I KILLED MY LOVER 54

 


SCENE 54: -

USIKU: -

GEREZANI: -

(Usiku mtulivu sana nje kuna upepo mwanana unavuma huku miti nayo inaukubali upepo ule na taratibu inayumba kwa madaha huku ikimtukuza Mungu, Liliana amelala usingizi wenye utulivu na hapo anaota njonzi)

(Ndoto)

Bianca: (marehemu anakuja namnyanyua Liliana kichwa na kukiweka kwenye mapaja yake kama kumpakata)

Liliana: (anamuona) mama? (anafurahi sana)

Bianca: (anafurahi sana) abee mwanangu

Liliana: umekuja?

Bianca: sijaja peke yangu nimekuja na mama yako

Liliana: mama yangu?

Bianca: (anatabasamu)

Mama mzazi: mwanangu

Liliana: (anafurahi kumuona mama yake) mmekutana huko?

Mama: ndio mwanangu na nimemshukuru kwa kukulea vizuri na kukupenda

Liliana: (anafurahi) nimewakumbuka

Bianca: pole sana liliana…pole hata kwa hili unalopitia (anaonekana kuwa na huzuni) ni mimi ndo nimekusababishia mpaka leo upo hapa

Liliana: (anakaa maana alikuwa amelalia mapaja ya Bianca) hapana mama nilimuadhibu Robert kwa lile alilokufanyia mama

Mama: (anatabasamu)

Bianca: hata hivyo sijaja kulia hapa nimekuja kukuambia ni wakati wako wa kufurahia maisha Liliana hautawahi kuja kuteseka kama ulivyoteseka maisha yako yote

Liliana: (anamuangalia mama yake mzazi) nataka niende na nyie

Bianca: ili iweje mama? Bianca utamuachia nani? Vipi kuhusu mpenzi wako? Wote hao wanakuhitaji (anamshika bega) hata jela hautakaa sana mama utatoka

Liliana: (anakaa kimya)

Mama: vipi unawaza nini?

Liliana: namuwaza Raphael

Bianca: amefanya nini?

Liliana: ananipenda kweli

Bianca: anakupenda kweli na wala sio utani yule kijana ndo sababu ya furaha yako mwanangu

Liliana: kwahiyo nimuamini?

Bianca: kabisa

Mama: muamini mwanangu wewe na yule kijana mtajenga familia nzuri yenye upendo utasahau maisha yako ya zamani utasahau uchungu ambao maisha yamekupitisha mwanangu utakuwa ni mwenye furaha

Liliana: kweli mama?

Bianca: kabisa

Mama: acha kuhuzunika kuwa na furaha maana huu ni mwanzo mama furaha yako iko mbele inakuja utaifurahi sana

Liliana: asante mama

Bianca: tunakupenda sana mwanetu

Liliana: nawapenda sana mama

(Bianca na mama wanatoweka)

Liliana: (anashtuka kutoka usingizini)

Mage: (amelala pembeni yake) vipi mwenzetu umeota ndoto mbaya?

Liliana: hapana Mage ile ilikuwa sio ndoto ilikuwa kabisa naongea nao

Mage: kina nani?

Liliana: mama zangu

Mage: mama zako? Kina nani?

Liliana: mama yangu mzazi na Bianca

Mage: umewakumbuka tu unawaza sana

Liliana: hapana walikuja kabisa wamenipa moyo kuwa ni wakati wangu wa kufurahia maisha

Mage: ni ndoto hiyo

Liliana: unadhani sitafurahi maisha tena?

Mage: hapana rafiki yangu sio kwamba hautafurahia maisha nilichomaanisha haiwezekani mtu aliyekufa akaja tena mkaongea

Liliana: (anaguna) basi itakuwa ndoto

Mage: eeh lala

Liliana: (anajifunika shuka huku anajisemea moyoni) iwe ndoto isiwe ndoto nachojua ni kwamba nimefurahi sana kuwaona tena (anatabasamu)

Kichanga: (kimelala fofofo)

Post a Comment

0 Comments