I KILLED MY LOVER 17

 

SCENE 17:

(asubuhi na mapema siku moja baada ya yule mwanamke kumuona Liliana, anafika nyumbani kwa shangazi na mjomba wa Liliana)

Mwanamke:(anagonga mlango) hodi jamani?

Anna:(anafungua mlango) karibu (kwa heshima) shikamoo

Mwanamke: marahaba mama hujambo?

Anna: sijambo

Mwanamke: mama yako yuko wapi?

Anna: ndani… (anaufungua mlango kumruhusu kuingia ndani)

Mwanamke:(anaingia ndani anakuta sebule iko wazi anashangaa sana) jamani samahani kwa kuingilia mambo yenu kwani nini tatizo? mbona sebuleni hakuna kitu?

Anna: vitu vilianza kuuzwa kimoja baada ya kingine

Mwanamke: Kisa?

Anna: madeni mama kwenye vicoba

Mwanamke: aisee?

Anna: ndio…sasa sijui utakaa wapi maana hatuna hata kiti, labda nikuletee kigoda

Mwanamke: niletee mwanangu

Anna:(anaelekea jikoni na baada ya muda anarudi akiwa na kigoda anampa yule mwanamke kisha yeye anakaa chini)

Mwanamke: sasa na wewe mbona shule huendi?

Anna:(anaguna) yaani tangu Liliana ameondoka hapa kaondoka na kila kitu hela ya kula tu hapa ni matatizo…tu

Mwanamke: aisee? na baba yako?

Anna: yupo tu

Mwanamke: aisee

(Shangazi anatokea chumbani kwake)

Shangazi: vipi na wewe asubuhi yote hii kwa watu unataka nini?

Anna: mama?

Mwanamke: pole kwa matatizo

Shangazi:(kwa jazba) matatizo gani?

Mwanamke: ya kuuza kila kitu cha ndani

Shangazi: (anachukia sana) hayakuhusu

Anna: mama…

Shangazi:(kwa Anna) na wewe…nini? embu toka nenda zako huko sitaki hata kukuona

Mwanamke: yaani una gubu kama mama mkwe, yaani Yesu anisaidie nisikujibu vibaya Zaidi…hata hivyo sikuja kukuona nimekuja tu kutangaza ushindi

Shangazi: wa nani na sisi unatuhusu nini huo ushindi?

Mwanamke: unawahusu maana unamhusu Liliana

Anna: kafanyaje binamu yangu?

Mwanamke: kawa mzuri jamani…ana maisha mazuri

Bella:(anaingilia maongezi akitokea jikoni) kivipi

Mwanamke: njia za Mungu hazichunguziki…nachojua tu sasa ni mtu ambae ni tajiri kwa kweli mrembo ana furaha

Anna: maskini binamu yangu…

Shangazi:(anabaki ameganda tu kama sanamu)

Mwanamke: ndo hivyo

Anna: ama kweli malipo ni hapa hapa duniani, alikosa hata maji ya kunywa hata kama alikuwa ndani ya nyumba ya wazazi wake leo hii sis indo tunakosa mpaka maji ya kwendea chooni tunaomba au tunanunua maji ya mia tano duh!!

Shangazi: anapatikana wapi?

Anna: ili ukamuharibie Amani yake?

Shangazi: namuulizia tu…

Mwanamke: kwa kuibia nimempiga picha… (anawaonyesha picha ya Liliana)

(Wote wanabaki midomo wazi)

Bella: aisee

Anna: huyo ndo binamu yangu Liliana

Mwanamke:(kwa Anna) halafu alikuulizia

Bella: mimi ee’

Mwanamke: hapana alimuulizia Anna

Anna: maskini kumbe bado ananikumbuka, kwahiyo hamukuongea maneno mengi

Mwanamke: hapana mama yake mkali huyo tena anaweza hata akakupiga anampenda sana Liliana

Anna: jamani…

Mwanamke: ndo hivyo

Bella:(anaguna) mimi nampenda binamu yangu Liliana

Mwanamke: mara baada ya kumuona kawa mzuri?

Anna:(anacheka sana) kweli anayepanga riziki ni Mungu…na kama amepanga kuwa utaishi vizuri utaishi vizuri tu…binamu yangu alizaliwa katika utajiri hivi vyote vilikuwa vyao lakini mama na baba wakafanya wanayoyajua akaishi vibaya sana na nina uhakika alitamani hata kufa, ila Mungu akamwambia usilie mwanangu mimi ni baba wa yatima nitakuvusha

Mwanamke: oh, haleluya jina la bwana lihimidiwe

Shangazi:(amekasirika kupita kiasi)

Anna: sasa anaishi vizuri akiwa na mama ambae

Mwanamke:(anadakia) si mama yake ila anamlea kama mwanae

Anna: We Mungu

Shangazi:si umwambie na mimi anitendee kama alivyofanya kwa huyo Liliana

Mwanamke:(anacheka sana) nimecheka si kwa kukudharau ila nimecheka Kukuonyesha kuwa Mungu hadhihakiwi mama…tubu dhambi zako atakusamehe yeye ni mwingi wa rehema na fadhili zake ni za milele

Shangazi: hayo mahubiri yako peleka huko…mimi uniache na wanangu

Mwanamke:(anasikitika) kwani kuna mtu kakushika wewe na wanao? tunakushauri tu

Shangazi: hatutaki ushauri wako unaweza kwenda tu na wala sitaki kukuona unanitia kiwingu tu halafu huwa sikupendi kweli yaani lione na sura lake lilivyo baya

Mwanamke: maskini mama Anna

Shangazi: toka hapa muone kazi kufuatilia mambo ya watu

Mwanamke: najua unaugua moyoni kwa habari niliyokuletea ya Liliana pole…ona watoto wako hawaendi shule kama Liliana alivyokuwa haendi shule, dunia duara unachomtendea mwenzio siku moja itakurudia iwe nzuri au mbaya

Shangazi: nimekuambia ondoka zako bwana usiniletee kiwingu hapa

Mwanamke: naondoka mpenzi (anaondoka zake)

Shangazi: huyu mwanamke mjinga sana anakuja kuleta umbea hapa yaani ndo maana watanzania hata hatuendelei maana kila wakati badala ya kufanya yanayotuhusu tunakalia yasiyo wahusu

Anna: umeumia sana kusikia habari za Liliana? ulidhani atakufa? uliposema tusimtafute ulijua kabisa kuwa lazima atakufa huku kwa njaa

Shangazi:na wewe usiniletee habari zako hapa kwanza nina mawazo mengi mume wangu sijui anaumwa nini jamani yaani anaumwa na nyie hamuendi shule maisha yamekuwa magumu kitu tulichonacho hapa ni nyumba tu hatuna vitanda, masofa wala vyombo sina biashara ya aina yoyote, maisha yamekuwa magumu…Leo hii wanangu mnauza karanga na matunda barabarani huku mliishi maisha mazuri

Anna: Maisha mazuri yamerudi kwa mwenyewe

Post a Comment

0 Comments