I KILLED MY LOVER 42

 


SCENE 42: -

NYUMBANI KWA BIANCA: -

MCHANA HUOHUO: -

(Liliana anaingia nyumbani kwao huku Analia kwa uchungu sana)

Bianca: (anamuona) Liliana…?

Liliana: mama (analia sana)

Bianca: vipi mwanangu (anaacha kumwagilizia maua yake) njoo mama shida nini mwanangu mrembo? Mbona unalia?

Liliana: (anamsogelea) Robert mama

Bianca: kafanyaje yule mwanaume?

Liliana: (anafuta machozi) ameniumiza sana…kwanza ameniambia kuwa ni mume wa mtu ana mke na watoto

Bianca: that bastard (anakasirika sana)

Liliana: cha pili ameniambia kuwa ameathirika na Virusi vya UKIMWI

Bianca: Jesus…(anasikitika) don’t worry child utaishi mwanangu utaishi mwanangu nakwambia kweli kabisa kuwa utaishi

Liliana: maisha yangu yameisha

Bianca: No ndo kwanza yanaanza mama…

Liliana: (analia sana)

Bianca: nyamaza mwanangu kwani wewe hujasikiaga kuwa kuna watu wanaishi na VVU kwa Zaidi ya miaka hata 30?

Liliana: (analia sana) mama

Bianca: achana nae

Liliana: (Analia sana)

Bianca: twende ndani mwanangu…hutakiwi kuwa na stress…

Liliana: mama Robert ameniambia kuwa hataki mtoto tena ana watoto watatu wanatosha

Bianca: achana nae

Liliana: bora angenilea mimi na mtoto

Bianca: nipo mimi…nitakulea mwanangu

Liliana: mama

Bianca: achana nae

Liliana: ameniumiza sana mama

Bianca: muache mama

Liliana: ameniambia kuwa anakupenda sana anataka kukuoa

Bianca: yule ni mshenzi amekuambia hivyo?

Liliana: ndio mama

Bianca: ni mjinga siwezi kuwa karibu na mtu aliyemuumiza mwanangu kwa vyovyote vile

Liliana: oh mama

Bianca: yule hana akili kama kukuacha si angekuacha kwa uzuri tu kuliko kukufanyia alivyokufanyia hana akili mjinga sana yule

Liliana: kwahiyo mama hutamkubali

Bianca: child, mimi sio mama mbaya naomba uelewe hilo mimi ni mama ninayekupenda kwa dhati kabisa mama

Liliana: (anafuta machozi)

Bianca: hata ingekuwa hivyo Robert hanivutii hata kidogo so relax my child

Liliana: (anashusha pumzi kuonyesha kuridhika kwa jibu hilo)

Liliana: kwahiyo mama nitajikuta namsahau Robert na haya yote yatakuwa mapito?

Bianca: yes, child…pole kwa haya yote mwanangu ni mapito yataisha tu…usijali utatulia tu

(Anna anafika walipo)

Liliana: oh cousin… (Anamkumbatia)

Anna: nini wewe una shida gani?

Liliana: nina stress

Bianca: (kwa Liliana) mama

Liliana: abee mama?

Bianca: nimekuambiaje?

Liliana: basi mama sitaongea tena mama

Bianca: (kwa tabasamu tulivu anamgeukia Anna) karibu mama

Anna: asante aunt

Bianca: baba yako yuko wapi?

Liliana: (anacheka) mama nilijua tu utamuulizia

Bianca: (anacheka kwa aibu kidogo) namuulizia tu kama nitakavyouulizia Bella (kwa Anna) eti Bella yuko wapi?

(Wanacheka)

Anna: atakuja baadae

Bianca: (anacheka)

Anna: hata hivyo sio mbaya sana baba na aunt ni wachumba

Bianca: (anacheka kwa aibu)

Liliana: nakumbuka hilo (anatabasamu) tuanze maandalizi ya harusi

Bianca: ni mapema sana bwana

Anna: wala hata sio mapema

Liliana: eti mapema…mama tuna miezi mitatu bado hatujafanya chochote sio shopping sio mpango wowote

Anna: wewe wasiwasi wako nini?

Bianca: si ndo hapo…embu naombeni mniache mzee mie

Liliana: eti mzee mama wewe sio mzee wewe ni forever 16

Bianca: hata mimi naona

(Wanacheka)

Bianca: (anamuangalia Liliana) afadhali unacheka mwanangu

Ana: kwani shida nini maana nauliza hata huniambii

Bianca: ah achana na hayo

Anna; (kwa Liliana) cousin?

Liliana: sijisikii kuongea sasa hivi cousin nitakuambia

Anna: okay sitawauliza tena ukijisikia kuniambia utaniambia

Liliana: usijali binamu by the way twende ndani tukale nina njaa

Bianca: (anacheka)

Liliana: mama? mbona unacheka?

Bianca: nimefurahi tu…unapenda kula sana

Liliana: (anacheka huku anaingia ndani)

Anna: (anamfuata ndani)

Bianca: ah mimi sitaendelea kukaa nje naingia ndani nikale mie

Mbise: nitamalizia kumwagilizia

Bianca: asante Mbise

Mbise: (anaendelea kumwagilizia maua)

Bianca: (anaingia ndani)

Post a Comment

0 Comments