I KILLED MY LOVER 51

 


SCENE 51: -

NYUMBA NDOGO YA ROBERT: -

(Lydia amekaa na watoto wake wakizungumza mambo mbalimbali ya maisha ikiwemo ya marehemu Robert)

Lydia: lililotuleta limeisha sasa turudi Canada

Raphael: sirudi Canada mama

Lydia: what do you mean?

Raphael: namaanisha sirudi Canada

Lydia: vipi kuhusu kazi yako?

Raphael: nitapata kazi nyingine huku

Gabriel: una shida gani kwanini hurudi Canada?

Raphael: nataka nianze kuishi maisha yangu nimeshakuwa mkubwa nina miaka 26 sasa sitaki kuwa chini ya mtu yeyote najua mimi ni last born wenu naomba msinibebe hivyo milele

Michael: are you in love?

Raphael: (kimya kidogo)

Lydia: (kwa hasira) kaka yako anakuuliza mbona hujibu?

Gabriel: mama please…yeye sio mtoto tena ana haki ya maamuzi yoyote

Lydia: najua anayempenda

Michael: kama unamjua basi ni vizuri

Raphael: yes, iam in love with Liliana

Lydia: huwezi kushare na baba yako

Raphael: nampenda

Lydia: she is H.I.V positive

Raphael: hata mimi mama…hata mimi ni muathirika usisahau hilo mama

Lydia: (anamuangalia kwa hasira) nakuambia achana na huyo mwanamke

Raphael: no mama iam so sorry

Lydia: utamuitaje huyo mwanae Raphael mwanangu huu uhusiano hauwezekani

Raphael: I will make it possible mama

Lydia: hatakukubali

Raphael: I don’t care nitafanya kila kitu mpaka anielewe I will not give up mpaka nimpate kipenzi cha moyo wangu I love her mama

Lydia: nendeni mkaandae mabegi iam booking flight tunaondoka

Raphael: mtaenda without me nanunua nyumba

Michael: bro, she is in jail now

Raphael: I will wait for her

Lydia: seven years?

Raphael: hata kama ingekuwa kumi

Gabriel: aisee inasikitisha sasa amekukubali?

Raphael: I don’t care atanikubali tu nitapambana mpaka nimpate yeye ni kila kitu I want her to be my wife

Lydia: be careful young man usione nimenyamaza ukadhani nafurahia

Raphael: iam so sorry mama ila rudi Canada peke yako au na kaka zangu

Gabriel: iam not going back either

Lydia: usiniambie you are also in love

Gabriel: yes

Lydia: (anashangaa) na nani?

Gabriel: with the country

Michael: iam not going back too

Lydia: mna matatizo gani?

Gabriel: baba alitaka tuje huku

Michael: alitaka kutufata

Gabriel: mara ya mwisho alisema tuje huku

Lydia: okay enough… (anakaa kimya) hata mimi sirudi Canada

(Wanashangilia)

Lydia: ila upuuzi wako wewe Raphael sijauafiki

Raphael: I said iam sorry mama

Lydia: siafiki

Gabriel: mama Raphael huyu si unamjua? Hakuwahi kuwa na girlfriend sijui alikuwa anaogopa nini…muachie aenjoi first experience yake

(Michael na Gabriel wanacheka)

Lydia: it is not funny…unadhani atamuitaje yule mtoto

Gabriel: wherever mama amuite kaka, ba mdogo vyovyote mama ni sawa tu

Lydia: no…no..no ana bahati mbaya huyo mara wazazi wake wamekufa haya na huyo Bianca nae kafa unataka kwenda kufa mwanangu?

Raphael: sifi mama nitaishi vizuri sana

Lydia: hapana I don’t trust that girl itakuwa amezaliwa na mikosi

Raphael: ipi mama?

Lydia: kila anayemsogelea anakufa…nyie itafakarini hadithi yake

Raphael: she deserves to be happy mama hata yeye ni mtu

Lydia: sijakataa kwamba yeye sio mtu

Gabriel: bali?

Lydia: sitaki aisogelee familia yangu tena

Michael: too late mama, last born wako ameshamuangukia

(Wanacheka)

Lydia: sasa mnacheka nini?

Gabriel: kesho tukamuone

Lydia: nani?

Michael: mkwe wako

Lydia: over my dead body

Gabriel: relax

Lydia: (ananyanyuka na kuondoka kwa hasira)

Raphael: (anataka kumfuata)

Gabriel: Rapha muache

Michael: rudi ukae anahitaji kutulia kwanza we can understand her

Raphael: (anakaa kimya)

Gabriel: wewe kama umempenda basi kuwa nae tu fight for her

Michael: we will support you don’t worry sawa ee

Raphael: sawa brothers nashukuru sana

Gabriel: relax sawa ee

Raphael: (ananyanyuka) ngoja nikapumzike

Gabriel: okay brother

Raphael: (anaondoka kuelekea chumbani)

Post a Comment

0 Comments