I KILLED MY LOVER 29

 


SCENE 29: -

KESHO YAKE ASUBUHI: -

(Liliana anatoka chumbani kwake akiwa bado amevaa nguo za kulalia anaenda moja kwa moja mpaka chumba maalumu cha kupata chakula (dining room), huko anawakuta wafanya kazi wake wanaandaa meza kwa ajili ya watu kupata kifungua kinywa)

Liliana:(kwa mpishi) shikamoo dada Siwema

Siwema: marahaba…umeamkaje? (kwa mshangao kidogo) leo mbona umechelewa kuamka?

Liliana: ah (anacheka)jana nilichelewa kulala

Siwema: mbona uliingia mapema chumbani kwako?

Liliana: nilikuwa naangalia tamthilia

Siwema:(anacheka) au ulikuwa unaongea na shemeji?

Liliana:(anacheka) lakini mna nini nyie?

Siwema: sio vibaya ukiwa nae na wala hadhuru kuwa nae

(Wanacheka)

Bianca:(anakuja mahali hapo) za asubuhi (anavuta kiti anakaa)

Liliana:(anasimama na kwenda kumbusu mama yake shavuni)

Bianca:(anambusu pia) good morning child

Liliana: morning mama

Bianca: umechelewa sana kuamka

Liliana: iam so sorry mama

Bianca: huna vipindi chuoni

Liliana:ni mchana mama sasa hivi nakaa nyumbani siku nzima nipo kwa ajili yako

Bianca: nice, na nilikuwa nimemisi sana kukaa na wewe…sasa unaonaje asubuhi hii ukaenda kule mashineni mimi nimezeeka nimechoka sana na pia sioni vizuri

Liliana: haina shida mama…nitaenda

Bianca: ukirudi najua utaenda chuo ukirudi kutoka chuo tutatoka mimi na wewe tukakae mahali tufurahie

Liliana: ah…mama nilitaka kukuambia kuwa jioni nitakuwa na mtoko

Bianca:na kina Anna?

Liliana: No mama

Siwema: ndo maana umechelewa kuamka leo

(Wanacheka)

Liliana: jamani dada

Bianca:(anatabasamu) oh jamani nina mkwe?

Liliana: hapana mama si nilikuambia bado ndo kwanza tunaanza kujuana

Bianca: okay mama ila you have to be very careful my child hawa vijana siku hizi wana mambo mengi sana

Liliana: mama sio kijana ni mtu mzima

Bianca: that’s good my dear

Liliana:(anacheka)

Siwema: mlete tumuone shemeji

Liliana:(kwa Siwema) bado hatujaanza mahusiano na wala hatujui kama tutakuwa na chochote kati yetu

Bianca: mtakuwa tu na chochote nawaombea

Liliana:(anacheka)

Bianca: ila mimi nina vituko natamani kumjua tu hata kama hamjaanza mahusiano nataka kumuona mwanaume aliyefanikiwa kuubeba moyo wa mwanangu kipenzi

Liliana: mama hata sina uhakika kama nampenda

Bianca:(anacheka) unanidanganya hata mimi shoga yako?

Liliana: kweli

Bianca: mlete nataka kumuona

Liliana: mama

Bianca: consider me your friend usinifiche nataka kumuona kuanzia mwanzo mpaka mwisho…kwani hajaoa?maana umeniambia ni mtu mzima

Liliana: alikuwa na familia ila kwa bahati mbaya wote wakafariki kwneye ajali ya ndege

(Siwema na Bianca wanasikitika)

Bianca: dah kupoteza wapendwa wake kwa wakati mmoja this must be very challenging

Liliana: sana

Siwema: sasa wewe ndo ujipange umpe watoto kwa mkupuo ili aone anaweza kuwa na amani tena

Liliana:(anacheka) jamani mimi sijaanza nae mahusiano naongea just nimempenda

Bianca: najua ila sisi tunaongelea tu ukipata nafasi hiyo ndo ufanye yote hayo kama kunionyesha, kumzalia watoto kwa mkupuo

Liliana: yaani nyie wawili mnapenda umbea Loh

Siwema:(anacheka kimbea)

Bianca: umbea kwa mwanamke ni kawaida kusutwa suna shoga yangu

Liliana: mama

(Wanacheka)

Siwema: sasa ukimleta nyumbani si tunaanza kuandaa harusi

Liliana:(anashangaa) walaaaaaa…

Siwema: jamani

Bianca:(anacheka) mwenzangu wewe Siwema umetisha kuzidi mimi

Siwema: nimefanyaje anti

Bianca: yaani kuja mara ya kwanza tu tayari unataka na wali (anashangaa)umenimaliza nguvu (anacheka sana)

Liliana: jamani nawapenda mnapenda sana kunipa raha

Bianca:na sisi tunakupenda zaidi

Siwema: tuletee tu huyo shemeji

Bianca:(kwa Siwema) wewe nae si amesema kuwa atamleta au?

Siwema: sijasikia vizuri

(Wote wanacheka)

Liliana: jamani kuna watu wana vituko kwenye huu ulimwengu loh

Siwema:(anacheka kidogo) sasa kama sijasikia nisiseme

Bianca:(anakunywa chai yake) enhe…kwahiyo Liliana unaenda mashineni

Liliana: naenda muda sio mrefu ngoja nikaoge

Bianca: okay my child ila usisahau kumleta mkwe

Liliana: mama

(Wanacheka)

Siwema: sasa nani ana shauku kuzidi mwenzie

Bianca:si wewe mpaka unataka wali kabla hata ya watu hawajuana vizuri

Siwema:na sisi tunataka wali sio kila siku sijui kwa jirani Fulani mara nani mara nani na mimi nataka humu ndani

Bianca: kuwa mpole

Liliana:(ananyanyuka) ngoja mimi niondoke maana nikiendelea kuwashangaa nitawashangaa mpaka ratiba zangu zitaingiliana (anacheka huku anaelekea chumbani kwake)

Bianca: wacha weeeeee mbona ratibaaaaa (anacheka kimbea)

Siwema:(anacheka pia)

Post a Comment

0 Comments