I KILLED MY LOVER 38

 


SCENE 38: -

NYUMBANI KWA BIANCA: -

(Bianca anatoka ndani kwake huku anaongea na simu)

Bianca: (kwa Lupemba) Liliana yupo wapi?

Lupemba: yupo bustanini

Bianca: sawa (anaendelea kuogea na simu huku anaelekea bustanini alipo Liliana)

Liliana: (amekaa kwa utulivu huku anakunywa maziwa)

Bianca: (anamfikia) hi baby

Liliana: Hi mama

Bianca: mbona umekaa huku peke yako?

Liliana: (anamuegemea mama yake begani) hapana mama nimeamua tu kukaa huku

Bianca: any problem dear?

Liliana: No mama, nipo sawa kabisa mama yangu

Bianca: umeamua tu kukaa peke yako?

Liliana: ndio mama

Bianca: au umegombana na mkwe

Liliana: hapana mama tupo vizuri sana

Bianca: tunatakiwa kuandaa shera si umesema mtafunga ndoa hivi karibuni?

Liliana: yes, mama (anafurahi sana) yaani mama nampenda Robert na ananipenda pia

Bianca: nimekuwa naota kukuona ukiwa na furaha na ninaitamani siku hiyo mwanangu…yes Robert anaonekana ni mtu mzuri sana

Liliana: halafu anakufurahia kweli ananiambia kuwa wewe ni mpole sana na una sifa nzuri

Bianca: oh mama…mwambie nashukuru sana hata mimi namfurahia sana kama anaweza akakupa Amani na furaha niliyokuwa natamani niione ukipewa na mwanaume

Liliana: mama usijalli daddy ananipa vyote hivyo and he bought me a car

Bianca: (anashangaa huku anaweka mikono mdomoni) a Car?

Liliana: yes

Bianca: girl that is your husband

Liliana: I know mama

Bianca: iam so proud of him mwambie nimesema asante sana

Liliana: nitamwambia

Bianca: shoga sasa una magari mawili nigawie moja basi

Liliana: nitakupa lile la zamani

(Wanacheka)

Bianca: nakutania

Liliana: najua unanitania maana unayo ya kutosha

(Wanacheka)

Bianca: ah Liliana asante kwa kuja maishani mwanangu ona sasa nina shoga wa kupiga nae umbea

Liliana: mimi ndo niseme asante mama

Bianca: basi tuambiane

Liliana: hapo ndo sawa sasa

(Wanacheka)

Liliana: (Anakunywa maziwa kidogo) mama

Bianca: nambie mwanangu

Liliana: ungemkubalia mjomba tu tucheze harusi

Bianca: amekutuma?

(Wanacheka)

Liliana: hapana mama ila nahisi ni jambo zuri kumkubalia tu mfunge ndoa tucheze weeee mpaka basi

Bianca: kwani sijamkubalia?

Liliana: (anashangaa) umemkubalia lini?

Bianca: nakutania mwaya

Liliana: mkubalie bwana maana wote hamna wenza mngekuwa tu bwana mke na mume, mjomba wangu ni mchapakazi

Bianca: alikuwa anakubaka

Liliana: (anamuangalia mama yake) mama hayo ni ya kale

Bianca: siwezi kuyasahau

Liliana: nimeamua kumsamehe mama na nimeona nguvu ya msamaha nina Amani sina kinyongo moyo wangu hauumi kama ningeamua kukibeba kitu hicho

Bianca: (anakaa kimya)

Liliana: mama msamehe tu na uendelee na maisha kama hicho ndo kitu pekee kinachokufanya usimkubalie

Bianca: (anaguna) mtoto una maneno wewe

Liliana: (anacheka)

Bianca: au amekutuma?

Liliana: hapana

Bianca: ubaya siku hizi haongelei

Liliana: (anacheka) anaongelea sana tu mbona yaani kila tukikutana labda kwa chakula au tu stori huwa anakuambia ungemkubalia

Bianca: nina miaka 61 tayari nimeshazeeka

Liliana: mama love doesn’t know age boundaries

Bianca: na pia mjomba wako ni mdogo kwangu

Liliana: hamuonyeshi halafu age is just a number mama

Bianca: sawa ila

Liliana: usijinyime raha mama na furaha yako ipo njiani unaiona

Bianca: (anakaa kimya)

Liliana: nakwambia mama mpe nafasi mjomba mtakuwa wapendanao wazuri sana

Bianca: (anaguna)

Liliana: usijizue mama

Bianca: okay nitachukua ushauri wako

Liliana: (anafurahi sana) hayo ndo maneno mama… age is just a number

Bianca: mpaka aseme yeye

Liliana: atasema tu

Bianca: (anacheka) na wewe unajua kupangaa maneno

Liliaana: mimi nitafurahi sana nikisikia harusi yako na mjomba

Bianca: kama itakupendeza basi sawa mama

Liliana: (anafurahia sana)

Bianca: muone… (anamshika bega) usisahau kufurahi hivi mwanangu hata kama ukiwa unapitia magumu gani wewe jua tu Mungu yupo na anatupigania kazi yetu sisi ni kukaa kwa utulivu tukimtegemea yeye

Liliana: yes, mama

Bianca: keep on smiling my daughter

(Wanakumbatiana)

Liliana: oh mama (anamkumbatia)

Post a Comment

0 Comments