I KILLED MY LOVER 40

 


SCENE 40: -

BAADA YA MWEZI MMOJA: -

NYUMBANI KWA BIANCA: -

(Majira ya saa nane mchana, jua linawaka kweli kweli na kwasababu hiyo watu mbali mbali wanapata vinywaji vya baridi kuyapa ahueni makoo yao yaliyokauka kwa sababu ya joto kali. Bianca yupo nyumbani kwake nae kama ilivyo kwa watu wengine nae anapata kinywaji chake cha baridi, wakati anaendelea kupata kinywaji chake Robert anafika mahali hapo)

Bianca: (anamuona) oh mkwe

Robert: (anatabasamu) habari yako mrembo?

Bianca: (anashangaa kidogo)

Robert: mbona unashangaa?

Bianca: Liliana hayupo

Robert: sijaja kumuona yeye nimekuja kukuona wewe

Bianca: kama umekuja kuongelea mahari umeshawahi kuoa na unajua taratibu

Robert: sijaja kwa ajili hiyo mrembo nimekuja kwa ajili yako

Bianca: (kwa mshangao) yangu?

Robert: yes, yako kwani vibaya

Bianca: sio vibaya ila inashangaza halafu acha kuniita mrembo

Robert: (anakaa) nakupenda sana Bianca

Bianca: (kwa ukali) wewe shika adabu yako

Robert: najua hata wewe unanipenda naonaga unavyoniangalia nikija hapa nyumbani

Bianca: wewe ni mpuuzi sana

Robert: tukana unavyoweza nimeshakuambia ninakupenda na ninataka kukuoa wewe na sio Liliana sijui hata unanielewa

Bianca: ni kwa bahati mbaya sana mwanangu anakupenda sana

Robert: mrembo acha kumuongelea Liliana tuoane mpenzi nitaondoka na wewe tutaenda mbali

Bianca: nina mwanaume tunatarajia kuoana lakini pili Liliana anakupenda na wala sipo tayari kuharibu uhusiano wangu na Liliana now get out now

Robert: unaolewa?

Bianca: ndio

Robert: utaolewa na mimi tu na sio na mtu mwingine

Bianca: you are crazy

Robert: yes, very crazy about you my love nipe nafasi mpenzi

Bianca: get out now

Robert: usiolewe Bianca

Bianca: naomba uniache tafadhali (anaita) Lupemba, Mbise

(Wanakuja)

Bianca: naomba mumuondoe huyu mwanaume humu ndani mara moja

Mbise: sawa aunt

Robert: msihangaike naondoka mwenyewe ila hatujamalizana (anaondoka)

Lupemba: Aunt kuna shida gani?

Bianca: (amekasirika sana) huyu mwanamume ni mtu wa ajabu sana

Lupemba: amefanya nini?

Bianca: naomba msimwambie Liliana tafadhali

Mbise: hatutamwambia

Bianca: amenitongoza ananiambia anataka kunioa

(Wanashangaa)

Lupemba: kumbe ni mtu mbaya ee

Bianca: sana

Mbise: maskini halafu Liliana anavyompenda

Bianca: simtaki tena maishani mwangu huyu mwanaume asije tena hapa

Lupemba: ni mpenzi wa Liliana na atakuja tu kwasababu ya mapenzi yao

Bianca: nitatafuta njia ya kumkataza Liliana

Liliana: (anafika mahali hapo)

Bianca: (anatulia) Mbise, Lupemba kaendeleeni na kazi zenu

Liliana: (anawakaribia)

Mbise: sawa aunt

lupemba: (anaongoza njia)

Mbise (bado amesimama hapo)

Liliana: (anakaa pembeni ya mama yake)

Bianca: (anatulia) Mbise, nimesema kaendeleeni na kazi zenu

(wanaondoka)

Liliana: vipi za hapa mama…shikamoo mama

Bianca: (anamkumbatia) marahaba mwanangu

Liliana: mama kuna jambo nataka kukuambia

Bianca: nini tena?

Liliana: mama iam pregnant…

Bianca: (anashangaa)what?

Liliana: yes, mama…iam pregnant

Bianca: Liliana kwanini umekuwa ni mjinga kiasi hicho

Liliana: (anashangaa) mama?

Bianca: Robert sio mwanaume mzuri

Liliana: mama Robert ananipenda sana na ni yeye ndo aliniambia anataka familia nyingine baada ya familia yake wote kufariki kwenye ajali mbaya

Bianca: im so disappointed with you Liliana haki ya Mungu sikutegemea hili

Liliana: mbona sikuelewi, mbona ulikuwa unafurahia?

Bianca: sitaki sasa… nimebadili mawazo

Liliana: mama

Bianca: (anatulia) haya mwambie kuwa una mimba

Liliana: (anamshangaa)

Bianca: iam sorry dear kuna mtu amenichanganya sasa hivi

Liliana: pole mama…naomba ufurahi maana unaenda kupata mjukuu

Bianca: asante mwanangu kwa habari hii

Liliana: okay mama najua Robert atafurahi sana akisikia hii habari

Bianca: asante haya kapumzike

Liliana: (anambusu mama yake shavuni kisha anaingia chumbani kwake)

Bianca: my child, umefanya nini mama…kumbebea mimba mwanamume mjinga kama Robert umefanya ujinga mkubwa sana mama hata sijui kwanini umefanya hivyo mama lakini ni kwasababu hujui mama ila najua utajua tu…(anakaa) utajua tu …kwamba huyu mwanaume ni BAD NEWS atatusababishia makubwa maana anataka kutugombanisha mwanangu na sitaruhusu hata kwa nini wewe ni mwanangu na utabaki kuwa kipenzi changu

Post a Comment

0 Comments