kukimbilia chumbani kwake)

Mjomba: lakini wewe ndo ulinishauri

Shangazi: ulikuwa na uwezo wa kukataa nakusimamia kwenye msimamo wako…badala yake usiku ule ulikuja hapa na kukata breki na kurudi nyumbani bila mtu yeyote kukuona…kwahiyo kila mtu anajua kuwa ilikuwa ni ajali

Mjomba:(anasikitika sana) najuta kwa kila kitu

Shangazi: pole (ananyanyuka na kuondoka zake)

Mjomba:(anabaki anasikitika na kujuta kwa kila kitu alichowahi kufanya kwa kifupi moyo wake unauma kwa matokeo yaliyotokea kwa matendo yake)

Shangazi: (anamchungulia mume wake)

 

 

Post a Comment

0 Comments