I KILLED MY LOVER 20

 


SCENE 20: -

(Asubuhi na mapema sana ndo kwanza ndo panapambazuka, Liliana na Bianca wanafika katika nyumba wanaoishi shangazi na mjomba wake Liliana)

Liliana:(anagonga mlango)

Bianca:(amesimama anaangalia mazingira yale)

Anna:(anafungua mlango)

Liliana: Da. Anna

Anna: Lily?

Liliana: ndo mimi

Bianca:(anatabasamu)

Anna: mbona mapema?

Liliana: mimi naenda shule…ndo nimepita kumuonyesha mama nilipokuwa naishi

Anna:(anafungua mlango) karibuni… (kwa Bianca) shikamoo

Bianca: marahaba

Liliana:(kwa Bianca) mama...hapa ndo nilipokuwa naishi

Anna:na ndo nyumba yake

Liliana: hapana nimeiacha tu

Bianca: ana nyumba nyingine (anamuangalia Liliana kisha anatabasamu)

Anna: jamani karibuni

(Liliana na Bianca wanaingia ndani)

Liliana:(anashangaa mazingira yalivyo) mbona hakuna makochi?

Anna: michezo ya mama

Bianca:(anashangaa) alikuwa anadaiwa au?

Anna: ndio

Bianca: makubwa…

Anna: karibuni mkae tu chini

(Bianca na Liliana wanakaa)

Anna: ngoja nikawaamshe baba na mama

Liliana: sawa

Bianca:(anabaki anayashangaa mazingira yale) sasa wanaishije?

Liliana:(anabaki anaguna) sijui

(Shangazi na mjomba wanakuja wakitokea chumbani kwao)

Mjomba: Liliana?

Liliana: shikamoo mjomba

Shangazi:(anamshangaa Liliana jinsi alivyo) wewe ni Liliana?

Bianca:(anatikisa kichwa)

Mjomba: marahaba Liliana mwanangu naomba unisamehe sana…mwanangu nipo chini ya miguu yako mama naomba unisamehe kwa kila kitu nilichowahi kukufanyia mwanangu kuna mengi sana nimekukosea

Shangazi:(kwa kejeli) amekusalimia tu hajakuambia uanze kujielezea wewe baba vipi?

Bianca: sidhani kama amekosea

Shangazi:(anabenjua midomo) semeni shida yenu

Liliana: shangazi…

Shangazi:(kwa jazba)

Bianca: wewe dada vipi kwani? si amekuita tu…yaani una roho mbaya wewe… (kwa Liliana) naona hawataki kukusikiliza mwanangu tuondoke

Mjomba:(kwa Bianca) hapana dada…tulia tu, bwana usiwe na jazba mpendwa wangu…karibu sisi tunakusikiliza yeye kama hatakusikiliza ni kimpango wake

Bianca:(anamuangalia shangazi kwa hasira sana) yaani hata sidhani kama wanao unaishi nao vizuri

Shangzi:(anamuangalia Bianca kwa hasira sana)

Bianca: huyu mama vipi? yaani mtoto umemlea kwa mateso pamoja ya kuwa mali zote zilikuwa ni zake, leo kaja kukusalimia unaanza kuleta ujeuri (kwa Liliana) twende mwanangu

Anna:(kwa Bianca) jamani shangazi sisi, (anaonyeshea yeye, baba yake pamoja na Bella) tunakusikiliza

Bianca:(anashusha pumzi) sawa

Shangazi:(amebaki amevuta mdomo)

Bianca: kwanza tumepita kuwasidia kitu Fulani…tulipokutana na nyie siku ile tukaona tuwasaidie kiroho safi tu lakini

Mjomba: sawa…

Bianca: mimi Liliana ni mwanangu sasa hivi ni zawadi kutoka kwa Mungu, maana sikubarikiwa mtoto, ila mungu akaona anipe mtoto kwa njia zake anazozijua mwenyewe

Mjomba: sawa kabisa

Bianca: Zaidi ya Mungu kunipa mtoto Mungu amenipa ndugu ambao ni nyinyi

Anna:(anatabasamu)

Bianca: tumekaa na Liliana tumeona tu tujumuike pamoja tusaidiane

Mjomba: sawa ndugu yangu ni wazo zuri sana

Bianca: asante

Mjomba: nasi tutaupokea huo msaada wako na tutaubariki sana

Bianca: asante

(Kimya kinapita kama watu wote kuna kitu wanatafakari)

Bianca: sawa…kwahiyo tuanze changamoto zenu ni zipi?

Anna: shule…na chakula, na baba anaumwa

Bianca:(kwa mjomba) unaumwa nini kaka?

Mjomba: acha tu dada naona ni malipo yangu ya mabaya niliyowahi kufanya

Shangazi: umeulizwa unaumwa nini sio kujielezea

Bianca: yupo sawa kujielezea pia

Mjomba: naumwa figo...limekufa

Bianca: pole sana…. utapona tu…tutalishughulikia utapona tu (kwa watoto) na nyie

Anna: shule na chakula

bianca: mtapata… (kwa shangazi) na wewe

Mjomba :(anadakia) madeni yeye ndo chanzo cha matatizo yetu

Bianca: okay nitakulipia na pia nitakuomba uje ufanye kazi katika moja ya godown yangu, mimi ni mfanyabiashara wa mchele nina kampuni na nina wafanyakazi wananifanyia kazi hapo

Mjomba: asante sana mpaka kazi utatupa?

Bianca: ndio kaka, hata wewe ukipona nitakupa kazi pia

Mjomba: asante sana

Bianca: msijali (huku ananyanyuka) Liliana anachelewa shuleni tutapita tena

Mjomba: asante sana

(Bianca na Liliana wanatoka nje wakisindikizwa na Anna pamoja na Bella)

Anna: haya karibuni tena

Bianca: asante…mbaki salama jamani

Bella: haya

(Wanaondoka)

Mjomba:(anaguna) Mungu asante sana…ubarikiwe sana

(Shangazi anarudi kulala bila kusema kitu, Anna na Bella nao wanarudi chumbani kwao,mjomba anabaki peke yake sebuleni)

Post a Comment

0 Comments