SCENE 43: -
OFISINI KWA BIANCA: -
(Asubuhi tulivu tena yenye
kupendeza machoni kwa Bwana na wanadamu, Bianca akiwa ni mwenye tabasamu tulivu
anaingia ofisini kwake akiwa na lengo la kuianza siku yake kama ilivyo kawaida
yake)
Mfanya
usafi: (anamuona na kwa heshima
anamsalimia) aunt
Bianca:
hello
Mfanya
usafi: shikamoo aunt
Bianca:
(kwa upole na upendo) marahaba mama
hujambo mwanangu…
Mfanya
usafi: sijambo…umependeza sana aunt
Bianca:
nashukuru sana
Mfanya
usafi: (anatabasamu kidogo kisha
anaendelea na kazi zake)
Bianca:
(anaelekea ofisini kwake)
Mjomba:
(anatokea kwa nyuma yake) bibie
Bianca:
(anageuka taratibu huku anatabasamu)
oh vipi?
Mjomba:
umependeza sana…za asubuhi?
Bianca:
salama za mwamko?
Mjomba:
za mwamko nzuri mrembo wangu
Bianca:
(anatabasamu kwa aibu kidogo)
Mjomba:
basi cha kufanya wewe endelea na kazi tutaonana baadae mpenzi
Bianca:
(anatabasamu kisha anaelekea ofisini
kwake)
Mjomba:
(anatabasamu kidogo kisha anaelekea ofisini
kwake)
Bianca:
(anafika ofisini kwake anaweka mkoba
pembeni kisha anakaa kwenye kiti chake cha kuunguka) life is good…mwanangu
anatarajia kuniletea mjukuu na mimi natarajia kuolewa na mwanaume nimpendae (anacheka) Liliana amekuwa ni kiumbe cha
kuniletea bahati na ninajivunia kuwa mama yake nampenda mwanagu
(Mlango wake unagongwa)
Bianca:
pita mlango uko wazi
Robert:
(anaingia)
Bianca:
(tabasamu linaanza kupotea usoni mwake) Robert?
Robert:
yes, my queen…mbona umenuna ghafla hujafurahi kuniona hapa?
Bianca:
(anaghazabika sana) Liliana yupo
chuoni hayupo hapa
Robert:
unajua sijaja kwake nimekuja kwako (anamsogelea)
Bianca:
(ananyanyuka na kumkwepa) naomba
tuheshimiane
Robert:
kwanini unanichukia kiasi hicho?
Bianca:
sikuchukii na wala sikuwazii mabaya
Robert:
sasa mbona hupokei simu zangu na nikikuomba kuonana na wewe hutaki?
Bianca:
Robert ndugu yangu naomba uniache tafadhali
Robert:
nimeshaachana na mwanao kama unaona hicho ndo kikwazo…nimemuacha kwani
hajakuambia?
Bianca:
naomba haya mazungumzo yaishie hapa tafadhali naomba
Robert:
sitaondoka mpaka utakaponikubalia Bianca nakupenda sana you are so beautiful
lady nisaidie nakupenda nataka kuwa na wewe
Bianca:
siwezi kuwa na wewe
Robert:
kwanini?
Bianca:
kwanza nani amekuonyesha ofisini kwangu?
Robert:
hilo sio swali nililokuuliza mbona unanijibu swali juu ya swali?
Bianca:
okay naolewa na mchumba wangu hatapendezwa na mimi kuwa na mwanaume mwingine
Robert:
nani anakuoa Bianca…haki ya Mungu tena bianca sikudanganyi nitamuacha mke wangu
na kukuoa wewe mpenzi wangu
Bianca:
jamani sikutaki Robert una nini lakini? Una wazimu?
Robert:
ndio nina wazimu (anamkumbatia kwa nguvu)
Bianca:
(anamsukuma na kumzaba kibao cha nguvu)
tena ukome pumbavu sana
Robert:
(anashika shavu) nakupenda sana
Bianca ila usingenizaba kofi umekosea sana
Bianca:
get out…
Robert:
utalipa nakwambia
Bianca:
embu toka hapa…utanifanya nini?
Robert:
umekosea sana usingefanya hivyo nakwambia
Bianca:
ndo utanifanya nini? embu acha kunitishia mimi pesa zako hapa hata mimi nina
pesa…na usidhani eti kisa una pesa utapata kila kitu utakachotaka…mimi na
mwanangu sio bidhaa kwamba utatubadilisha pale utakapotaka
Robert:
sina mpango wa kukubadilisha Bianca
Bianca:
naomba utoke ofisini kwangu na isitokee hata siku moja umerudi hapa
Robert:
(anamkaribia na kumbusu kwa lazima)
Bianca:
(anamsukuma na kumpiga kibao kikubwa
Zaidi ya mwanzo)
Robert:
(anashikwa hasira mpaka macho yanakuwa
mekundu) umerudia tena
Bianca:
nitarudia mara nyingi Zaidi kama hutaondoka ofisini kwangu
Robert: (anamvuta
na kumlazimisha kumkumbatia)
Bianca:
(kwa kupayuka) security
Mjomba:
(anasikia sauti ya Bianca anakimbilia
ofisini kwa Bianca) nini?
Robert:
ondoka hayakuhusu huu ni ugomvi kati ya wapendanao
Mjomba:
wewe si Robert mkwe?
Robert:
nilikuwa sasa mimi ni baba yake Liliana
Mjomba:
una maana gani?
Robert:
mimi na Bianca tunapendana
Bianca:
sikutaki na wala sitaki kusikia upuuzi wako
Robert:
mbona unamuogopa huyu mzee ni nani yako?
Bianca:
huyu ni mchumba wangu na siku sio nyingi tutakuwa wanandoa naomba umheshimu
Robert:
Bianca seriously umeenda kumchukua huyu mzee mchafu mchafu unaniacha mimi
mwananume nadhifu tena mtanashati nina pesa zangu
Bianca:
(anacheka kwa kejeli) eti nadhifu…wewe
nadhifu? Basi kama ni hivyo baki na unadhifu wako niachie mimi mzee wangu
nimempenda mwenyewe na uchafu wake
Robert:
I love you and you know it
Bianca:
utaondoka mwenyewe au niite polisi?
Robert:
usihangaike nitaondoka mwenyewe sasa ila baadae nitarudi
Bianca:
hautakaribishwa
Robert:
tutaona…(anaondoka)
Bianca: (anakaa
kwenye kiti)
Mjomba:
inabidi ukapumzike
Bianca:
hapana nipo sawa
Mjomba:
(anamkumbatia mchumba wake kwa upendo)
nipo pamoja na wewe mpenzi mpaka mwisho usijali mama nipo na wewe
Bianca:
asante mpenzi wangu
(wanakumbatiana)
Mjomba:
haya nenda nyumbani bibie (anatabasamu)
kapumzike mke wangu
Bianca:
(anatabasamu kidogo anabeba mkoba wake na
kuondoka zake)
0 Comments