I KILLED MY LOVER 16

 


SCENE 16

(Liliana na Bianca wanashuka kwenye gari moja matata kwa lugha nyingine gari la kifahari, Liliana amependeza kuliko kawaida na nuru ya uso wake ni ang’avu sana, amenenepa na pia anaonekana ana furaha mno, wanaongozana na kuingia katika duka moja la nguo la kifahari sana)

Bianca:(anafika mapokezi) habari yako…

Dada mapokezi: salama shikamoo

Bianca: marahaba…natafuta nguo nzuri za mtoto wangu hapa

Dada: okay karibu piteni mchague

(Liliana na Bianca wanapita na kuanza kuchagua nguo)

Liliana:(anashangaa shangaa ila anajikuta anawakumbuka wazazi wake)

Bianca:(anamuona) mama ni nini mwanangu pita uangalie nguo unayopenda

Liliana:(anatabasamu) sawa mama…

Bianca: sipendi kukuona unalia wala kuhuzunika…yaache ya nyuma mwanangu…achana na mawazo mimi ni mama yako na ninakuhakikishia kuwa utaishi maisha uliyopangiwa na Mungu…Mungu alikupangia uishi maisha mazuri na ndo maana ukazaliiwa kwa wazazi wenye uwezo ni ndugu tu ndo walikuharibia ila Mungu hakukata tamaa na wewe na ndo maana upo hapa na mimi …nitakulea vizuri maana Mungu hakunipa mtoto wangu mwenyewe ila kanipa mtoto nitakutunza mwanangu mzuri sawa mama ee…

Liliana: ndio mama…

Bianca: ukitoka hapa twende tukale icecream au unaonaje?

Liliana: sawa mama

(Wanaendelea kuchagua nguo)

Bianca:(anapokea simu aliyopigiwa)

(Wakati huo kuna mtu anaingia, anaangaza ghafla anamuona Liliana, anapigwa butwaa)

Mwanamke: Liliana??

Liliana:(anageuka na kumuangalia mwanamke aliyemuita) shikamoo

Mwanamke: marahaba…unanikumbuka?

Liliana: hapana…

Mwanamke: mimi mama Joyce nilikuwa jirani yenu

Liliana:(anajaribu kuvuta picha)

Mwanamke: mara ya mwisho nilikuwa ni mmoja wa watu waliokuja kukuokoa wakati unapigwa na shangazi yako

Liliana: ah…sawa sema sikuwa naangalia

Mwanamke: usijali…yaani umenenepa…umekuwa mzuri kweli yaani

Liliana: asante…dada Anna hajambo?

Mwanamke: hajambo jamani

Mwanamke: uko wapi siku hizi mwanangu jamani mungu mkubwa kweli

Bianca:(anakuja alipo Liliana na yule mwanamke) mama…vipi? uko sawa??(kwa mwanamke) habari yako dada?

Mwanamke: salama dada kwema?

Bianca: kwema (kwa Liliana) vipi…mbona huchagui nguo

Mwanamke:(anamuangalia Bianca kuanzia viatu alivyovaa, mkufu wa dhahabu, pete za dhahabu, simu ya gharama) Duh!!huyu mwanamke anaonekana ana pesa jamani

Bianca: abeee…unaniongelesha?

Mwanamke: hapana dada

Bianca:(anamshika mkono Liliana na kuondoka nae)

Liliana:(anamvuta Bianca nyuma)

Bianca: nini mwanangu

Liliana:(kwa mwanamke) huyu ni mama yangu anaitwa mama Liliana

Bianca:(anafurahi kusikia hivyo)

Mwanamke: mama yako?????!!!!

Liliana: ndio (kwa Bianca) mama, huyu alikuwa jirani yetu nyumbani

Bianca: okay…haina shida mwanangu (anamuangalia mwanamke) nashukuru kukufahamu…upite kwetu ututembelee au unaonaje?

Mwanamke: sawa, ni wapi?

Bianca: uzunguni…

Mwanamke: wow…

(Liliana na Bianca wanaendelea kuchagua nguo)

Liliana:(anapata nguo na kujaribisha)

Mwanamke:(anabaki mdomo wazi) njia za Mungu hazichunguziki…leo nimemuona Mungu na anapendeza jamani yaani sijamuona Liliana nimemuona Mungu kupitia Liliana, mtoto aliyekuwa analala stoo, anakula makombo nyumbani kwao, aliyekuwa anafagia uwanja wote peke yake leo anang’aa hivi…jina la bwana lihimidiwe…ninakusifu wewe Mungu wa Ibrahim, Isaka na Yakobo, Mungu wa Mussa, Mungu wa Eliya ama hakika wewe ni mtu wan ne katika maisha yetu…nitaenda kumsimulia shangazi yake Liliana matendo makuu ya mungu

Bianca:(anageuka kumuangalia yule mwanamke anagundua kuwa bado anawaangalia sana) child, huyo mama ana shida gani kwani

Liliana: hana shida mama

Bianca: mbona haachi kutuangalia…asije akawa jambazi bure

Liliana: hapana mama yeye sio jambazi ni mtu mzuri tu

Bianca: okay

Mwanamke:(anaamua kuendelea na kazi zake zilizomleta hapo)

Liliana:(anatabasamu kuona nguo nyingi na nzuri) mama zote zangu

Mwanamke:(amesimama pembeni yao anatabasamu)

Bianca:(anapata wasiwasi) mwanangu huyu mama isije ikawa katumwa na shangazi yako aje akuharibie Amani yako

Liliana: mama usijali jamani

Bianca: haya mwanangu…mimi nakusikiliza wewe

Mwanamke:(anafika alipo Liliana) mwanangu ilikuwaje mpaka ukafika hapa?

Bianca:(anadakia) wewe dada kwani vipi nimekuona muda mrefu sana unamfuatilia mwanangu tatizo nini?

Mwanamke: sio ugomvi…mimi nimeokoka na ninampenda Yesu sina cha kukutishia mdogo wangu kuwa na Amani

Bianca:(anatulia)

Liliana: nilikuwa natembea mtaani ndo nikakutana na mama yangu

Mwanamke: usisahau kumtolea Mungu sadaka…nawakaribisha kanisani siku moja mje mjumuike nasi

Bianca: tutakuja (anamshika mkono Liliana na kuondoka)

Liliana: mama, wala sio mtu mbaya,

Bianca: we huyaoni macho yake…jamani Mungu amenipa mtoto kwa njia zake za pekee halafu nimuachie mtu aje akuchukue ghafla tu?

Liliana: hakuna atakayekuja kunichukua mama mimi nipo na wewe mpaka mwisho wa dunia

Bianca:(anacheka) wewe mwisho wa dunia unaujua?

Liliana:ee

(Wanacheka kisha wanatoa mizigo yao nje na kulipa kisha wanaondoka)

Mwanamke: nitamsimulia kila mtu matendo makuu ya Mungu…haleluya…ee mungu ulisikia kilio cha huyu mtoto muda mrefu, umempa kicheko, umemfuta dhiki na kilio, unastahili sifa na utukufu

(Bianca anawasha gari kisha wanaondoka huku Liliana anaendelea kuonyesha furaha isiyo na kifani)

Liliana: mama asante sana

Bianca: usijali mwanangu

(yule mwanamke nae anamaliza kuchagua nguo analipa kisha anaondoka zake huku akiendelea kumsifu Mungu, watu wanamshangaa yeye wala hajali)

Mwanamke: Mungu anaishi jamani

Post a Comment

0 Comments