I KILLED MY LOVER 36

 


SCENE 36: -

SAFARI YA KWENDA ZANZIBAR: -

(Liliana na Robert wanafika Zanzibar kwa ajili ya mapumziko ya mwisho wa wiki wanafika katika hoteli ya kifahari ya Golden Tulip Zanzibar Resort)

Robert: (anafika mapokezi) hello habari

Dada: salama shikamoo, karibu sana

Robert: asante…tulifanya booking online

Dada: jina

Robert: Robert Masaga

Dada: (anaangalia) sawa nimeona (Anampa ufunguo) karibuni sana na enjoy your stay

Robert: thank you so much

Dada: (anatabasamu)

Robert: (anamgeukia Liliana) twende baby

Dada: (anawaangalia) jamani huyo si baba na mwana? Au baby amemaanisha mtoto na sio mpenzi…eeh mdomo koma (anaendelea na kazi zake)

Robert: (anavuta begi huku anaangalia namba ya vyumba) najua umechoka baby…tutapumzika muda sio mrefu

Liliana: wala hata usijali nipo sawa

Robert: najua umechoka

Liliana: safari ilikuwa ya kawaida mbona hatujalala njiani tumekuja kwa ndege na pia nataka kufanya kitu kimoja tuweke mizigo kisha tukatalii nasikia Zanzibar pako vizuri sana kwa upande wa utalii

Robert: sana (anapata chumba anafungua) njoo tuingie hapa mara moja halafu tutatoka

Liliana: sawa baby...

Robert: call me daddy

Liliana: Daddy

(wanacheka)

Robert: (anaweka mizigo chumbani) basi sawa tunaweza kutoka sasa

Liliana: tutaenda wapi labda unapajua

Robert: hapana hata sipajui

Liliana: tutaulizia tu

Robert: sawa haina shida

Liliana: oh, I love Zanzibar

Robert: and I love you my love

Liliana: and I love you daddy…lakini Daddy tunafunga ndoa lini?

Robert: soon baby jiandae tu kuwa bibi harusi my love

Liliana: (anafurahi)

Robert: najua unatamani sana kuwa bibi harusi

Liliana: hakika tena wa kwako baby jamani ninavyokupenda

Robert: najua baby… (anaangaza angaza) okay tuulize watu sasa tunaanzia wapi?

Liliana: kwani baby tunakaa huku kwa siku ngapi?

Robert: siku moja tu najua unatakiwa uwe chuoni lakini pia na mimi natakiwa niwahi kazini

Liliana: lakini daddy hiyo ni mbaya jamani

Robert: kwanini?

Liliana: nataka nikae na wewe

Robert: kusoma kwanza

Liliana: ah daddy

Robert: ndo hivyo

Liliana: ila una roho nzuri sana na unijali sana asante baby kwa upendo wako

(Wanabusiana)

Robert: usijali nitakutunza milele malkia wangu

Liliana: na mimi nitakupenda milele I can’t wait for our wedding to happen

Robert: oh, you little mama

Liliana: napenda ukiniita hivyo

(Wanacheka wanashikana mkono kisha wanatoka nje tayari kwa ajili ya kutalii mji mkongwe na wa kihistoria mji wa Zanzibar)

Liliana: natamani iwe hivi siku zote

Robert: na itakuwa

Liliana: nataka kumnunulia zawadi mama

Robert: oh, gift for the beautiful mama

Liliana: (anacheka) yeah

(Wanaendelea kufurahia maisha)

Post a Comment

0 Comments