SCENE 33: -
BAADA YA WIKI MBILI: -
(Majira ya saa moja usiku wanawake,
Bianca, Siwema, mfanya usafi, Liliana, Anna na Bella, wapo jikoni wanamalizia
maandalizi kwa ajili ya kumpokea Robert kwenye familia)
Bella
:( Kwa Liliana) Lione linavyotuweka
roho juu juu utasema tunapokea mahari Leo
Bianca:
si dalili jamani
(Wanacheka)
Mjomba
:( amekaa sebuleni peke yake) kwahiyo
Mimi mlinzi huku sebuleni
Bianca:
ukitaka njoo upike na kifua chako
(Wanacheka)
Anna:
anatujaribu ee
Siwema:
mi nishaanza kutenga
Bianca:
nyie huyu ana usongo… khaaaa
Liliana:
jamani si ndo maana kamili ya kuwa punctual hataki mambo yafanyike deadline
(Wanacheka)
Bianca:
aende zake huko
Siwema:
jamani Mimi Nina raha…leo namuona shemeji jamani
(Wanacheka)
Mjomba
:( anakuja walipo)
Bianca
:( anatania) maskini njaa imembana
mpaka kaona aje atusimamie
Mjomba:
namuona mlinzi anafungua geti halafu kuna gari Fulani linaingia sijui ni la
mgambo
(Wanakurupuka na kuanza kufanya
kazi kwa haraka Zaidi)
Bianca:
gari la mgambo wapi huku ni gari la mkwe
Siwema:
Yallah!!!!Yaani Shem kaja kabla ya sisi kumaliza kitu chochote jamani huko
kulikuwa sio kujivuta ni kuhangaisha
Liliana
:( anatoka na kwenda nje)
Robert
:( Kama kawaida yake kupendeza anashuka
kutoka kwenye gari lake la kifahari)
Liliana
:( anamuona) wow...Umependeza
Robert
:( anaachia tabasamu la kuvutia Zaidi)
Asante
Liliana:
karibu nyumbani nadhani huwa unakuja ila mara nyingi unaishia nje
Robert:
yes
Liliana:
karibu ndani Leo baby
Robert
:( anatabasamu) Asante mama (anamkumbatia)
Liliana
:( anamkumbatia pia)
(Bianca, Anna, Bella na Siwema
wamesimama dirishani wanachungulia)
Bianca:
aaaah mkwe mzuri bwana
Siwema:
ndo maana Liliana wetu kanasa hapo
Mjomba:
kuna majitu ni mambea
Bianca:
eeeh eeh wewe umbea kwa mwanamke ni kawaida kusutwa suna babuuuuuu
Mjomba:
wache weeeeee…
(Liliana na Robert wanaingia ndani walipo
wengine)
Bianca:
karibu Sana baba
Robert:
oh, Asante Sana mama (anamshika mkono)
na wewe ni…
Bianca
:( anampa mkono) Bianca…mama Liliana
Robert:
wow…nimeona tunda halianguki mbali na mti wake
Bianca
:( anacheka) kwanini?
Robert:
you are as beautiful as Liliana
(Wanacheka)
Liliana
:( anaenda Kwa mjomba) Na huyu ni
mjomba wangu…
Robert
:( anampa mkono)
Mjomba
:( anamkumbatia) karibu Sana mkwe
Robert:
Asante Sana mjomba
(Wanacheka)
Liliana
:( Kwa Anna na Bella) hawa ni my
bestfriends, my cousins and my sisters
Robert:
wow… (Anawapa mikono)
Anna
na Bella :( wanamsalimia)
Robert:
marahaba
Liliana:(kwa Siwema na wafanyakazi wengine) na
hawa ni marafiki zangu na dada zangu wa nguvu
Robert:
oh (anawasalimia)
Siwema:
Karibu shemeji yangu
Robert:
Asante Sana
Bianca
:( anaketi kwenye sofa kubwa)
tafadhali karibu mketi jamani msisimame
(Wanakaa kila mmoja kwenye Sofa
Lake)
Bianca
:( Kwa Liliana) come child come sit
with me
Liliana
:( anakaa pembeni ya mama yake)
Bianca
:( Kwa Siwema) njoo mara moja dear
Siwema
:( anamuendea Bianca)
Bianca
:( ananong’ona) andaa supu watu
wakute wanaburudisha midomo Yao
Siwema:
sawa aunt (anaondoka)
Bianca
:( Kwa Robert) jisikie nyumbani baba…
Robert:
Asante mama…Asante kwa mwaliko huu kiukweli nimefurahi sana kuwepo hapa jioni
ya leo
Bianca
:( anatabasamu) tumefurahi kwamba
umekubali wito wetu…tumefurahi Sana kuwa na wewe jioni ya leo
(Siwema na wafanyakazi wengine
wanaleta supu kwenye trei lenye matairi, wanaendesha mpaka walipo watu, watu
wote waliopo sebuleni wanachukua bakuli la supu kwa zamu)
Robert
:( anaonja) wow…wonderful soup
Bianca
:( anatabasamu) mambo ya mwanangu Liliana
Robert
:( anacheka) Safi Sana
Liliana
:( anacheka Kwa aibu)
Robert
:( anamuangalia Liliana kisha
anatabasamu)
(Watu wanaonekana kufurahia
maongezi na ugeni ule, wanaongea mambo mengi sana yahusuyo maisha. Kila mmoja
kwenye familia anaonekana kumpokea vizuri Robert mpenzi wa Liliana)
Siwema
:( anatoa vyombo vya supu)
Robert:
wow nimeenjoi supu
Bianca:
eti eeh…. (Anamuangalia siwema)
chakula tayari?
Siwema:
ndio aunt
Bianca:
karibuni mezani jamani (anaongoza njia)
(Watu wanamfuata nyuma,
wanapofika mezani wanakaa kwenye viti, kila mmoja na sahani yake, wanapakua
chakula kwa zamu na kila kitu kinaonekana kuwa sawa kati ya familia hiyo na
mgeni wao, wanakula huku wanaendelea na mazungumzo. wanakunywa vinywaji
mbalimbali na kila mmoja wao amependeza sana ama hakika walikuwa wamejipanga
kwa ugeni ule)
Bianca:
nimeenjoi jamani…nyinyi je
Wote:
tumeenjoi pia (wanagonga glasi ishara ya
kufurahia maisha)
0 Comments