I KILLED MY LOVER 39

 


SCENE 39: -

CHUONI KWA KINA LILIANA: -

(Liliana anashuka kwneye gari lake jipya alilonunuliwa na mpenzi wake, anatumia funguo kufunga gari kisha kwa mwendo wa kujidai anatembea kuelekea darasani)

Liliana: (anapiga hatua chache)

Sauti: (kutokea nyuma yake) Liliana?

Liliana: (anageuka) oh Gervas

Gervas: naam umepotea sana na siku hizi huonekani kabisa

Liliana: mbona mimi nipo jamani?

Gervas: (anamfikia) I miss you (anataka kumkumbatia)

Liliana: (anasogea nyuma kama kukwepa Fulani hivi)

Gervas: lakini kwanini hunitaki Liliana?

Liliana: kwasababu nina mpenzi

Gervas: mpenzi yule anayelingana na baba yako au babu kabisa

Liliana: it doesn’t matter nampenda hivyohivyo age is just a number

Gervas: yule ni mume wa mtu

Liliana: yes, alikuwa ameoa ila mke na watoto wake wote wameshatangulia mbele za haki

Gervas: (anasikitika) siku moja utakuja kukumbuka maneno yangu ungekuwa na akili ungemfuatilia mapema huyo mwanaume...

Liliana: Gervas please kama humpendi Robert endelea kumchukia kimya kimya sio kuanza kusema unayoyasema

Gervas: wake up ni wewe tu ndo umelala kila mtu anaona kwa macho lengo lake ni kukuchezea

Liliana: nimekuambia acha

Gervas: nakupenda sana Liliana nitaumia sana nikisikia umeharibikiwa

Liliana: kuharibikiwa na nini? Kwani ni kosa kupenda?

Gervas: hapana sio kosa Liliana ila kosa ni kupenda sehemu ambayo sio sahihi

Liliana: na kwa Robert sio sehemu sahihi?

Gervas: kabisa

Liliana: nitavunga sijakusikia Gervas ila ukirudia nitasahau kwamba tuliwahi kuwa marafiki

Gervas: (anasikitika)

Liliana: sasa unasikitika nini?

Gervas: nakusikitikia wewe Liliana ambae kwa sababu ambazo sizijui unakataa kukubali ukweli juu ya hawara yako

Liliana: sio hawara yangu ni mpenzi wangu

Gervas: ni mume wa mtu yule

Liliana: unataka nini Gervas embu niambie mbona unapenda kuniumiza

Gervas: sikuumizi

Liliana: au kwasababu nilikukataa?

Gervas: hapana hiyo sio sababu nimekuwa nikikupenda kwa miaka sasa tangu hata bado hatujaanza chuo

Liliana: kwahiyo?

Gervas: nakutakia mema tu Liliana siku moja utayakumbuka maneno yangu

Liliana: niyakumbuke kwa lipi?

Gervas: yaishe

Liliana: please leave me alone jamani sitaki shida mimi na wewe na wala mtu yoyote nicheni niishi maisha yangu kwa Amani

Gervas: sijakugusa na wala sina mpango wa kukugusa nakushauri kama rafiki

Liliana: kama utaendelea kuniambia hivyo basi sitakuwa rafiki yako navunja urafiki na wewe

Gervas: sijui una nini? Umekuwaje Liliana mbona ulikuwa mtu mzuri sana huyo mwanaume amekufanya nini mbona kama umekuwa mjinga?

Liliana: umeanza kuniita mjinga?

Gervas: ona sasa yaani umekuwa sio muelewa

Liliana: ndo nimekuwa hivyo sasa embu niache sasa

Gervas: aisee

Liliana: excuse me

Gervas: Liliana nisamehe kama kuna sehemu nimekosea

Liliana: hujanikosea mimi umemkosea mpenzi wangu…mume wangu mtarajiwa

Gervas: mumeo mtarajiwa?

Liliana: ndio hujapenda?

Gervas: imenishangaza kidogo

Liliana: ndo hivyo…now if you don’t mind iam going to my class

Gervas: sawa masomo mema

Liliana: (anaondoka)

Gervas: (anabaki amebutwaa) mume mtarajiwa?

Post a Comment

0 Comments