I KILLED MY LOVER 18

 


SCENE 18: -

(Ni asubuhi ya siku nyingine siku kadhaa zimepita tangu familia ya shangazi na mjomba wake Liliana kujua kuwa kuhusu maisha mapya ya Liliana, Anna yupo barabarani amebeba deli la vitumbua anauza,anapita gari moja baada ya lingine akinadi biashara yake,kuna watu wananunua na kuna wengine hawanunui wanamuacha apite aende zake kwa upande wa pili yake na Bella mdogo wake Anna nae anauza vitumbua na kama ilivyo dada yake nae ananadi bidhaa yake,watu wananunua na wengine hawanunui wanamuacha aende zake)

Bella: baba, vitumbua

Baba :( anapita anampuuzia)

(Upande wa Anna yeye anaendelea kuuza vitumbua kwa kasi, wakati anaendelea kuuza vitumbua anamuona Liliana kwa mbali)

Anna:(anashangaa) Hee!!! Liliana?

(Bianca anaendelea kuendesha gari akimpita Anna)

Anna: Lilly…Lily

Liliana:(anasikia ile sauti ingawa kwa mbali sana)

Anna:(anazidi kuita na Zaidi anaona akimbilie gari) Liliana

Liliana:(anaisikia sauti kwa uhakika Zaidi) mama kuna mtu ananiita

Bianca: nani tena?

Liliana: sijui ila kama sauti naijua

Bianca:(anatafuta sehemu nzuri ya kuegesha gari) embu ngoja niegeshe gari hapa…(anaegesha)

(Bianca na Liliana wanashuka kutoka kwenye gari la kifahari na kumuangalia huyo mtu aliyekuwa anamuita kama kweli ni anna au lah)

Anna:(analifikia gari kwa kukimbia) Liliana

Liliana:(anamshangaa binamu yake huyo alivyo) Anna?

Anna: Liliana (anajikuta Analia sana)

Liliana:(akiwa ndani ya sare za shule mpya anamkimbilia binamu yake huyo na kumkumbatia)

Anna:(anamkumbatia pia huku Analia sana)

Liliana: nini kimetokea?

Bianca:(amesimama pembeni yao anawaangalia wanavyopokeana)

Liliana: pole usilie dada…

Anna: acha tu…ulipoondoka tu ikawa kama vile umeondoka na kila kitu chako Liliana

Liliana: kwanini?

Bianca: watoto

Anna:(anamsalimia) shikamoo

Bianca: marahaba mtoto mzuri hujambo?

Anna: sijambo…

(Wakati huo na Bella nae anakuja mahali walipo)

Bella:(anamshangaa Liliana) Lily???

Liliana:(bila kinyongo anamkumbatia)

Bella: unaenda shule?

Bianca:(anaonekana ana shauku ya kujua wale ni kina nani)

Liliana: ndio naenda kuanza leo

Bella: umependeza (kwa Bianca) shikamoo

Bianca: marahaba… (kwa watoto wote) mi naona tutoke hapa maana ni barabarani sana

Liliana: sijakutambulisha

Bianca: tupande gari mwanangu tutatambulishana kwenye gari

(Wanapanda kwenye gari na haraka Bianca analiondoa gari hilo)

Bianca: enhe!!nambieni

Liliana: hawa ni binamu zangu, (anamshika Anna) huyu anaitwa Anna…ni dada yangu na huyu (anamshika Bella) anaitwa Bella hawa ni watoto wa shangazi na mjomba wangu

Bianca: wale uliokuwa unakaa nao?

Liliana: ndio…

Bianca: okay (anageuka nyuma kuwaangalia maana wamekaa kwenye siti za nyuma) sasa imekuwaje wanauza vitumbua barabarani?

Anna:ni umaskini umetuvaa ghafla…

Bianca: poleni...kivipi sasa?

Anna: mama ana mikopo mingi sana sehemu mbalimbali alikuwa anachukua mikopo kisha anafanyia starehe yeye na baba sasa kila kitu kinaondoka kilichobaki ni nyumba tu na wala sijui kama nyumba nayo itasalimika maana ana madeni mengi sana

Bianca: pole sana…

Bella:(anamshangaa sana Liliana)

Anna: hatuna kitu sasa tunaishi kwa kuunga unga kama hivi

Bianca: aisee poleni sana ila kuna jambo mmejifunza?

Anna: ndio yapo mengi mama

Bianca:vizuri..kwamba kila tunachokifanya kiwe kibaya au kizuri kitakurudia tu, ukitenda mazuri yatakurudia mazuri na mpaka utafurahi mwenyewe lakini ukitenda mabaya,utavuna mabaya na mpaka utajuta kwanini uliyatenda yale…Mungu hutupa jinsi na kadiri ya matendo yetu mema au mabaya,yeye ndo hakimu mkuu na wa haki anatoa hukumu kwa haki na bila upendeleo utadanganya wote ila sio Mungu utatoa hongo unavyoweza ila kwa Mungu utachemsha mwenyewe kwahiyo utavuna  jinsi ulivyopanda kama umepanda mahindi utavuna mahindi na sio mbogamboga kwahiyo tujitahidi sana kutenda yaliyo mema

Anna:ni kweli mama yangu

Bianca: mama yenu na baba yenu walifanya mambo wakidhani Mungu haoni, au walidhani kwa kuwa haonekani basi haoni na wala hasikii…Mungu ni muumba dunia na kila kitu hapa duniani ni mali yake na ni yeye anayetawala kila mtu na kila kitu yupo kila sehemu na kwa kila mtu anaangalia kila kitu tunachofanya na ndo maana mwisho wa siku akitoa majibu tunabaki tunashangaa

Bella:(anasikiliza kwa umakini na anajikuta anahuzunika)

Bianca: ila msijali…mimi na Liliana tutakuja kuwatembelea na Mungu akiruhusu tutawasaidia kidogo tutakachokuwa nacho

Anna: tutashukuru sana mama

Bianca:(anatoa noti za shilingi elfu kumi kama tano hivi) hii hapa elfu hamsini itawasaidia siku mbili tatu wakati tunajiandaa kuja kuwatembelea (anawapa pesa)

Anna:(anapokea kwa mikono miwili) asante mama

Liliana:(anawaangalia kisha anawachekea)

Bianca: msijali…anyways naenda kumpeleka Liliana shuleni, tutaonana

Anna: asante mama(anashuka)Bella tushuke…

Bella:(anashuka huku anataka kulia akimuangalia Liliana)

Bianca: nyumbani wapi? embu ngoja niwape nauli (anatoa elfu kumi na tano) haya kamsalimieni mama

Anna: haya asante mama(wanaondoka)

Bianca:(kwa Liliana) haya mwanangu twende shule eeh

Liliana: sawa mama

Bianca:(analiondoa gari kuelekea shule)

(Anna na Bella wanabaki wanaliangalia lile gari mpaka linapotokomea)

Post a Comment

0 Comments