I KILLED MY LOVER 37

 


SCENE 37: -

BAADA YA SIKU TATU: -

NYUMBANI KWA BIANCA: -

(Jioni ya siku ya jumapili honi inasikika nyumbani kwa Bianca na haraka mlinzi anafungua geti. Gari la Robert linainga nyumbani hapo.)

Liliana: (kwa mlinzi) shikamoo Lupemba

Lupemba: marahaba malikia umerudi?

Liliana: nimerudi…

Lupemba: za Zanzibar

Lilian: salama

Lupemba: pamekupenda kweli umenawili sana

Liliana: (anatabasamu)

Robert: (kwa Lupemba) habari yako…

Lupemba: nzuri bwana shemeji…karibuni sana

Robert: asante sana (anaendesha gari mpaka eneo la maegesho)

Liliana: (anataka kushuka)

Robert: you are the queen acha nikufungulie

Liliana: ah thank you so much jamani

Robert: (anashuka anamfungulia mlango wa gari)

Liliana: (anashuka huku anatabasamu) shukrani daddy (anamuongoza njia kuelekea ndani)

(Bianca amekaa na Bella, Anna pamoja na baba yao yaani mjomba wake Liliana)

Bianca: (anamuona mwanae) jamani dear hupokei simu zangu wewe

Liliana: iam so sorry mama (anamuendea na kumkumbatia)

Bianca: (ananyanyuka na kumkumbatia pia)

Liliana: shikamoo mama

Bianca: marahaba shoga yangu na bora umekuja (anamuangalia Robert) mkwe habari yako

Robert: nzuri mama… (kwa wote) habari zenu

(Wanaitikia)

Liliana: (kwa mjomba) shikamoo mjomba

Mjomba: marahaba mama za Zanzibar

Liliana: nzuri

Mjomba: karibu

(Wafanyakazi wanachukua mizigo ya Liliana na kuingiza ndani)

Bianca: (kwa Robert) karibu uketi baba

Robert: no sikai mama…

Bianca: jamani… sawa kama umeamua hivyo

Robert: nitakuja siku nyingine sasa hivi nasubiriwa ofisini

Bianca: usijali… (kwa Liliana) haya mtoe mwenzio uje unipe ya Zanzibar

Liliana: (anacheka) haya mama (anamuongoza njia Robert kuelekea nje)

(Wakiwa nje)

Liliana: oh, daddy nilitaka nikae na wewe tena

Robert: tutaonana jioni basi

Liliana: haya

Robert: ila una mama mrembo sana…hivi hana mtu? Samahani kwa kukuuliza

Liliana: No daddy its okay…na pia mama hana mtu ingawa hata mjomba huwa anampenda

Robert: sasa mjomba na mama yako watapendana vipi?

Liliana: hivi sijakuambia ee ila mmoja wao hapo hatuna undugu wa damu kwahiyo sio mbaya wao kupendana

Robert: mama yako mpole sana mstaarabu sana yaani ni mwanamke ambae anafaa kwakweli

Liliana: daddy umeanza sasa mi naona wivu

Robert: ah nasema tu nampa sifa zake jamani kwani vibaya?

Liliana: hata hivyo nakutania bwana

Robert: najua

Liliana: haya wewe nenda nina mambo mengi sana ya kumwambia mama

Robert: really? (anacheka)

Liliana: yes, daddy

(Wanabusiana)

Robert: baadae

Liliana: see you baby

Robert: (anapanda gari lake na kuondoka zake)

Liliana: (anarudi ndani)

Anna: enhe binamu tuambie sasa

Bella: umependeza shogaaa uende ukaishi huko

Liliana: tutaenda kuishi na daddy baada ya harusi

Bianca: (anashangaa) Oh My God jamani unaolewa?

Liliana: ameniambia soon (anatabasamu)

Anna: all the best cuzo

Liliana: (anacheka huku anajitupa sofa karibu na alipokaa mjomba wako)

Anna: wewe mambo yameshaiva nini…Robert hataki ujinga asije akakosa chombo bureeee

Bella: umeona ee

Liliana: (kwa mjomba wake) mjomba unaonaje hii?

Mjomba: kama inakupa Amani basi na mimi nina Amani lakini

Liliana: nini mjomba?

Bianca: hivi mtamuweza huyu ana mambo mengi kichwani wala hakuna uwalakini hapo

Liliana: (anacheka)

Anna: nina furahi sana kama binamu yangu una Amani

Liliana: Robert is best man that I have always waited for

Bianca: I bless you child

Liliana: amen mama

Bianca: jamani (kwa wote) mimi nina njaa kama bado mnamshangaa aliyetoka Zanzibar pambaneni mtashinda (ananyanyuka na kuelekea eneo la chakula) na Siwema nae sijui kapata danga gani hayupo

(Wanacheka)

Siwema: aunt lakini mbona unapenda kunisingizia? (anamuona Liliana) wow jamani Liliana za huko

Bianca: ulikuwa umemkumbuka?

Siwema: saaaana mweee

Bianca: (anafyonza kisha anawageukia wengine) embu njooni tule jamani achaneni na Siwema ana matatizo

(Wanacheka huku wananyanyuka kuungana na Bianca kwa ajili ya chakula)

Bianca: (kwa Liliana) umekuwa mrembo kweli binti yangu

Liliana: (huku anakaa) asante mama

(Wanaanza kula huku wanazungumza masuala mbalimbali)

Post a Comment

0 Comments