I KILLED MY LOVER 23

 


SCENE 23: -

JUMATATU

(asubuhi ya siku ya jumatatu siku ambayo kesi ya mauaji inayomkabili Liliana inaendelea kusikilizwa, watu wakiwemo familia ya bwana Robert inaingia mahakamani kwa ajili ya kusikiliza kesi hiyo, baada ya watu kukaa na kutulia Liliana anakuja akiwa anasindikizwa na askari magereza, anasimama kizimbani na hakimu anamruhusu kuendelea na simulizi ili wapate sababu ya yeye kumuua Robert ambae alikuwa ni hawara yake, baada ya kupewa nafasi hiyo anaendelea na simulizi hiyo)

FLASHBACK: -

(mchana mzuri kabisa, jua linachoma sana, Bianca, Liliana, shangazi, annna, Bella pamoja na mjomba wapo uwanja wa ndege kwa ajili ya safari ya kwenda India kwa ajili ya matibabu ya mjomba)

Bianca :( anapiga simu) ah huyu nae mbona hafiki hapa unajua tunaweza kuchelewa yaani watu bwana

(Simu inaita)

Mtu:(anapokea simu)

Bianca: finally, jamani umepokea simu…njoo basi unajua tunakusubiri wewe tu

Mtu: samahani boss nakuja

Bianca: okay fanya haraka (anakata simu) ah…unajua kaka unaenda na meneja wangu mimi nitabaki hapa kumlea mwanangu na pia kuangalia biashara zangu

Mjomba: haina shida dada nakushukuru sana

Shangazi:(anabenjua midomo kama hapendi)

Bianca: usijali kabisa kaka yangu (anamuangalia shangazi) na wifi atakuwa kazini na akiwa na akili mambo yatanyooka na Maisha yatarudi kama hapo awali…

Mjomba: oh, asante sana dada yangu wewe ni kama malaika uliyetumwa na Mungu mwenyewe kuja kuniokoa mimi na familia yangu

Bianca:(anacheka kidogo) ila mbona kama vile wifi anaonekana hapendi? yaani au hataki kufanya kazi inawezekana tu wewe ukae nyumbani haina shida

Mjomba: hapana dada usimjali huyu…wewe fanya unachopanga dada yangu ni kitu kizuri tu dada…

Bianca:(anamshika Liliana) mwanangu…muage mjomba anaenda India kutibiwa

Liliana:(anatabasamu kidogo) safari njema mjomba wangu

Mjomba: asante sana mwanangu

Shangazi:(anacheka kimbea) eti mwanangu…mwanao? ungekuwa unambaka kila usiku utasema ni mkeo?

Bianca:(anakasirika sana)

Liliana:(anabaki anamshangaa sana)

Bianca: sasa hayo yameingiaje huku sisi tunaagana ili kaka yangu hapa aende India akiwa na Amani na furaha...

Liliana:(kimya)

Anna: mama…

Shangazi: kelele…na wewe

Bianca: wewe dada vipi? mbona unakuwa kama mwendawazimu wewe?

Shangazi: mwendawazimu ni wewe…sijui unafanya hayo kwa mume wangu ili umchukue nimeshakujua mipango yako

Bella: mama?

Shangazi: nini mnadhani siwezi kusema kwasababu eti yeye ni tajiri?

Bianca:(anakasirika sana)

Shangazi: huna mume unamendea waume za watu kama ulivyomendea mtoto wa watu

Bianca:(anashikwa hasira na machozi yanamlenga)

Liliana:(anamshika Bianca bega) mama

Shangazi: yaani nyie mnachonyenyekea ni kwamba mnamuogopa kwa ajili ya mali zake...na sio vinginevyo

Anna: mama huo sio ukweli…mama yake Liliana ni mtu mzuri sana na sote tunampenda sababu ya roho yake nzuri…wewe ndo mwenye roho mbaya mama

Shangazi:(anamzaba kofi Anna) wewe mtoto shika adabu yako …mimi ni mama yako

Anna: una roho mbaya sana mama

Shangazi:(anataka kumpiga kofi)

Bianca:(anamzuia) inatosha…acha ukichaa wako wewe mwanamke

Shangazi:na hiyo kazi yako siitaki

Bianca: sijakulazimisha…unaweza ukaacha

Shangazi:na wanangu sitaki uwasaidie

Bella: mimi nataka kusaidiwa kwa kweli

Shangazi: mimi ndo mama yako na nimesema hiyo kuwa sitaki muende shule hiyo aliyosema huyu mwanamke

Anna: tunaenda

Shangazi: halafu wewe Anna wewe unajifanya wewe ndo wewe…unanijibu mimi ni mama yako

Mjomba: mama usiyejitambua…embu acha ujinga wako wewe…na utulie tupo kwenye halaiki ya watu hapa

Shangazi: unadhani naogopa kwamba tupo kwa watu? siogopi na wala sijali (anapaza sauti) simpendi huyu mwanamke mjinga mjinga

Bianca: usiniite mimi mjinga…wewe dada hunijui

Shangazi:na wala sitaki kukujua mwanamke uliyekuja kuharibu familia yangu

Mjomba: familia uliiharibu mwenyewe ndugu yangu na unalijua hilo

Shangazi: yaani hata sikutaka kuwepo hapa

Bianca:(anaita) security…kuna mtu anatusumbua hapa

(Security wanakuja mahali hapo)

Mmoja wa walinzi: aunt ni nani analeta fujo mahali hapa?

Bianca:(anamnyooshea kidole shangazi)

Mlinzi: samahani... (anamshika shangazi) naomba utoke nje hatuhitaji watu wakorofi ndani hapa

Shangazi: nataka kumuaga mume wangu anasafiri

Mlinzi: toka nje tafadhali

Shangazi: sitoki sasa

Mlinzi: unataka tutumie nguvu?

Shangazi: jaribuni muone timbwili lake

(Walinzi wanaangaliana kisha kwa nguvu wanamvutia nje)

Bianca: unaleta ubabe kwenye hamna… (kwa watoto wa mjomba) hivi mnaishi vipi huko?

Anna:(anaguna)

Meneja:(anakuja) samahani boss nimechelewa

Bianca: sio sana...haya jiandaeni muondoke

Meneja: haina shida mkuu

Bianca: mambo mengine tutakuwa tunawasiliana…

Meneja: sawa boss

Bianca: kila kitu kipo tayari ni kufika tu na kutibiwa…malzi na chakula vyote vipo vizuri

Meneja: sawa boss

Mjomba: asante sana dada Mungu akuzidishie

Bianca: usijali ni kidogo sana hicho…nafanya hivi kwasababu ya Liliana

Mjomba: usijali dada nakushukuru sana

Bianca: nendeni ndege yenu imeshatangazwa

(Wanaagana kisha mjomba na meneja wanaondoka na kuwaacha kina Bianca wanajiandaa kuondoka kurudi nyumbani)

Post a Comment

0 Comments