I KILLED MY LOVER 35

 


SCENE 35: -

USIKU WA SIKU HIYOHIYO: -

(Usiku wa kawaida hali ya hewa ni ya kawaida sana, Bianca yupo chumbani kwake amekaa kitandani anasoma kitabu Fulani kama kawaida yake kabla ya kulala)

Bianca :( anavua miwani) ah nimechoka kweli Leo (anajinyoosha)

Liliana :( anagonga mlango) mama

Bianca: karibu mwanangu…

Liliana :( anafungua mlango)

Bianca: oh, my child…Leo hatujaonana kabisa

Liliana: kabisa mama...Tumekuwa tukipishana Sana

Bianca: karibu ukae mama

Liliana: Asante mama (anakaa pembeni yake)

Bianca: nambie…unaonekana umechoka Sana

Liliana: nimechoka ndio (anamuangalia usoni) wewe ndo umechoka Zaidi mama

Bianca: Ni kweli Leo nimeshinda kiwandani yaani nimechoka Sana

Liliana: pole Sana mama yangu ni muda wako muafaka sasa wa kupumzika...Mjomba si yupo?

Bianca: Ni kweli yupo ila sipendi kumchosha na yeye ana stress zake

Liliana: stress za kukosa mke au?

Bianca :( anacheka) sijui mwenyewe

Liliana: by the way mama…kwanini ulikataa mjomba akuoe

Bianca :( anacheka) wewe ni nani?

Liliana: mwanao

Bianca: Na yeye Ni?

Liliana: mjomba wangu…

Bianca: sasa nitaolewa vipi na kaka yangu

Liliana: jamani mama (anacheka)

Bianca: ndo hivyo…siwezi kuolewa na kaka yangu

Liliana: wacha weeee ila tungecheza kwenye harusi yenu...Fikiria basi

Bianca: wewe mtoto mjomba wako amekutuma nini?

Liliana: wala Mimi Nina shida zangu nyingine tu

Bianca: sawa nambie shida yako maana ushaanza kuniogopesha...Una shida gani?

Liliana :( anacheka kidogo) nambie

Bianca: wewe ndo uniambie shida yako mwanangu una shida gani? Au una mimba?

Liliana: jamani mama

Bianca: kwani vibaya? Nataka mjukuu nikae nae siku nzima namshika mashavu namchezea chezea

Liliana: kweli mama unataka mjukuu?

Bianca: kabisa

 Liliana: nitakupatia mjukuu mama

Bianca: Asante kwa kunipa ahadi nzuri kama hiyo

Liliana :( anacheka)

Bianca: enhe nambie sasa

Liliana: kuna mtoko wa kwenda   Zanzibar wikiendi hii…naweza kwenda mama?

Bianca: oh, my child uko huru kufanya yanayofurahisha nafsi yako

Liliana:(anafurahi) asante mama

Bianca: anything for you child

Liliana: tunaondoka ijumaa jioni tunarudi jumapili jioni

Bianca: okay child…haina shida Sana my love

Liliana: nakupenda mama

Bianca: nami nakupenda mwanangu

Liliana :( anamkumbatia) acha nikalale…usiku mwema mama

Bianca: usiku mwema mama… (Anamkumbatia pia)

Liliana: haya lala sasa

Bianca:(anacheka)

Liliana:(anaondoka)

Bianca:(anabaki anatabasamu anazima taa kisha anajifunika shuka na kulala)

Liliana: oh, my mama…Mungu amlinde mama yangu...aje ale matunda yangu (anapiga hatua kuelekea chumbani kwake) yupo kama mama yangu mzazi nakumbuka mama yangu alikuwa kama mama yangu Bianca...ni kama Mungu amemrudisha mama yangu kupitia Bianca…asante Mungu kwa nafasi hii ya kuwa na mama (anaingia chumbani kwake)

 

Post a Comment

0 Comments