I KILLED MY LOVER 49

 


SCENE 49: -

NYUMBANI KWA ROBERT: -

USIKU: -

(Robert anatoka nje ya nyumba yake kwa lengo la kwenda sehemu Fulani maana amebeba ufunguo wa gari na anaelekea gari lake, wakati anapiga hatua anahisi kuna mtu anamuangalia kwa mbali)

Robert: (anageuka nyuma) nani?

Mtu: (kakaa kimya)

Robert: nani?

(Kimya)

Robert: (anapiga hatua)

Mtu: (anapiga hatua kumfuata)

Robert: nani?

Mtu: (anajitokeza na sio mwingine bali ni Liliana)

Robert: you?

Liliana: (anatabasamu)

Robert: unafanya nini hapa wewe mwanaharamu

Liliana: mwanaharamu ni wewe Robert (anacheka) usidhani nakuogopa yaani nitakuchoma visu kwanza ndo nikuchomee humu ndani

Robert: (anacheka sana) Oh My God yaani Liliana bado una mawazo ya kijinga? Eti kuniua mimi? Ona uliposimama yaani unaniogopa sana

Liliana: (anamsogelea) you think so? (anatabasamu) usiniambie

Robert: (anashangaa)

Liliana: nahesabu siku tu Robert ikifika tu arobaini ya mama yangu nakuua yaani nampa zawadi hiyo nitakuua kama ulivyomuua mama yangu

Robert: (kwa ujasiri) usiponiua Liliana nitakuua mimi Liliana

Liliana: deal?

Robert: done

(Wanakaziana macho)

Liliana: (anatabasamu kwa dharau)

Robert: (anacheka kwa dharau pia)

Liliana: nenda ulipokuwa unaenda

Robert: kila nikikutana na wewe ni lazima mambo yangu yaharibike

Liliana: yataharibika Zaidi na Zaidi subiria (anacheka sana) yataharibika utajuta

Robert: (anachukua simu na kutaka kupiga)

Liliana: unapigia polisi au wasichana wavivu ambao hawajui kutafuta pesa basi kwa ujinga huo wanajikuta wanalaghaiwa na wewe na kujiingiza kwenye matatizo?

Robert: (anaendelea kutafuta namba Fulani)

Liliana: (anamsogelea Zaidi na kumkazia macho) unaniogopa?

Robert: ah wapi

Liliana: kuna baridi mbona kama unatoka jasho?

Robert: this is none of your business

Liliana: ulichogundua ni kwamba mimi ni kifo chako yaani kila kitu chako kinahisi mimi ni kifo chako ndo maana unatetemeka (anacheka)

Robert: hunitishi

Liliana: really?

Robert: really

Liliana: haya sawa pigia simu huyo unayetaka aje akusaidie

Robert: siiti msaada naita dereva wangu

Liliana: hata huyo ni msaada fikiria tena na tena huwezi kuendesha gari umeniogopa ni bora uniogope hivihivi my dear maana nitakumaliza

Robert: nimeshakuambia kwamba hunitishi

Liliana: na mimi nimekuuliza really

Robert: nimejibu really

Liliana: haya bwana…tuendelee kuhesabu siku baba tutafika daddy

Robert: usiniite daddy

Liliana: utajijua (anacheka kisha anaondoka)

Robert: this woman (anabaki na hasira)

Liliana: nakukera acha nikukere (anacheka sana)

Robert: ananikera sana sijui katokea wapi

Liliana: (anacheka sana huku anatokomea gizani)

Rpbert: (anafyonza kisha anaingia kwenye gari) bastard…

Post a Comment

0 Comments