I KILLED MY LOVER 19

 


SCENE 19: -

(Anna na mdogo wake wanarudi nyumbani wakionekana wana furaha sana, wanarudi na madeli yakiwa bado na vitumbua)

Shangazi: nyie mbona mmerudi na madeli yana vitumbua? au biashara ni mbaya leo? (amekaa barazani nay eye anauza vitumbua na vinaonekana havijaguswa) mi mwenyewe leo watu hawajavigusa toka asubuhi yaani bora jana walikuja kuniunga kidogo ila leo hamna kabisa

Bella: mama leo tumemuona Liliana

Shangazi:(anashtuka) eti kawa mzuri kama yule mmbea alivyokuwa anasema

Anna: ndio….na zaidi anatembea kwenye gari na anaenda shule nzuri sio kama alivyokuwa hapa kwakweli

Shangazi: anha!!! Basi bora yake…

Bella: yaani nikikumbuka alivyokuwa anaenda shuleni na sketi imechanika leo anaenda shule ndani ya gari

Shangazi :( anaguna)

Anna: yaani Mungu amemuokoa sana jamani

Shangazi: basi sawa…kama amefanikiwa ni vyema

Anna:(anaingia ndani kuweka deli kisha anarudi)

Shangazi:(anajisemea moyoni) imekuwaje?

Anna:(anarudi kutoka ndani)

Shangazi: ila mbona kama mna furaha sana

Anna: mimi nimefurahi maana nimemuona binamu yangu niliyedhani amekufa siku nyingi leo nimemuona tena akiwa na afya nzuri na mwenye furaha

Shangazi: sawa kama ni hivyo sawa (anaonekana ana kinyongo sana)

Anna: ametupa hela

Shangazi: nani amewapa?

Anna: huyo mama anayemlea Liliana

Shangazi: wametoa wapi

Bella: we mama yaani wana hela kweli yaani…lile gari tu ni la kifahari sio mchezo

Shangazi: kumbe

Bella: ndio hivyo mama

Anna :( anatoa elfu kumi tano na kumpa mama yake)

Shangazi: yote hii? (anaichukua)hapa nikalipe kwenye kikundi

Anna:(anampokonya) ukalipe kwenye kikundi kwanini? huku ndani hakuna chakula na baba anaumwa na kila kitu hakipo sawa hapa...unalipaje sasa huku kuna vitu vingi vya kufanya

Shangazi: mimi ndo mama mwenye nyumba hii…usinijibu

Anna: mama hali yetu ni mbaya na ni wewe ndo umesababisha maisha yetu yamekuwa hivi yaani mama…halafu sasa hivi tunapata hela ya chakula unataka kupeleka kwenye kikundi

Shangazi: unataka tuendelee kudaiwa? unataka hii nyumba iende?

Anna: sasa mama kwa hii elfu hamsini utalipa nini ili nyumba isiende?

Shangazi: nimekuambia kuwa nitaipeleke kwenye kikundi

Bella: mama hatuna chakula

Shangazi: mtashindia hivyo vitumbua, na kesho tena mtaenda kujianika hapo ili huyo binamu yenu awaone tena awape tena hela

Anna: mama wewe upoje mama, mbona una roho ya ajabu hivyo?

Shangazi:(anamzaba kofi) pumbavu naona unataka kunitawala wewe mtoto

Mjomba:(anaonekana amesimama mahali hapo muda mrefu sana na ameshuhudia yote) Anna anasema ukweli (anaonekana amekonda sana) ni kweli kabisa kwanini una roho mbaya hivyo?

Shangazi:na wewe kelele kazi tu kula na kulala sasa hivi mpaka wanao wanakushinda kutafuta hela, umekaa ndani kama mzoga halafu mwisho wa siku unajifanya wewe ndo kila kitu na kibaya Zaidi unajifanya wewe ndo unajua nani ana roho nzuri na nani ana roho mbaya

Mjomba: mimi ni mume wako na baba wa watoto wako

Shangazi: umeshapoteza hiyo hadhi ya kuwa baba wa watoto wangu…na mume wangu wewe ni mwanaume suruali

Mjomba: mama Anna...hayo ni maneno gani…unaongea tena mbele ya watoto

Anna na Bella:(wanaangaliana)

Shangazi: nitaongea navyotaka baba na wewe hutakuwa na chochote Zaidi ya kukaa kimya na kufuata nachotaka mimi

Mjomba:(anacheka sana)

Shangazi: unacheka nini? unanidharau sio

Mjomba: ndio…nakucheka na kukudharau hela sio yako ila unaitolea matumizi zinakutosha kweli wewe

Shangazi: nimekuambia kuwa nyamaza na sitaki kusikia sauti yako

Mjomba: dhambi zinakutafuna mama Anna na bado zitakutafuna sana mpaka utajuta

Shangazi: wewe mwenyewe dhambi zinakutafuna…unaumwa magonjwa ambayo hata hayeleweki tumekupima mpaka UKIMWI hauna sasa utakuwa ni nini?

Mjomba: mimi natafunwa na dhambi ila sio kama wewe mwenzangu

 Shangazi: nimefanyaje?

Mjomba: watu hata hawakutaki, unauza vitumbua vinang’ong’wa na nzi hapa mpaka unaona uviingize ndani viliwe na watoto

Shangazi:(anakasirika sana) nakuchukia wewe baba kuliko chochote

Mjomba: sijali…mimi nimebaki tu kufa na kulipa dhambi nilizowahi kutenda

Anna: baba usiseme hivyo

Mjomba: hapana mwanangu nasema ukweli kabisa na wala sina nachoficha mwanangu nimetenda dhambi nyingi na nyingine ni mbaya mpaka nashindwa kuzitaja

Anna: Mungu amekusamehe baba…kwakuwa umezijua dhambi zako na kuzikiri

Mjomba: mwanangu

Shangazi: eti Mungu kamsamehe (anacheka sana)

(Mjomba, anna na Bella wanaangaliana)

Shangazi: mtaangaliana sana lakini hiyo pesa ni ya kupeleka kwenye kikundi

Mjomba: unashangaza sana mama Anna yaani hela ya watu wewe unaibeba utasema umeitafuta wewe

Shangazi: huyo Liliana aliwahi kuwa chini yangu kwanza hii hamsini haitoshi kwa malipo ya kumlea

Mjomba:(anacheka tena) embu niacheni mimi

Anna:(anacheka pia)

Mjomba: eti kumlea kwanza nani amekuambia Liliana kakupa hiyo elfu hamsini kama malipo eti ya kumlea?

Shangazi: ndio si alikuwa anaishi nyumbani kwangu

Mjomba:(kwa mshangao kidogo) nyumbani kwako?

(Anna na bella wanacheka sana)

Shangazi: mnanicheka

Mjomba: unachekesha

Shangazi:(anaingia ndani kwa hasira)

Mjomba: kwahiyo kachukua hela?

Anna: ndio

Mjomba: muacheni, tutapata tu nyingine

(wanabaki wanamshangaa mama yao kwa kitendo hicho cha kuchukua pesa kwa nguvu)

Mjomba: mke wangu anachanganyikiwa taratibu jamani

Anna: yaani acha baba

Mjomba: alivyo anaweza kumfanyia kitu kibaya Liliana… (anabaki anasikitika)

Post a Comment

0 Comments