I KILLED MY LOVER 31

 


SCENE 31: -

JUMAMOSI: -

SIKU YA SHEREHE: -

(majira ya saa 12 jioni, Liliana anahangaika na maandalizi ya kwenda kwenye sherehe aliyoalikwa na Robert)

Bianca: mbona upo juu juu unaogopa kuchelewa au unaogopa kukosa usafiri honey unajua kabisa una dereva wako na atakupeleka wakati wowote

Liliana:(anamalizia kuvaa) mama tatizo ni kwamba hata sijui ukumbi ulipo…na hata hivyo amesema kuwa atatuma dereva aje anichukue

Siwema:(anakuja) dear kuna gari nje linakusubiri

Liliana: are you serious?

Siwema: ndo nakwambia… (anaongea kwa kunong’ona) gari ni la ki fahari

Bianca: wache weeee (anatoka kwenda kulichungulia) Oh My God…mwanangu mzuri na hawezi kukosa mwanaume mwenye hadhi zake

Liliana:(anakuja akiwa amependeza sana)

Siwema na Bianca: oh My God…

Bianca: mwanangu wewe ni chombo

Siwema: hakika

Bianca:(anataka kulia)

Siwema:(kwa Bianca) sasa usianze kutaka kulia hapa kama wale wa mama wa kihindi wanaonyeshwa kwenye zee world

Bianca: hata siwaigi ila nimefurahi tu mwanangu kakua mkubwa na sasa ana maisha yake nakuombe kheri mwanangu

Liliana:(anatabasamu) asante mama

Bianca: nakupenda mwanangu enjoy your party

Liliana:(anamkumbatia)

Bianca: nisije nikakuharibia gauni lako mama…ni zuri

Siwema: amepewa zawadi na shemeji

Liliana: exactly

Bianca: wow…nataka kumuona mkwe wangu jamani

Liliana: utamuona soon

(Honi ya gari inapigwa)

Bianca: shoga nenda usije ukaonekana huna adabu bure mwanangu

Liliana:(anatoka nje lilipo gari)

(Bianca na siwema wanamfuata nyuma na akumsindikiza kwa macho)

Bianca: wow gari zuri ee

Siwema: sana

Bianca: mtoto wetu ana amani sana ona anavyotabasamu…

Siwema: kabisa Mungu ni mwaminifu…nakumbuka kalikuja kakiwa na umri wa miaka saba (7) kadogo hakana hata furaha, wala afya…

Bianca: uzuri wa moyo wake ni wa kusamehe, fikiria alimsamehe shangazi na mjomba wake…pamoja na mateso yale yote

Siwema: ndo maana Mungu amembariki sana

Bianca: namuombea Baraka zaidi

(Gari lililombeba Liliana linaondoka mahali hapo)

Bianca: Mungu amlinde mwanangu

Siwema: amina

Bianca: twende ndani na sisi kwa umbea

(Wanacheka huku wanaingia ndani)

Liliana:(amekaa kwenye gari kama malkia, anachezea simu mara ajipige picha mara ajiangalie nywele mara viatu yaani ilimradi tu afurahi)

(Baada ya mwendo wa dakika 30 njiani hatimaye wanafika kwenye ukumbi ulioandaliwa kwa ajili ya sherehe ya ufunguzi wa tawi la biashara nyingine ya Robert, Watu wamependeza sana na kuna shamrashamra za sherehe kila mgeni mualikwa ameshika kinywaji chake mkononi)

Liliana:(huku anashuka kutoka kwenye gari) kuna watu wengi sana

Dereva: yaani watu wengi sana ila usijali…nitakusindikiza mpaka kwenye meza iliyoandaliwa kwa ajili yako na meza hiyo ndo ya boss pia...

Liliana: oh My God asante sana kaka

(Dereva anamuongoza Liliana mpaka kwenye meza iliyokuwa tayari kwa ajili yake)

Dereva: hapa sasa ndo kwenye meza yako

Liliana:(anakaa) asante sana

Dereva:(anaondoka)

Robert:(anakuja huku mikononi mwake amebeba glasi mbili za vinywaji moja ni juisi na nyingine ni pombe kali) mrembo

Liliana:(anageuka) oh (anatabasamu)

Robert: karibu… (anamuangalia juu mpaka chini) umependeza sana mrembo (anampa kinywaji) asante sana kwa kukubali wito wangu

Liliana: asante pia kwa mwaliko (anapokea kinywaji) hata wewe umependeza

Robert:(anaachia tabasamu) asante mrembo

Liliana: kuna watu wengi sana leo

Robert: mimi ni mfanyabiashara mkubwa sana nadhani hata mama yako atakuwa ananijua

Liliana: itakuwa anakufahamu…maana hata yeye ni mfanyabiashara

Robert:ni muhimu nikutane nae huwezi jua naweza kupata business partner

Liliana: kabisa

(Kuna mtu anaongea stejini kunakuwa na utulivu)

Mtu: naomba nimkaribishe mkurugenzi mtendaji Bw. Robert

(Watu akiwemo Liliana wanapiga makofi)

Robert:(anaenda mbele na kufungua tawi rasmi)

(Watu wanapiga makofi)

Robert:(anarudi kukaa kwenye meza alipokaa Liliana)

Liliana: hongera kwa kufungua tawi…

Robert: asante mrembo...ningependa uje ufanye kazi na mimi

Liliana: what?

Robert: yes…njoo please I will be waiting au nitaonana na mama yako nimwambie…

Liliana: bado nasoma Robert

Robert: haijalishi…please naomba

Liliana: okay ngoja niongee na mama nitakujulisha

Robert: okay…

(Watu mbalimbali wanamfuata Robert kuna wengine wanaomba apige picha nao, wengine wanampongeza kwa kazi nzuri na mafanikio ya biashara yake)

Liliana:(anamuangalia huku anajisemea moyoni) ni mtu muhimu kumbe ona watu walivyo wengi…anafaa kuwa mwanaume wangu…(anatabasamu)

Robert:(anaendelea kuonyesha ukaribu kwa watu)

(Sherehe inaendelea na kila mmoja wao anaonekana kutosheka na kufurahia hafla hiyo ndogo)

Liliana:(anamuangalia Robert huku anatabasamu) he is the one!!!

Post a Comment

0 Comments