I KILLED MY LOVER 15

 


SCENE 15: -

(Mchana Bianca anafika nyumbani akiwa na daktari wake binafsi anayemtibu pindi anapokuwa anaumwa, baada ya kusalimiana na mlinzi na wafanyakazi wake anaingia ndani na anamkuta Liliana amekaa anaangalia runinga, Liliana sasa ni mtoto mrembo muonekano wake ule wa uchakavu umebadilika na amekuwa ni mtoto mrembo na uso wake una nuru mpya na ya matumaini)

Liliana: shikamoo mama

Bianca:(anatabasamu) safi sana...niite hivyohivyo mama…marahaba mwanangu hujambo?

Liliana:(anaachia tabasamu) sijambo

Bianca: msalimie anko...

Liliana: shikamoo anko…

Daktari: marahaba

Bianca:(anatabasamu) dokta huyu ni mwanangu…Mungu amenipa mara baada ya kumuomba kwa muda mrefu

Daktari: hongera sana umemu adapt au inakuwaje?

Bianca: nimemu adapt…

Daktari: kwahiyo unamjua vizuri…

Bianca: doctor she is my daughter and I love her, anyway nimemuona ana vidonda vingi…mwilini mwake nataka umpe dawa ya kuvikausha na pia mpime magonjwa mengi na kama yanatibika naomba tumtibu nataka aanze maisha upya…anaonekana amepitia mengi…

Daktari: unaonekana humjui vizuri sana

Bianca: nitamjua tu…she is so beautiful na pia anaonekana ni mtulivu anafaa kuwa binti yangu

Daktari: umelilia mtoto sana…  I hope umepata mtoto uliyekuwa unamtaka siku zote….

Bianca: kabisa…

Daktari: ana umri gani?

Bianca: saba…

Daktari: bado mdogo kumbe

Bianca: nataka nimpeleke shule…international school na akitaka kukaa boarding au day ni yeye tu…

Liliana:(anaonyesha kufurahia habari ile) asante mama nataka kusoma

Bianca: utasoma tu mwanangu nitakusomesha katika shule nzuri mpaka wewe mwenyewe utafurahi mwanangu umesikia ee

Liliana: ndio mama(anatabasamu)

Daktari:(anaanza kumpima vipimo mbalimbali) wewe ni mtoto mzuri eeh…usiogope sindano ee (anamchoma sindano na kuchukua damu kwa ajili ya vipimo mbalimbali) good girl … (kwa Bianca) basi sawa nitakuletea majibu baadae mimi ngoja niende…

Bianca: sawa dokta tutawasiliana...

Daktari: poa(anatoka)

Bianca:(kwa Liliana) umekula mama?

Liliana: ndio nimekula…

Bianca: umekula nini?

Liliana: ugali...na nyama

Bianca: unapenda mwanangu?

Liliana: ndio…

Bianca: safi sana mama…yaani naahidi kukutunza vizuri ila tu hujaniambia pale ulikuwa unafanya nini maana nilikupita kama mara mbili nikakuonea huruma sana…

Liliana: mimi ni mtoto yatima mama na baba yangu walikufa kwenye ajali, baada ya kifo chao nikaenda kuishi na mjomba pamoja na mke na watoto wake…shangazi na mjomba walikuwa wananitesa sana, wananifanyisha kazi ngumungumu na kunipiga, sikuenda shule nzuri ingawa ile nyumba na mali zote ni za kwangu

Bianca: maskini mwanangu…enhe embu endelea

Liliana: mjomba akawa ananibaka usiku

Bianca: Mungu wangu…jamani mbona kuna wanadamu wengine hawana huruma?

Liliana: acha tu, nikawa sipati chakula cha kutosha…nalala stoo utasema sio nyumba yangu

Bianca: aisee…kwahiyo ikawaje mpaka ukaishia mitaani?

Liliana: kuna siku shangazi alinipiga sana jamani mpaka nikaona nitakufa ndo nikakimbia na kwenda mitaani

Bianca:(anashusha pumzi) aisee…dah!!!Mungu nae ana mitihani yake lakini usijali kabisa mama hapa umefika hautapata mateso wala nini…Mungu alituumba ili tuhudumiane…mimi mpaka unavyoniona hivi ni mtu mzima ila sina mtoto na wala sina mume…ila hilo la mume wala halikunipa wasiwasi, linalonipa tabu mimi ni kutokuwa na mtoto nina mali nyingi nina mabiashara, nina majumba lakini sina mtoto hata leo nikifa nitamuachia nani

Liliana: ndugu zako...

Bianca: hawapo hapa wapo nchi za nje hukona wana maisha yao na pesa zao unajua sisi wazazi wetu walikuwa na pesa sana wakaturithisha yaani hatuna hata shida...sana

Liliana:(anatabasamu)

Bianca: ndo hivyo kuwa na Amani hapa nitakulea kama mwanangu kabisa na wala hautakuwa na shida yoyote sawa mama?

Liliana: ndio mama…

Bianca:(anaita) Siwema, Husna

(Wanakuja na kusimama mbele ya Bianca na Liliana kwa heshima)

Bianca: Husna naomba unisafishie kile chumba cha midoli nilichokifunga miaka mingi nikiamini ipo siku na mimi Mungu atanisikia na nitakuwa na mtoto wa kucheza kwenye hicho chumba

Husna: sawa anti

Bianca: Siwema nenda ukapike mlo mzuri sana wa jioni nitakaa mezani na mwanangu na kufurahia chakula hicho

Siwema: sawa anti(anaondoka)

Liliana:(anakumbuka maisha yalivyokuwa akiwa na shangazi yake na mjomba wake, jinsi alivyokuwa anakula makombo kama mbwa na alipokuwa analala)

Bianca:(anamshtua)

Liliana:(anashtuka)

 Bianca: unawaza wapi?

Liliana:(anatabasamu)

Bianca: sipendi kukuona unawaza mwanangu…

Liliana: sawa mama…

Bianca: Husna alienda kukununulia nguo za kuanzia kwahiyo nimeona wala sio nzuri sana kesho nitakupeleka dukani ukachague upendavyo sawa ee

Liliana: sawa mama…nitafurahi

Bianca: usijali (anachukua rimoti) mbona huwashi TV mwanangu

Liliana:(anakumbuka alivyokuwa anajaribu kuwasha TV alivyokuwa anapigwa)

Bianca: washa bwana…hii ni TV yako mwanangu…

Liliana: sawa mama, asante mama nashukuru kwa upendo nilikuwa nimekumbuka kupendwa hivi

Bianca:(anatabasamu) usijali nitakupenda kweli (kimya kidogo) unapenda katuni naweza kuweka katuni na kuangalia na wewe hata siku nzima…

Liliana: napenda sana marehemu mama yangu alikuwa ananiwekea sana

Bianca: usiwakumbuke bwana mimi nipo hapa niangalie mimi

Liliana: asante mama

Bianca: usijali (anabadilisha chaneli) sasa katuni sijui zipo namba ngapi

Liliana: hata sijui

Husna: yaani anti ni namba 302

Bianca: kumbee

(Wote wanacheka huku Bianca akiweka katuni ili waangalie pamoja, wanaonekana kufurahi sana maana kuna vicheko vingi sana)

Post a Comment

0 Comments