SCENE 32: -
(Kesho yake asubuhi Bianca
anaingia chumbani kwa Liliana ambae anaonekana bado amelala na wala hana dalili
za kuamka kwa wakati ule)
Bianca:(anafunua mapazia)
(Mwanga unaingia ndani)
Liliana:(kwa sauti ya usingizi) jamani da Siwema
Bianca:
sio Siwema ni mama
Liliana:(anakurupuka) shikamoo mama
Bianca:
marahaba…hujambo
Liliana:(anapiga miayo) sijambo
Bianca:
umechoka sana ee
Liliana:
kiasi mama(anatabasamu)
Bianca:
nambie mwanangu za kwenye sherehe?
Liliana:
nzuri… (ananyanyuka kutoka kitandani na
kwenda bafuni anachukua mswaki anasimama mlangoni ili aendelee kuongea na mama
yake)
Bianca:
jana ulirudi saa ngapi?
Liliana:
saa saba usiku
Bianca:(anashangaa) mbona hukuniamsha
Liliana:
mama jamani ningeanzia wapi? nilikuwa naona nitakusumbua hata hivyo nilikuwa
nina usingizi
Bianca:
enhe ilikuwaje
Liliana:(anapiga mswaki)
Bianca:
wewe nae niambie
Liliana:
tulikula, tulikunywa, tukacheza maisha yakawa mazuri kweli kweli
Bianca:
wow…enhe mkwe anasemaje kuhusu kuja huku?
Liliana:
atakuja mwisho wa mwezi huu…hata hivyo anataka kukutana na wewe…pia for
business purpose
Bianca:
unadhani mimi nina tatizo basi? (ananyanyua
mabega) yeye aje tu
Liliana:(anacheka)
Bianca:
lakini una amani mwanangu?
Liliana:
nina amani mama…mimi na yeye tumeanza mahusiano yetu
Bianca:
kweli?
Liliana:
yes, mama na ninajua mahusiano yetu yatadumu…(anatabasamu)jana amenionyesha kuwa mimi ni wa muhimu nilikaa meza
moja na yeye na unajua yeye ndo alikuwa mkurugenzi mtendaji…yaani acha tu
Bianca:
wow, nice child
Liliana
:( anacheka)
Bianca:
na mimi kwa umbea nimeshamwambia mjomba wako
Liliana:
sio mbaya mama
Bianca:
I hope hujachukia
Liliana:
wala maana hata Kama tungeficha vipi lazima angejua tu
Bianca
:( anatabasamu)
Liliana
:( anacheka) mama bwana
Bianca:
nimefanyaje?
Liliana:
yaani wewe mzungu kweli
Bianca:(anaguna kidogo) unajua kwanza umeshakuwa
kale kamtindo kakunyima ndo matokeo yake unaenda kuboronga huko tunabaki
tunatoa macho mimi nakuruhusu huku nakufundisha kama haupo tayari kuwa mama
sasa hivi kuwa makini…sikufundishi umalaya ila tu nahisi wewe ni msichana
mkubwa na ni mwanamke kamili nikisema nikunyime kuwa na mahusiano mimi
itanisaidia nini mimi? Matokeo yake utaenda huko ufanye bila kuwa na kinga
yakakukuta nikaumbuka na ukali wangu…ila tu kuwa makini mwanangu
Liliana:ni
kweli mama…
Bianca:
halafu wewe sio mtoto miaka yote mwanangu tangu nimekupata nimekuwa
nikikufundisha kuhusu haya si unakumbuka
Liliana:
ndio mama
Bianca:
kwahiyo unajua…sasa kama umepata tena mtu mzima I feel iko safe zaidi maana
hautapata mpasuko wa moyo
Liliana:
yes mama
Bianca:
umeshafika chuo najua akili yako ni pana sana
Liliana:
kabisa mama
Bianca:
mkwe anaitwa nani?
Liliana:
Robert
Bianca:
I feel he is good for you
Liliana
:( ananawa mdomo kisha anamuendea mama
yake) asante mama... (Anamkumbatia na
kumbusu)
Bianca:
okay ngoja tujiandae kwa mapokezi ya kumpokea kwenye familia tunataka kumuona
ili tujue mtu uliyenae
(Wanakumbatiana kwa mapenzi ya mama na mtoto)
0 Comments