I KILLED MY LOVER 30

 


SCENE 30: -

USIKU WA SIKU ILE ILE: -

(Majira ya saa moja na nusu, hali ya hewa ni ya kawaida kama siku zote kaubaridi kwa mbali na utulivu wa hali ya juu, Liliana anafika katika mgahawa mmoja maarufu akiwa anaendeshwa na dereva wa familia yake)

Dereva: madam, tumeshafika je una lolote la kunielekeza?

Liliana: asante sana anko kwa sasa sina la ziada nitakupigia baadae kidogo baada ya kumaliza

Dereva: sawa madam

Liliana:(anashuka kwenye gari, anachukua simu yake) embu ngoja nimpigie nijue kama amefika au mimi ndo nimewahi nisije nikaonekana nina kihelehele bure

Dereva: naweza kwenda? Au kuna tatizo?

Liliana: hakuna tatizo anko wewe nenda tu

Dereva:(anaondoa gari mahali hapo)

Liliana: mbona hapokei simu huyu mtu ni ana nini?

(Simu yake inaita)

Liliana:(anapokea) hello

Sauti nzito ya kiume: samahani mrembo sikusikia simu

Liliana:(anatabasamu) oh Robert uko wapi?

Robert: tulipokubaliana…. kukutana…

Liliana: mimi nipo hapo Robert

Robert: nipe kama dakika moja nije nikuchukue malkia...mrembo kama wewe unatakiwa usije ukaingia sehemu kama hii peke yako

Liliana:(anacheka kidogo) sawa nakusubiri Robert

(Wanakata simu)

Liliana:(anasimama kusubiri)

(Baada ya kama dakika mbili hivi Robert anakuja mahali hapo)

Robert: hello beautiful

Liliana:(anageuka huku anatabasamu) Hi

Robert:(anambusu shavuni) karibu… (anamshika mkono kisha anaingia nae ndani)

Liliana: wow…this restaurant is very beautiful

Robert:(anatabasamu) not as beautiful as you are

(Wanafika kwenye meza alipokuwa amekaa Robert)

Robert:(anampa Liliana ua) this is for your beauty… (anavuta kiti)

Liliana:(anapokea huku anatabasamu) asante sana Robert(anakaa)oh you are such a gentleman

Robert:(anasukuma kiti na kuhakikisha Liliana amekaa vizuri kisha anarudi kukaa kwenye kiti chake, anachukua glasi yake iliyo na wine anakunywa kidogo) karibu wine

Liliana: iam so sorry I don’t drink

Robert:(anaangaza macho yake anamuona mhudumu) dada…samahani

Mhudumu:(anamjia Robert) karibu...

Robert: msikilize mrembo hapa

Liliana: Malta ...only grand malta…

Robert:(anakunywa kinywaji chake kidogo) nadhani ungejaribu wine iko poa sana

Liliana: usijali next time

Robert: una misimamo

Liliana:(anacheka) nimefundishwa na mama yangu

Robert: oh my God…I must meet your mother…

Liliana: utampenda…she is my best friend…yaani tunataniana kama tunalingana…yaani mama yangu ni kila kitu nampenda sana

Robert: wow

Liliana: kweli ni muhimu umuone utampenda sana

Robert: anaonekana ni mrembo sana kama wewe ni mrembo kiasi hiki yeye anaonekana ni kisu…maana wanasema a fruit doesn’t fall far from its tree...yaani tunda halianguki mbali na mti wake…

(Wanacheka)

Liliana: kabisa…

(Kimya kidogo huku kila mmoja wao anawaza kitu Fulani kichwani mwake)

Liliana:(anakohoa kidogo)

Robert: I love you Liliana kweli natamani uwe wangu uwe mama wa watoto wangu wapya nataka kuanza familia mpya niondokane na huu upweke my dear

Liliana:(anabaki amepigwa butwaa)

Robert: unaweza ukafikiria kwanza sio lazima unijibu leo hii unaweza ukanijibu hata baada ya siku mbili wala sina haraka mrembo

Liliana: nitakujibu Robert…

Robert: asante naomba uendelee kufurahia usiku wako na usifikirie chochote right now kila kitu kifikirie baada ya hapa kwa sasa naomba niwe na wewe kimwili na kiroho

(Wanacheka)

Liliana: eti kimwili na kiroho

Mhudumu:(analeta kinywaji cha Liliana)

Robert:(anashika menu) wa jikoni yuko wapi? namuomba

Mhudumu: sawa ngoja nikamuite(anaondoka)

Robert:(kwa Liliana) cheers (ananyanyua glasi)

Liliana :(ananyanyua kinywaji chake) cheers

(Wanagonga glasi)

Robert: iam so happy today…

Liliana: kwanini?

Robert: napenda kampani yako na tangu siku ya kwanza nimekuona nilikuwa natamani nipate wasaa kama huu ila nikakosa sasa leo nimepata nimefarijika sana

Liliana: usijali…

Robert: nitafurahi sana siku nikikupata

Liliana:(anacheka kwa aibu)

Robert:(anatabasamu)

Mpishi:(anakuja) karibuni

(Wanaagiza chakula kisha mpishi anaondoka kurudi jikoni baada ya kuwasikiliza)

Robert: naomba nikualike kwenye sherehe ya kufungua tawi la moja ya kampuni zangu siku ya jumamosi kama utakuwa free

Liliana: oh, asante sana nitakuwa free jumamosi mara nyingi nakuwa sina kazi nyingi

Robert: karibu sana

Liliana: asante sana nitakuja…tutaongea tu ni saa ngapi

Robert: nitakuambia kwenye simu ratiba kamili

Liliana: okay haina shida

Robert: :(anatabasamu) wewe ni mrembo sana

Liliana: hata wewe ni mtanashati sana

(Wanatabasamu kila mtu anaonekana kuvutiwa na mwenzie)

Post a Comment

0 Comments