I KILLED MY LOVER 50

 


SCENE 50: -

BAADA YA SIKU 40: -

USIKU: -

(Usiku ulio mtulivu kabisa, kila kitu kimetulia kasoro wadudu wa usiku wanalia kwa sifa kumtukuza Muumba wao, Liliana akiwa amevaa nguo nyeusi tena amejifunika na kitambaa cheuzi usoni anaingia nyumbani kwa Robert)

Liliana: (anafika ndani hapo) ona linavyojiamini limeacha mlango wazi na nilijua tu kuwa linaachaga mlango wazi maana lina miadi na wanawake huyu mwanaume kweli hana akili mshenzi sana

Robert: (amelala chumbani kwake hana habari juu ya ujio wa Liliana)

Liliana: (anazima taa zote mpaka za nje) ni giza kwelikweli hapa sasa naweza kuanza kazi yangu (anatoa kisu na kumuendea Robert anaanza kumchoma kwa nguvu)

Robert: (anaamka kwa maumivu makubwa) jamani nani?

Liliana: (anawasha tochi ya simu yake) umeniona mimi ni kifo chako…

Robert: Liliana (anatoa macho) nisamehe

Liliana: ili uniue? Umesahau kuwa tuliambiana kuwa nisipokuua utaniua? No way baba lazima ufe (anamchoma kisu mfulululizo)

Robert: (Analia kwa maumivu makubwa kisha anakata roho)

Liliana: (anashusha pumzi kubwa sana sana kisha anacheka kwa nguvu) yes, I killed my lover…I killed him (anajikuta Analia ghafla) mama this is for you (anachukua dumu la mafuta kisha anamimina kila pande ya nyumba ile kisha anatoka anawasha kiberiti na kukitupia pale halafu kwa mwendo wa kasi sana anaondoka zake)

 

END OF FLASHBACK: -

(Liliana bado kasimama kizimbani anasimulia kisa kilichosababisha kumuua aliyekuwa hawara yake)

Liliana: ndo ilikuwa hivyo ni kweli nilimuua kwasababu ya hasira na uchungu hata hivyo alinikejeli na kunionyesha kuwa yeye ana nguvu hata serikalini

(watu wananong’ona wengine wanasikitika)

Raphael: (anasikitika sana)

Lydia: (anasikitika pia) yaani alikuwa yupo radhi aniache ili amuoe Bianca pamoja na shida na dhiki tulizopitia pamoja? Aisee huyu mwanaume hakutakiwa kubaki kwenye jamii yetu

Gabriel: daddy was my hero ila baada ya kusikia hii hadithi hapana alifanya vibaya

Michael: daddy why did you do this umemuumiza mtoto wa watu maskini aliishi kwa shida sana Mungu akampa mama aliyempenda kwa dhati kwa tamaa zako ukamuua umemkosea sana mtoto wa watu

Hakimu: (anashusha pumzi) aisee pole sana binti kwa hayo uliyopitia ila pamoja na yote Mungu atabaki kuwa Mungu kwa ukuu wake….

Liliana: asante sana mheshimiwa…nashukuru sana

Hakimu: (anakaa kimya kidogo) aisee hadithi inasisimua sana

Watu: sana aisee

Liliana: (amejiinamia kwa huzuni)

Hakimu: una umri gani?

Liliana: miaka 24

Hakimu: bado mdogo sana

Liliana: (anakaa kimya)

Hakimu: tuchukue mapumziko kidogo kisha tutarudi kusikiliza hukumu

(Watu wananyanyuka na kwenda nje)

Liliana: (kwa unyonge anatoka kizimbani na kushuka walipo binamu zake)

Anna: Liliana

Liliana: (machozi yanamtoka) nilifanya yale kwasababu ya hasira na pia niliona kuwa Robert hakufaa kuishi kwenye jamii ila kumbe nilikuwa nakosea ningejua ningeiachia sheria ifuate mkondo wake

Bella: basi binamu usilie yameshatokea

Liliana: nitapokea hukumu nitakayopewa kwa mikono miwili na ndo ninayostahili

Bella: (anasikitika sana)

Raphael: (anamuangalia Liliana sana)

Gabriel: (kwa sauti ya kunong’ona) dogo sikuelewi what is wrong are you in love with our father’s killer

Raphael: umeisikia vizuri hiyo hadithi? Nani aliyemfanya mwenzie afanye hilo?

Gabriel: (anakaa kimya)

Raphael: inaonekana hujasikiliza hadithi vizuri ametusimulia kwa upana na tumemsikia na kumuelewa tumejua kwanini alichoma nyumba na kumuua baba yetu, mama yake aliuawa kinyama alilipa kisasa

Lydia: baba yenu alinikosea sana

Michael: (anasikitika sana) yaani baba alichofanya kwanza alitukana kisha akataka kutukataa kwakweli dah

Lydia: ndo hivyo... (anaangalia mlangoni) naona watu wanarudi

Raphael: (anamuangalia Liliana)

Gabriel: basi nenda ukamuangalie vizuri maana naona una dukuduku kweli yaani

Raphael: (anaenda alipo Liliana) Liliana habari yako?

Liliana: (anamgeukia) abee salama… (anampa mkono) nani vile?

Raphael: Raphael

Liliana: nambie

Raphael: ah sina la kusema sana nimekuja kukusalimia tu

Liliana: nashukuru sana (anatabasamu kidogo)

Hakimu: (anaingia)

(Watu wanakaa kimya kisha wanasimama kwa heshima)

Hakimu: (anakaa)

Watu: (wanakaa pia)

Hakimu: habari za muda tena?

Watu: (wanaitikia)

Anna: (anaonekana kuwa na wasiwasi sana)

Bella: (Analia maana anatambua kuwa binamu yake anafungwa)

Anna: eeh Mungu…

Hakimu: basi kutokana na hadithi hiyo ya kuhuzunisha tumejua kwanini binti alifanya unyama ule (anakaa kimya kidogo) hata hivyo hakupaswa kujichukulia sheria mkononi angeiamini sheria na ingemsaidia hivyo anahukumiwa kifungo cha miaka saba jela na kazi ngumu (anagonga meza) basi tumeishia hapa (ananyanyuka na kuondoka)

Anna: (anaangua kilio)

Raphael: (anasikitika sana)

Liliana: (anatabasamu)

Askari: (anamchukua Liliana) twende binti (anamuangalia kwa huruma) hata hivyo umeishi maisha magumu sana Mungu akusaidie mwisho wako uwe mzuri uwe na familia na kadhalika miaka saba sio mingi na pia ukiwa na tabia njema utatoka mapema

Liliana: sawa

Anna: Liliana my cousin (anamkubatia huku Analia sana)

Raphael: (anakuja walipo Liliana na binamu zake) iam so sorry

Liliana: (anatabasamu) it is okay (anamfuata askari magereza)

Gabriel: maskini…yeye furaha yake iko wapi? (anasikitika sana)

Raphael: aisee (anasikitika sana)

Lydia: (hasemi kitu amekaa kimya tu)

(Watu wanatawanyika huku wengi wao wanaonekana kuwa na huzuni sana)

Post a Comment

0 Comments