I KILLED MY LOVER 53

 


SCENE 53: -

BAADA YA MIEZI MITATU: -

GEREZANI: -

(Raphael anafika magereza ambapo imekuwa ni kawaida yake kufika mahali hapo kila siku kumuona Liliana)

Raphael: (anaketi mara baada ya kumuona Liliana) unaendeleaje my love?

Liliana: naendelea vizuri

Raphael: umeshakunywa dawa baby?

Liliana: ndio tayari wewe je?

Raphael: mapema sana

Liliana: (anatabasamu)

Raphael: vipi Bianca yuko wapi?

Liliana: bado amelala

Raphael: (anacheka kidogo) leo bibie vipi kalala mpaka sasa hivi

Lilana: (anacheka) ukorofi tu hana lolote

Raphael: (anacheka kisha anakaa kimya kwa muda huku macho yake yanamtazama Liliana)

Liliana: (anatabasamu) mbona unaiangalia sana?

Raphael: asante

Liliana: ya nini?

Raphael: kila kitu

Liliana: oh My God Rapha

Raphael: what? (anatabasamu) asante kwa kunikubali maana nimetumia miezi miwili kuomba unikubali niwe mpenzi wako

Liliana: na ulikomaa (anacheka) mimi nilikuambia ya kwamba siwezi kuwa na wewe maana tayari niliwahi kuwa na baba yako na pili ni muathirika…lakini hata hukuogopa

Raphel: unajua funny fact ya mapenzi ni kwamba hayachagui I mean moyo ndo huwa hauchagui nani wa kumuangukia nilikuangukia tangu siku ya kwanza nakuona pamoja na kwamba wewe ni muuaji wa baba yangu bado tu nilihitaji kuwa na wewe

Liliana: (anacheka) yaani wewe

Raphael: ulipohukumiwa nilimuambia mama yangu juu ya hisia zangu kwako alikataa na wala sikujali nikakomaa na wewe kwasababu tayari nilikuwa nimekupenda sana sikuwa nimesikia la mtu kaka zangu tu ndo walikuwa wamenichukulia mimi na ujinga wangu

Liliana: (anacheka) umenifanya mwenzio nimetukanwa na mama yako

Raphael: (anashangaa) usiniambie mama yangu alikutukana

Liliana: ila yameisha huwezi kuamini mara ya mwisho kabisa ameniambia kuwa anatuacha tu tuwe na kwamba amenikubali hata siku nikitoka kifungoni nitakaribishwa nyumbani kwenu

Raphael: oh My God (anafurahi sana) nafurahi sana baby…tutafunga ndoa mapema tu ukitoka

Liliana: mwaka gani?

Raphael: hata ikiwa baada ya miaka mia sawa tu

Liliana: lakini Rapha

Raphael: I swear

Liliana: (anacheka kwa aibu)

Raphael: (anashika mikono ya mpenzi wake na kuibusu)

Liliana: asante kwa kunipenda

Raphael: unanipenda?

Liliana: (anacheka) nakupenda ndio

Raphael: ila sio Zaidi yangu

Liliana: nakupenda sana baby

Raphael: (anatabasamu) asante mama watoto wangu

Liliana: (anacheka)

Raphael: by the way baby…nimeshafungua ofisi, nimenunua nyumba

Liliana: ndani ya miezi mitatu hiyo?

Raphael: nilikuwa na hela kwenye akiba zangu…pesa nyingi tu na pia kwenye urithi wa baba mama ametugaia so hiyo imenipa nafasi ya kufanya yote hayo

Liliana: hongera sana

Raphael: ukitoka tu tutafunga ndoa

Liliana: baada ya miaka saba?

Raphael: ndio au nitaomba kama itawezekana nifunge ndoa na wewe ukiwa humu

Liliana: sidhani kama watakubali

Raphel: tutawauliza

Liliana: (anacheka)

Raphael: by the way nimekuja na chakula chako ukipendacho sana

Liliana: umejuaje kuwa nina njaa?

Raphael: nimehisi tu maana hata mimi nina njaa nikaona kabla sijaingia ofisini nipite hapa nile na wewe kisha niende kazini

Liliana: (bila kutegemea anambusu mpenzi wake mdomoni)

Raaphael: (anashangaa) wow thank you (anambusu pia)

Liliana: (anacheka)

Raphael: (anacheka) haya kula darling

Liliana: (anaanza kula)

Raphael: (anakula huku anamuangalia mpenzi wake)

Liliana: wewe mbona unaniangalia sana unataka kunikariri?

Raphael: hapana nashangaa tu uzuri wako

Liliana: (anacheka huku anatikisa kichwa)

Raphael: ni nini baby? Mbona unatikisa kichwa?

Askari: (anawaangalia kisha anacheka)

Raphael: (anafurahi sana)

Liliana: kula uende ofisini

Raphael: mimi ndo boss nikitaka sitaenda

Liliana: kwani tayari umeweka na wafanyakazi?

Raphael: lazima niwe nao kazi zangu sio rahisi kufanya mwenyewe

Liliana: I can imagine

Raphael: ndo uimagine sasa

(Wanacheka)

Liliana: (anamaliza kula) haya mie nimemaliza naomba na wewe umalizie uende kazini

Raphael: nimeshamaliza hata hivyo (anakusanya mifuko waliyotumia)

Liliana: acha nikatupe (anaenda kutupa)

Raphael: haya mie naenda nilikuja kukuona tu kidogo kupata kifungua kinywa nawe baadae nitakuja tupate chakula cha mchana pamoja

Liliana: asante

(Wanakumbatiana)

Raphael: (anambusu kisha anaondoka zake)

Liliana: (anarudi gerezani)

Post a Comment

0 Comments