I KILLED MY LOVER 22

 


SCENE 22: -

END OF FLASHBACK

(Tunarudi mahakamani ambapo Liliana anaendelea kuwasimulia kisa chote cha kwanini alimuua Robert ambae alikuwa baba wa mtoto wake na hawara wa muda mrefu sana. hakimu anaamua awapumzishe watu kwanza kabla ya kuendelea na kusikilizwa kwa kisa chote. kisa hicho kinaonekana kuwagusa baadhi ya watu maana wanaonekana wanalia wengine wanasikitika tu)

Hakimu: mahakama itaendelea kusikiliza mkasa huu jumatatu inayokuja hivyo nawaomba muendelee kujiandaa (anagonga meza kisha anaondoka)

Watu :( wanasimama)

Hakimu :( anaondoka)

(Watu wanatawanyika)

Lydia :( anamuendea Liliana) Pole Kwa maisha uliyopitia binti ila ningependa kujua kwanini ulimuua mume wangu?

Liliana: fika jumatatu utajua tu kwanini nilimuua mumeo

Raphael: pole Liliana kwa kila kitu kilichowahi kukutokea katika maisha yako, dah (anaonyesha kusikitika sana) umeteseka sana, umepitia mengi sana kwenye hii dunia una umri mdogo sana ila dah umepitia mengi sana, umebakwa sana nimesikia ulibakwa mara mbili na mjomba wako na mlinzi mmoja

Liliana: ndio

Raphael: pole Sana…

Liliana: ah Ni mapito tu ya dunia

Raphael: Ni kweli

Lydia: huyo mama aliyekulea alikuwa anaitwa Bianca ee

Liliana: ndio

Lydia: yuko wapi yeye simuoni

Liliana :( machozi yanamtoka)

Raphael: its okay Kama hutaki na wala hujisikii kuongelea hilo sasa hivi

Liliana: nitamzungumzia jumatatu

Lydia: sawa haina shida

Raphael :( anamuangalia Liliana kivingine kabisa)

Lydia :( anagundua kwamba mwanae anamuangalia Liliana) wewe ndo nini?

Gabriel :( anakuja walipo kina Liliana) pole Liliana Kwa yote tunatamani kusikia kisa hicho Zaidi ili tujue baba aliingiaje hapo mpaka ukamuua

Liliana: subirini jumatatu kila kitu kitaeleweka

Raphael: anyway…Anna yule binamu yako aliyekupigania mpaka akaleta watu wa haki za watoto nyumbani kwenu yuko wapi?

Liliana: alikuwepo hapa…sijui kaenda wapi

(Kuna sauti inatokea nyuma)

Sauti: Liliana?

Liliana :( anageuka) okay…tumemuongelea na yeye kafika

Anna :( binti mkubwa kabisa na ni mrembo sana)

Raphael: okay…na Bella

Anna: anakuja

Gabriel: habari zenu

Bella :( nae anafika) Liliana…

Raphael: yaani Liliana ametusimulia stori vizuri mpaka nimejikuta nawajua hawa watu… (kwa Bella na Anna) nyie mbona mmekuwa hivi?

(Wote wanacheka)

Anna: unatuona sisi tu je Liliana humuoni?

Raphael: (anacheka Sana)

Lydia :( anaonekana kutofurahia maongezi Yale)

(Polisi magereza wanakuja na kumchukua Liliana)

Liliana: tutaonana jumatatu

(Anna na bella wanaonekana kuwa na huzuni sana)

Anna :( anawaaga) jamani sie tunaenda

Bella: sisi tunaenda

Lydia: haya

(Anna na Bella wanaondoka)

Raphael :( anamuangalia Liliana kisha anajisemea moyoni) nampenda huyu mwanamke, najua aliniulia baba yangu na najua siku ya kwanza naonana nae nilimzingua sana ila leo nakiri kuwa nampenda jamani

Lilianaa :( anachukulia anarudi rumande)

Raphael: you will go through this

Lydia: jamani…we Raphael unawaza nini mbona sikuelewi muda mrefu

Rapahel: kivipi mama…Mimi sikuelewi wewe

Lydia: unamuangalia Sana katika aina ambayo siielewi

Gabriel: vyovyote vile kumbuka huyu mwanamke ni muuaji wa baba yetu na usisahau hilo

Raphael: embu subirini kwani kumuongelesha mtu vizuri ni dhambi?

Gabriel: hapana…sio kwamba kumuongelesha mtu vizuri dhambi…mama anaogopa kitu Fulani unavyomuangalia ni kama mtu unaemtamani

Raphael: oh, comeon Gabriel wewe nani kakwambia kuwa namtamani Liliana, for God’s sake alimuua baba yetu jamani mnahisije kuwa naweza kuwa nimempenda kwanza ana mtoto wa baba

Michael:(anakuja) hey…Liliana yuko wapi?

Raphael: amesharudi rumande

Lydia: huna hasira nae na wewe Michael…yaani mimi hata siwaelewi wote mnajua

Michael: mama bado hajamaliza kutusimulia sisi na mahakama akimaliza ndo tutapima hata mahakama itapima kwa sasa naomba tu tuwe wapole maana hatujui baada yay eye na mama yake kuwakaribisha mjomba na shangazi yake kwenye familia nini kilitokea

Raphael: Na baba aliingiaje hapo

Lydia: but still amemuua mume wangu

Raphael: hakuna anayekataa kuwa amemuua baba

Gabriel: yeah wanasema no one is guilty until proven by court of law hivyo basi Kama anavyosema Michael tusubiri

Lydia: tusubiri nini? Kwani nyie hamuoni kuwa alimuua baba yenu

Gabriel: mama yaani wewe huelewi ni hapo?

Lydia: kwamba pamoja na kwamba alimuua baba yenu bado mnamtetea sana

Raphael: tunamuhurumia Kwa hadithi aliyotupa hilo la kumuua baba ni lingine na hakuna aliyekataa kuwa amemuua baba na kuchoma nyumba yetu ila tunamhurumia kwa hadithi aliyopitia

Gabriel :( anacheka kidogo) dogo unapambana kumtetea huyu ndugu

Lydia :( anaonekana kukasirika Sana)

Michael :( anamshika mama yake) mama just chill usije ukapandwa presha bure

Gabriel: tuondokeni tujiandae Kwa ajili ya jumatatu

Michael: exactly

(Wanaondoka huku kila mmoja wao kasoro mama Yao amehuzunishwa na hadithi fupi aliyoitoa Liliana)

Raphael :( yupo kwenye gari ameshakaa ila ana mawazo yake mwenyewe) Liliana…iam sure hili nalo litapita…nimekupenda Liliana tangu siku ya kwanza nakuona nilikupenda ulionekana huna ukatili wowote

Gabriel :( anajisemea moyoni huku anamuangalia Raphael) dogo keshapenda huyu (anacheka)

(Safari inaendelea huku kila mmoja wao anawaza yake kichwani mwake)

Post a Comment

0 Comments