I KILLED MY LOVER 14

 


SCENE 14: -

(Liliana anatembea njiani na anaonekana ana njaa na amechoka sana, Analia sana na anaonekana amekata tamaa kabisa na maisha)

Liliana: bora ningekufa tu (Analia)kuliko kuteseka hivi bora nife tu

(Wakati Liliana analaani na kutamani kifo kuna gari linamfuata kwa nyuma yake na linaenda kwa mwendo mdogo sana na inaonekana huyo mtu kama anamvizia liliana)

Liliana:(anagundua gari nyuma yake anajaribu kukimbia)

Mtu kwenye gari:(anajaribu kumuita)

Liliana:(anasimama na kuangalia nyuma anagundua kuwa ni mwanamke mrembo sana mwenye umri kati ya miaka 40 mpaka 45)

Mwanamke: hata usiogope mwanangu…sitakudhuru nakuahidi hivyo

Liliana:(anaanza kulia) niue tu maana nimechoka sana kuishi niue tu mama nigonge na gari yako nife mama

Mwanamke: siwezi kukuua wala kukudhuru (anashuka kwenye gari lake la kifahari) usijali…nimekuona muda mrefu sana unaonekana una uchungu sana…mtoto mdogo sana wewe nini kinaweza kuwa kinakusumbua mwanangu?

Liliana:ni hadithi ndefu sana…mimi ni yatima sina mama wala baba

Mwanamke:na ndugu je?

Liliana:(anaendelea kulia sana) ni hadithi ndefu sana…

Mwanamke: mimi naitwa Bianca…ni mfanyabiashara nina biashara nyingi sana sijaolewa na wala sina mtoto…na ninatamani sana kuwa na mtoto wa kuishi nae

Liliana:(anaogopa sana)

Bianca: twende nyumbani kwangu

Liliana: hapana… (Anakataa na kujaribu kukimbia)

Bianca: mimi nakuhakikishia kuwa sitakudhuru nataka mtoto tu…jamani wanaume wangu wananikimbia maana sijawahi kumzalia yeyote hapo nimemuomba Mungu anipe mtoto…

Liliana:(anakimbia na kumuacha Bianca hapo)

Bianca: jamani mi wala sina nia mbaya jamani ninatamani tu mtoto wa kuishi nae sina mtoto nina wafanyakazi tu na sina Amani…nahisi mtoto atanipa Amani nayotafuta…nimemuona huyu mtoto tangu jana…na nimewaza tu kuwa anahitaji msaada…

Liliana:(anajikuta anarudi alipo Bianca)

Bianca:(anajiandaa kupanda gari lake ili aondoke)

Liliana: mama…

Bianca:(anamgeukia) nambie mwanangu?

Liliana: naumwa tumbo…

Bianca: una njaa mwanangu...twende nyumbani…

Liliana:(anapanda kwenye gari ingawa anaonekana ana wasiwasi sana)

Bianca: usiogope nimekufatilia kama siku mbili hivi sio nimekurupuka…sina mtoto na nina mali nyingi sana…ninaishi na wafanyakazi kuna mtunza bustani kuna dada wa usafi, kuna mpishi kuna mlinzi wote hao hawanipi ile faraja nayotamani kupata…nahitaji mtoto

Liliana :( anamuangalia chinichini)

Bianca :( anachukua biskuti na kumpa) kula hizi biskuti kabla hatujafika nyumbani…

Liliana :( kwakuwa ana njaa Sana anapokea na kuanza kula)

(Wanaendelea na safari na baada ya muda wanafika katika jumba safi la kifahari la Bianca.Bianca anapiga honi na haraka mlinzi anafungua geti)

Mlinzi: shikamoo anti

Bianca: marahaba…funga geti…

Dada wa usafi: shikamoo anti…

Bianca: marahaba… (Anaegesha gari katika maegesho)

Mpishi :(anafungua buti na kutoa vitu) leo naona umekuja na mgeni

Bianca:(anatabasamu) ndio…ingawa mwenyewe hajiamini… anaogopa kweli yaani (kwa Liliana) karibu nyumbani mwanangu

Liliana:(anawasalimia wote)

(Wafanyakazi wote wa nyumba ile kasoro mtunza bustani wanamuitikia)

Mtunza bustani (ndo anafika) shikamoo anti…

Bianca: marahaba (kwa Liliana) naomba nikutambulishe mwanangu…huyu dada wa usafi anaitwa Husna

Husna: karibu…

Bianca: mpishi jina lake ni Siwema

Siwema: karibu sana

Bianca: mtunza bustani ni Mbise

Mbise: karibu sana

Bianca:na mlinzi anaitwa Lupemba

Lupemba: karibu sana

Bianca:(kwa wafanya kazi wake) huyu anaitwa… (anamuangalia Liliana) jitambulishe

Liliana: mimi naitwa Liliana

Siwema: oh…jina zuri

Bianca: kwanzia leo yeye ni mwanangu…nimemuona mtaani muda mrefu sana nikamuonea huruma sana…leo nimemuona sana nikaona nisimuache. nimlete nyumbani yeye sasa ni binti yangu nitamlea ingawa simjui alipotoka…karibu nyumbani Liliana

Liliana:(anatabasamu) asante…

Husna:(anaangalia angalia huku na huku) nguo zake ziko wapi?

Liliana: sina nguo…

Bianca: twende nikakuonyeshe chumba chako upumzike…wakati huo Siwema andaa chakula…nikimaliza kumuonyesha chumba chake aoge, ale kisha apumzike

Siwema: chakula kipo anti…

Bianca: sawa (kwa Liliana) twende ndani…

(Wanaingia ndani nyumba ni ya kifahari kweli kweli na inapendeza sana kila kitu ni cha gharama, Bianca anamchukua Liliana na kwenda nae chumba kimoja kizuri sana)

Bianca: hiki chumba nilipanga kumpa mwanangu na kwakuwa Mungu hajanipa mtoto…basi wewe ndo mmiliki wa chumba hiki…

Liliana:(bado ana wasiwasi) asante

Bianca: niite mama…tafadhali…

Liliana: asante mama

Bianca: usijali…umekipenda?

Liliana: ndio ni kizuri… (anakumbuka alivyokuwa analala stoo) asante mama

Bianca: usijali…basi oga…kisha uje tule Siwema atakuwa anatenga ili tule...

Liliana: sawa…

Bianca:(anafungua mlango wa bafu la kifahari lililopo chumbani humo) oga mwanangu au nikuogeshe

Liliana: nitaoga tu mama ninajua kuoga

Bianca: haya mwanangu…ukimaliza uje upate chakula kisha upumzike kidogo…nimeona una vidonda vingi nitakupeleka hospitali

Liliana: sawa mama

Bianca:(anatoka nje)

Liliana:(anaingia kuoga)

Bianca: asante Mungu nimepata mtoto…Mungu mkubwa sana amenisikia maombi yangu

Husna: anti naomba hela nikanunue hizo nguo maana humu ndani hakuna ngujo za mtoto hata moja

Bianca: sawa na sijui akitoka kuoga atavaa nini (anatoa pesa na kumkabidhi Husna)

Post a Comment

0 Comments