I KILLED MY LOVER 34

 


SCENE 34: -

(Asubuhi ya kesho yake siku moja baada ya Liliana kumtambulisha mpenzi wake kwa familia yake, Robert anafika nyumbani kwa kina Liliana akiwa ni mtu mwenye furaha sana)

Robert :( anapiga honi)

Mlinzi :( anatoka) oh shemeji…unamtaka Liliana

Robert: eeh muite siingii ndani…

Mlinzi: ingia bwana yaani kila mtu anakupenda jamani humu ndani

Robert: kuna kitu nataka kumwambia Liliana nampigia simu yake simpati

Liliana :( anatoka nje) oh Rob?

Robert: Yes Lily…

Liliana: njoo ndani bwana

Robert: No kuna sehemu naenda na ninachelewa sana njoo nikwambie nachotaka kukuambia halafu mimi naondoka

Liliana :( anamuendea) nambie baby (anambusu)

Robert :( anambusu pia)

Liliana :( anaingia ndani ya gari)

Robert: I missed you baby (anatabasamu)

Liliana :( anatabasamu) Asante and I missed you too my love

Robert: nilikupenda Zaidi siku Jana

Liliana: kwanini?

 Robert: ukiona mwanamke anatoka katika familia yenye watu wenye upendo kiasi hicho ujue mwanamke huyo ni mwanamke mzuri sana

Liliana: kivipi?

Robert: kwamba ni wife material

(Wanacheka)

Liliana: Asante sana dear kiukweli ndugu zangu walifurahi sana

Robert: nataka twende Zanzibar

Liliana: kuna nini tena baby?

Robert: kutalii tu

Liliana: oh, tunaenda lini?

Robert: wikiendi hii...

Liliana: okay baby nitamwambia mama kuhusu Hilo halafu nitakupa jibu

Robert: sawa mpenzi wangu…halafu umependeza halafu unanukia Sana

Liliana: oh, baby Asante Sana na wewe umependeza na ofcourse unanukia sana

Robert :( anacheka kidogo) so tunaenda wote au?

Liliana: wapi?

Robert: ofisini kwangu

Liliana: No baby

Robert: kwanini?

Liliana: Nina kipindi chuoni muda sio mrefu nasubiri gari yangu itoke gereji niondoke

Robert: baby…kwanini nisikupeleke chuo?

Liliana: hapana sitaki kukuchelewesha mpenzi wangu…wewe nenda tu nikifika nitakutaarifu

Robert: okay baby…I love you

Liliana: I love you too my love

(Wanakumbatiana)

Liliana :( anashuka kwenye gari)

Robert: tutaonana baadae baby… (Anatabasamu) mama mzungu huyo

Liliana: si nilikuambia (anacheka pia)

Robert: nimempenda bure

Liliana :( anacheka) nitamuambia kuwa umempenda (anacheka Sana)

Robert: tunda halianguki mbali na mti wake

Liliana: una maana gani?

Robert: wewe na mama yako ni warembo sana

Liliana :( anacheka Sana)

Robert: of course, Na binamu zako wote warembo Sana

Liliana: yes, my love

Robert :( anacheka) haya kajiandae uende chuo

Liliana: sawa baby nikirudi nitamwambia mama

Robert: mwambie mama Nampa hi yeye ni mzungu sana yaani ana tamaduni za kizungu sana

Liliana: hiyo kuniruhusu kuwa kwenye mahusiano huku nasoma?

Robert: Sana

Liliana: kawaida tu mbona

Robert :( anacheka kisha anawasha gari na kuondoka zake)

Liliana:(anabaki anatabasamu) nafurahia maisha yangu kwakweli… (anavuta pumzi) imekuwaje mpaka maisha yangu yaebadilika kiasi hicho…sasa nina ndugu wananipenda…nina maisha (Anaangalia jumba lile la kifahari) nina mama na Zaidi nina mwanaume anayenipenda kwa dhati nina kila kitu nilichokuwa nawazia…nikurudishie nini bwana

Mlinzi :( anamuona) unaongea peke yako dada Liliana

Liliana :( anacheka) acha tu niongee peke yangu Mungu aliyonipa ni Zaidi ya kila kitu

Mlinzi: mshukuru sasa

Liliana: namshukuru Sana tu

Mlinzi: una bahati Sana…anti anakupenda Sana

Liliana: hata Mimi nampenda Sana mama yangu hata mpenzi wangu amempenda Sana mama yangu

Mlinzi :( anatabasamu) shemeji ni mkubwa ila mnaendana sana

Liliana :( anacheka Sana) jamani

Mlinzi: kweli tena kwani kina Bella hawajakuambia?

Liliana: huwa wananiambia Sana tu

Mlinzi: unaona sasa inamaana ni kweli

Liliana :( anacheka) wewe bwana naomba uniambie Kama dereva amerudi nachelewa (anaangalia saa yake ya mkononi) nachelewa Sana

Dereva :( anafika)

Mlinzi :( anaangalia anapotokea dereva) na yeye hatajwi

(Wanacheka)

Mlinzi: yaani

Liliana :( Kwa dereva) umechelewa Sana kaka

Dereva: nisamehe Sana

Liliana: jamani usijali kaka yangu

Dereva: tunakupenda Sana yaani wewe ni mpenda watu sana

Liliana: jamani…nawapenda pia

Dereva: haya twende

(Wanapanda gari na kuondoka zao)

Mlinzi: baadae jamani

 

Post a Comment

0 Comments