I KILLED MY LOVER 41

 


SCENE 41: -

NYUMBANI KWA ROBERT: -

(Liliana anafika nyumbani kwa Robert akiwa na furaha kubwa sana na yupo tayari kusema habari njema)

Liliana: (huku anaingia ndani) daddy

Robert: (hamfurahia) Robert

Liliana: (anashangaa)

Robert: sema shida yako maana sina muda mchafu wa kuona sura yako

Liliana: daddy jamani hayo matani yako siyataki

Robert: talk woman

Liliana: (anashangaa) jamani

Robert: (anakaa kimya)

Liliana: anyway, daddy nimekuja kukuambia kuwa nina ujauzito wako

Robert: nani amekuambia nataka mtoto

Liliana: (anashangaa) daddy ulisema kuwa unataka mtoto unataka familia mpya

Robert: nina familia mama…nina mke na watoto wanaishi Canada

Liliana: (anajikuta anaishiwa nguvu)

Robert: wewe ni takataka mbele ya mke wangu

Liliana: (anatokwa machozi) Robert ulinidanganya kuwa huna mke na watoto

Robert: akili tu niliitumia kukupata nilikubaka utotoni…siku ile usiku sijui ulikuwa unatoka wapi...ulinivutia sana kwahiyo nilitaka nikutumie tena ungekubali vipi kama ningekuambia kuwa nina mke na watoto

Liliana: (Analia) kumbe ni wewe ndo ulinifanyia yale utoto kumbe wewe ni yule mlinzi ndo maana sura yako haikuwa ngeni

Robert: (anakaa kimya)

Liliana: nimekusamehe…

Robert: sitaki unisamehe maana sikupendi nampenda Bianca

Liliana: mama yangu?

Robert: ndio…

Liliana: wewe ni mnyama

Robert: halafu tamu kuliko…mimi nimeathirika na wewe umeshaathirika…nimeathirika miaka mingi sana yaani hata mwanangu wa mwisho analingana na wewe nae ni muathirika

Liliana: (anachanganyikiwa)

Robert: nakuchukia sana Liliana

Liliana: nimekukosea nini?

Robert: hakuna ulichoniudhi…nilikuwa na wewe kisa nilimpenda Bianca sana na wewe ndo ulikuwa unaniunganisha nae…

Liliana: (anasikitika) mama anaenda kuolewa na mjomba

Robert: hiyo ndoa haitafika nipo radhi niue ila Bianca hataolewa na mtu na nipo radhi nimuache mke wangu Lydia nimuoe Bianca

Liliana: unampenda kiasi hicho?

Robert: nampenda sana

Liliana: (Analia sana)

Robert: you disguist me…yaani wewe ni mzuri tu ila hufai kuwa mke unafaa kuchezewa na kutupwa kama takataka

Liliana: aisee sikutegemea kusikia haya leo

Robert: ndo umesikia pasuka sasa

Liliana: it is not worthy it

Robert: ndo nimekuambia halafu huwezi amini nimesikia Amani ya ajabu nilipokuambia ukweli… (anamuonyesha picha za familia yake) huyu ni Gabriel, Michael na Raphael na mke wangu mpenzi Lydia wanaishi Canada huwa wanakuja mara kwa mara na ndo maana saa nyingine sitaki kuonana na wewe

Liliana: hongera sana

Robert: asante nakwambia haya ili huyo mtoto utafute njia ya kumtoa huyo mtoto

Liliana: subiri azaliwe umuue mwenyewe sipo tayari kubeba hii dhambi

Robert: utaitoa hiyo mimba hutoi?

Liliana: (anamkazia macho) simtoi…

Robert: hunijui

Liliana: utanifanya nini?

Robert: maskini nakuonea huruma umeshalia sana…ulikuwa unanipenda ee

Liliana: (Analia sana)

Robert: get out mke wangu atakuja muda sio mrefu akiondoka tu nakuja kwa Bianca wangu ni laizma nimuoe hata awe mke wa pili

Liliana: (anaondoka huku Analia sana)

Robert: (anacheka kwa dharau) mimi ndo Robert

Post a Comment

0 Comments