I KILLED MY LOVER 21

 


SCENE 21: -

(Jioni ya siku nyingine tena, siku kadhaa baada ya Bianca na Liliana kwenda kuwatembelea familia ya mjomba wake Liliana, gari kubwa la Bianca linaingia katika jumba lake safi na kifahari)

Bianca :( huku analiegesha pembeni ya magari yake mengine) jamani karibuni

Anna: wow…jamani bonge la jumba…

Liliana :( anatabasamu) karibuni…

Bella: Asante…yaani Lily kwenu pazuri kweli yaani

Liliana: Asante… (kwa mjomba na shangazi yake) karibuni

Mjomba: Asante Sana mwanangu

Shangazi :( anabenjua midomo na anaonekana hajafurahi hata kidogo)

Bianca: karibuni ndani(anawaongoza)

(Jumba ni la kifahari sio mchezo na kila kitu kinaonekana ni cha thamani sana)

Bianca:(anaita) Siwema

Siwema:(anakuja anakimbia) abee anti…

Bianca: nina wageni andaa chakula tutakula nao leo...wakati huo naomba uwaletee vinywaji (kwa wageni) karibuni jamani (kwa watoto) jisikieni nyumbani

Anna na Bella: asante

Bianca:(kwa Liliana) waonyeshe wenzio mazingira

Shangazi:(anajisemea moyoni) unajishaua umesikia wanangu wanataka kuona nyumba yako mbaya hii(anafyonza)

Bianca:(anasikia) vipi mbona unafyonza

Shangazi: wala…

(Watoto wanaondoka na kwenda nje)

Mjomba: hongera kwa nyumba nzuri dada

Bianca: asante sana kaka yangu

Siwema:(anakuja na vinywaji na kuvitenga mezani) he!!watoto wako wapi?

Bianca: wanacheza nje huko

Siwema: ngoja niwaite waje wanywe juisi

Bianca: waache tu wacheze watakunywa tu

Siwema: sawa(anaondoka)

Mjomba:(anachukua glasi ya juisi kisha anakunywa kidogo)

Bianca:(nae anachukua juisi na kuanza kunywa)

Mjomba:(anavuta pumzi ndefu sana) ah…dada kwa niaba yangu na familia yangu napenda kukushukuru sana kwa yote uliyotufanyia…hatuna cha kukulipa Zaidi ya kukushukuru sana, umelipa madeni ya mke wangu yote, umewaandikisha wanangu shule yaani kwakweli umeturudisha tunakushukuru sana

Bianca: usijali kaka yangu naomba mmshukuru sana Liliana alinisimulia stori yenu kisha akaniomba niwasaidieni kwa kidogo nilichojaaliwa

Mjomba: sio kidogo hiki ni Zaidi ya kikubwa…tena mwezi ujao naenda india kutibiwa na hii ni wewe ndo unawezesha na nikirudi umesema utanipa kazi kwenye moja ya viwanda vyako

Bianca: ndio na sio wewe na mkeo pia (anamuangalia shangazi) kama akitaka

Mjomba: atataka tu maana ameonja joto ya jiwe na ameona mziki wake

(Bianca na mjomba wanacheka)

Shangazi:(anachukua kinywaji na kuanza kunywa)

Bianca: kwahiyo bwana ni hivyo tunatakiwa tuhudumiane vyema hii ni kusudi la Mungu, ukijaaliwa kidogo basi wasaidie na wenzio Mungu atakubariki sana n asana

Mjomba: ndo maana Mungu anakubariki sana dada…ona ulivyojenga himaya

Shangazi: amejenga au amehongwa tu…mwanamke utawezaje kujenga hivi

Bianca:(anacheka kidogo) una mawazo madogo sana nan do maana hata vikundi vya vicoba walikupokonya kila kitu… (anacheka tena) ila ni kweli kitu kama nilihongwa eeh lakini hata ukihongwa kama huna akilia ya kuvilinda vitapotea tu…kama wewe uliachiwa jumba kubwa ila si ilikuwa nusu ulipoteze? kwa lile jumba ulilikjenga kwa nguvu zako?

Shangazi:(anamuangalia kwa hasira sana)

Bianca: nijibu ulilijenga wewe kwa nguvu zako? si ulipewa, ndivyo hata mimi niliolewa na mwanamume tajiri sana, alinipa kila kitu nikaishi vizuri sana ila aliniacha na kwenda kwa mwanamke mwingine na hakutaka kuchukua hata kiwanja kimoja alichoninunulia hapo sasa sikutaka kuzubaa nilifanya kazi kama mtumwa usiku na mchana ili nitimize malengo yangu na ndo maana unaniona nina vitu vyangu…ndio nilihongwa ila pia nilipambana kuvitunza

Mjomba: safi sana dada wanawake wanatakiwa waige mfano wako wewe ni jasiri sana (anakaa kimya kidogo) kwanini mumeo alikuacha?

Bianca: sio yeye tu…wengi tu…

Mjomba: kisa?

Shangazi: mkorofi

Bianca:(anacheka kidogo) hapana kisa tu sikuwa na uwezo wa kuzaa, sikuwazalia mtoto hata mmoja, sina mtoto ila Mungu akanisaidia nikampata Liliana

Mjomba: Liliana Baraka hiyo…tulimnyanyasa kwa muda mrefu sana ila badala atuchukie akatusaidia kwenye dhiki zetu

Bianca: hicho ndo kitu kinachonifanya nimpende Zaidi huyu mtoto

Shangazi:(anafyonza tena)

Bianca:(kwa shangazi) mbona wewe una roho ya kichawi au mchawi wewe mama

Mjomba: msamehe tu dada hajui alitendalo

Bianca: mkeo akiwa na hii tabia hakuna atakayeweza kumsaidia na anatakiwa atambue kuwa msaada anaopata ni kwa ajili ya Liliana isingekuwa Liliana nisingemsaidia

Mjomba: asante sana, na naomba umsamehe mke wangu

Shangazi:(kwa mumewe) unajifanya mtu mzuri…huku wewe ndo shetani kunizidi mimi

Bianca: kivipi tena jamani

Shangazi: aliua dada na shemeji yake…huyu ni katili kuliko hata mimi

Mjomba: mama Anna, nimeshatubu na nimeshaadhibiwa sana tu unatakaje kwani?

Shangazi: dunia nzima ijue kuwa wewe ni katili kuliko mimi

Mjomba: kwahiyo kumbe ni hivyo?

Shangazi: ndio ni hivyo

Mjomba: mashindano kwamba nani Zaidi si ndio?

Shangazi: ndio

Bianca:(anasikitika sana) aisee kaka unaishije na huyu mwanamke jamani?

Mjomba: acha tu

Bianca: anyway, hayo mwengine tutaongea siku nyingine kwa leo tuenjoi tu

Mjomba: kwakweli dada

Siwema:(anaandaa meza kwa ajili ya kutenga chakula)

(Giza linaingia)

Bianca: inamaana tumeongea sana jamani?

Mjomba: giza nalo limeingia

Bianca: msijali kuna vyumba vya kutosha humu mtalala tu

Mjomba: sawa dada yangu

Siwema:(anawaita watoto) njooni mnawe mikono chakula tayari (anawageukiwa wakubwa) karibuni mezani chakula tayari

Bianca: asante (kwa mjomba na shangazi) karibuni chakula(anawaongoza)

(Watoto, shangazi, mjomba pamoja na Bianca wanaelekea mezani kwa ajili ya chakula cha jioni, wanafurahia harufu ya chakula lakini Zaidi wingi wa chakula kile, Bianca anawakaribisha kwa moyo mkunjufu kabisa)

Bianca: jisikieni nyumbani

Post a Comment

0 Comments