I KILLED MY LOVER 52

 


SCENE 52: -

GEREZANI: -

(Liliana yupo gerezani akimnyonyesha mwanae anaonekana hana wasiwasi wala huzuni kuhusu hayo yote yanayotokea kwake)

Mmoja wa wafungwa: (anakuja alipo) wewe mpole sana…

Liliana: (anacheka) ila muuaji

Mfungwa: hapana sio hivyo bwana ulikuwa na maana yako yule askari ametusimulia yaani tumekuonea huruma

Liliana: (anacheka)

Mfungwa: mwanao mzuri…anaitwa nani?

Liliana: anaitwa Bianca

Mfungwa: mama yako wa pili?

Liliana: (anaitikia kwa kichwa ishara ya kukubali)

Mfungwa: naitwa Mage

Liliana: mimi naitwa Liliana au mama Bianca

Mage: safi sana shoga yangu

Liliana: (anatabasamu)

Askari: (anakuja) mama Bianca

Liliana: abee

Askari: kuna wageni wako wanakuita

Liliana: oh sawa (ananyanyuka na kuelekea nje)

(Nje kuna Raphael, Anna, Bella, Gabriel na Michael)

Liliana: (anafurahi kuwaona) mmekuja?

Anna: (anamchukua mtoto kutoka kwa Liliana)

Liliana: jamani karibuni

Raphael: (anatabasamu anapomuona Liliana anatabasamu)

Liliana: karibuni mkae

(Wanakaa)

Liliana: (kwa watoto wa Robert) bora mmekuja nataka niombe msamaha kwa yale yaliyotokea najua mmenichukia sana

Raphael: (anatabasamu)

Gabriel: usijali Lily hayo yamepita labda sisi kwa nafasi hii tukuombe radhi kwa yale yote uliyopitia tena yaliyosababishwa na mzee wetu najua asingefanya hivyo wala na wewe usingefanya hivyo

Liliana: (anaonekana kuridhika na jibu la Gabriel) asante kaka

Gabriel: Gabriel

Michael: na mimi naitwa Michael na huyu (anamshika Raphael bega) mdogo wetu wa mwisho anaitwa Raphael hajaoa wala nini ni mchapakazi ni mfanyabiashara mzuri pia

Gabriel: (anacheka) jamaa hili umeulizwa kwani?

Raphael: (anacheka kwa aibu)

Liliana: (anatabasamu) nafurahi kuwafahamu

Raphael: (anamchukua mtoto kutoka kwa Anna)

Gabriel: (anamchungulia mtoto) aaaawh katoto karembo

Liliana: kama bibi yake

(Wanacheka)

Liliana: (tabasamu linapotea ghafla)

Raphael: vipi mbona tabasamu limepotea

Liliana: bado kidonda kibichi moyoni mwangu namkumbuka sana mama yangu kipenzi mama aliyenilea kwa upendo mkubwa alinipa kila kitu leo hayupo (Analia)

Bella: lakini binamu hatujaja ili tuone machozi yako tumekuja ili tuone tabasamu la matumaini na sio huzuni

Liliana: (anafuta machozi)

Raphael: (anatoa kitambaa kutoka mfukoni na kumpatia Liliana)

 Liliana: (anapokea kisha anajifuta machozi) asante

Anna: (anamuangalia Raphael) kijana anaonekana ame…

Liliana: wala unaangalia vibaya

Bella; haya yetu macho

(Wanacheka)

Gabriel: sikujua nyie wadada ni watabiri wazuri wanasema lisemalo lipo kama halipo linakuja hili sasa sijui lipo au linakuja ndo Raphael utuambie

Liliana: (anacheka kwa aibu)

Raphael: (anacheka kwa aibu pia)

Bella: oyooooo hapa naona mambo mazuri sana

Liliana: kivipi?

Michael: anyways tungependa kuangalia mazingira ya magereza hii inavutia sana (kwa Gabriel, Anna na Bella) twendeni tukatembee kidogo

Kichanga: (kinalia)

Gabriel: (kwa Raphael) mpe Liliana mtoto

Liliana: (anamchukua na kumnyonyesha)

Gabriel: haya sisi tupo huku

(Wanaondoka na kuwaacha Raphael na Liliana peke yao)

Raphael: (anakohoa kidogo)

Liliana: (anamuangalia)

Raphael: ah (anashikwa na kigugumizi)

Liliana: vipi?

Raphael: najua sio muda muafaka wa kuongea haya mazungumzo ila siwezi kusubiri tena

Liliana: unazungumzia nini Raphael?

Raphael: ah naomba uniruhusu niwe baba yake Bianca na baba wa familia yako

Liliana: (anashtuka kidogo) me?

Raphael: yes, you Liliana

Liliana: how is that possible?

Raphael: what do you mean?

Liliana: iam your father’s killer

Raphael: I know lakini pamoja na hayo I want to give you family labda Mungu alitaka uitengeneze familia mwenyewe

Liliana: mimi nimlaaniwa kila atakayenisogelea basi ataumia au kufa

Raphael: hapana sio kweli Liliana naomba nafasi utaona mambo yatakavyokuwa

Liliana: (anaguna) I don’t know

Raphael: please think about it I wont rush you

Liliana: mimi sikufai

Raphael: nani kasema?

Liliana: (anatikisa kichwa)

Raphael: think about it (anambusu kwenye paji la uso kisha anambusu kichanga halafu anaondoka zake)

Liliana: (anabaki na maswali mengi sana) nini tena hii? Yaani nitembee na baba mtu na mtoto? Nahisi sio vizuri lakini pia mimi ni muathirika nitamuua mtoto wa watu (anaendelea kujiuliza maswali mengi sana)

Post a Comment

0 Comments